Saturday, August 31, 2013

HII NDIO PENALTI YA 'KIZEMBE' ZAIDI ILIYOIGHARIMU CHELSEA KWENYE SUPER CUP...


    
Hii ndio penalti ya 'kizembe' zaidi katika mechi kubwa iliyopigwa na Romelu Lukaku ambayo iliigharimu timu ya Chelsea ya England na kujikuta ikishuhudia Bayern Munich ya Ujerumani ikibeba Super Cup jana mjini Prague. Katika mechi hiyo ambayo Chelsea ilionekana kama ingeibuka na ushindi, timu zote zimaliza dakika 120 kwa sare ya 2-2 wakati Wajerumani hao wakisawazisha mara mbili huku bao la pili likifungwa na Martinez zikiwa zimesalia sekunde mbili za muda wa ziada. Jambo la kufurahisha ni kwamba mabao yote ya Chelsea yalifungwa kwenye lango moja na yale ya Bayern yakifungwa kwenye lango jingine.

MKE ADUNDWA NA KUTIMULIWA KWA KUASI KANISA ANALOSALI MUMEWE...

Biblia Takatifu.
Bila  yeye mwenyewe  kutarajia,  mke wa  ndoa  amejikuta  akicharazwa bakora na kutimuliwa  nyumbani  na  mumewe baada ya  mama  huyo kuacha kuabudu katika  madhehebu  ya Katoliki  alikofunga  ndoa  na mumewe  aitwaye Martin Kikondo (50) na kuamua kubatizwa  na kuanza kusali  katika  Kanisa  la Assemblies (EAGT).

KIONGOZI WA DHEHEBU LA WANAOKULA NYAMA ZA BINADAMU AUAWA NA WANAKIJIJI...

Kiongozi huyo, Stephen Tari akiwa hoi kwa kipigo kutoka kwa wanakijiji.
Kiongozi mmoja wa madhehebu ya wanaokula nyama za watu akijiita Yesu Mweusi, ambaye aliwachinja wafuasi wake wa kike wanaojulikana kama 'Flower Girl' na kunywa damu yao, amejiua mwenyewe kwenye misitu minene ya Papua New Guinea.

JICHO LA TATU...


PACHA ALIYETENGANISHWA MUHIMBILI ASUBIRI KUTENGENEZEWA NJIA YA HAJA KUBWA...

Madaktari wakifanya upasuaji katika Hospitali ya Muhimbili.
Saa 24 mara baada ya upasuaji wa kuwatenganisha watoto mapacha waliokuwa wameungana uliofanywa na jopo la madaktari bingwa saba, kutoka Hospitali ya Muhimbili (MNH) na Taasisi ya Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu na Mifupa (MOI), Dar es Salaam, mtoto mlengwa wa upasuaji huo ameonesha maendeleo mazuri na sasa ameanza kunyonya bila ya usumbufu.

ADHABU YA DOKTA WA PAKISTANI ALIYESAIDIA WAMAREKANI KUMNASA OSAMA YATENGULIWA...

Daktari Shakil Afridi (kulia) aliendesha programu ya chanjo mbele ya makazi ya Osama (pichani kushoto).
Daktari wa Pakistani ambaye alisifiwa kama shujaa baada ya kuwasaidia CIA kumsaka Osama bin Laden amefutiwa hukumu yake ya kifungo cha miaka 33 jela kwa uhaini.

Thursday, August 29, 2013

TAARIFA YA MSIBA...

*********************************
*********************************
MAMA NJILIMA AMETUTOKA!! 
Familia ya Mzee Duncan Njilima wa Ubungo N.H inasikitika kutangaza kifo cha mama yao kipenzi, (mama wa Wendy, Janet, Masunga, Bruce na Mandago) kilichotokea leo asubuhi baada ya kuugua kwa muda mfupi. Msiba na mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwao kota za Ubungo N.H jirani na Hoteli za Sharon na Whitemark. Bwana ametoa, Bwana ametwaa, Jina lake libarikiwe. Amina.
*********************************
********************************* 

'KIPANYA' CHAJIBAMIZA KWENYE LORI LA MIZIGO NA KUUA WATU 13...

Kamanda Kihenya Kihenya.
Watu 13 wamekufa katika ajali ya gari ya Toyota Hiace kugonga gari la mizigo lililokuwa limeharibika barabarani katika kijiji cha Ngogwa wilayani hapa.

UTALII HUU HAKIKA INATAKA MOYO WA KIPEKEE...

Watalii wakiendelea kutazama simba hao wenye uchu.
Ni karibu kuliko watu walio wengi wangeweza kutamani kuingia kwenye kundi la simba wenye njaa.

WAKUU WAHOFIA NCHI KUTAWALIWA NA WAGENI...

Abbas Kandoro.
Wakuu wa mikoa na wilaya nchini wana hofu nchi kutawaliwa na wageni endapo baadhi ya vipengele katika Rasimu ya katiba havitabadilishwa.

JICHO LA TATU...


KIBAKA AJIFYEKA MIKONO YOTE BAADA YA KUCHOSHWA NA TABIA YA WIZI...

Ali Afifi.
Mwanaume mmoja raia wa Misri amefyeka mikono yake yote miwili kwa kuitega kwenye njia ya treni iendayo kasi ili kukomesha wizi wake uliokithiri.

WAHAMIAJI HARAMU 21,192 KUTOKA MIKOA MITATU WAONDOKA NCHINI...

Wahamiaji haramu.
Wahamiaji haramu 21,192 kutoka mikoa mitatu nchini, wameondoka kwa hiari yao kurejea kwao  katika kipindi cha mwezi mmoja tangu Serikali itoe agizo la kutaka waondoke.

Wednesday, August 28, 2013

MAPACHA WALIOUNGANA VIUNONI KUTENGANISHWA KESHO MUHIMBILI...

Chumba cha upasuaji.
Upasuaji wa kutenganisha watoto wawili waliozaliwa wameungana viunoni, unatarajiwa kufanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

WAFANYAKAZI 1,067 WATIMULIWA TAZARA KWA KUSHIRIKI MGOMO...

Baadhi ya abiria waliokuwa wakitarajia kusafiri kwa treni ya TAZARA wakiwa hawajui hatima yao kufuatia mgomo wa wafanyakazi wa shirika hilo jana.
Wafanyakazi 1,067  wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania  na Zambia (TAZARA), wamefukuzwa kazi mara moja kuanzia jana.

JICHO LA TATU...


WATANZANIA 247 WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA...

Baadhi ya dawa za kulevya zilizokamatwa hapa nchini.
Watanzania 247 wamekamatwa katika nchi mbalimbali duniani na wanashikiliwa kwa tuhuma za kukutwa wakisafirisha dawa za kulevya.

Tuesday, August 27, 2013

'BOMU' KANISA LA KKKT KIJITONYAMA NI KIFAA CHA HALI YA HEWA...

Kamanda Suleiman Kova.
Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imebaini kuwa chombo kilichodhaniwa kuwa bomu katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama hakikuwa bomu, bali ni kifaa cha Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) cha kuchunguza anga.

JICHO LA TATU...


MJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI ATIMULIWA CCM...

Nape Nnauye.
Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM imeridhia kuvuliwa uanachama kwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Kiembesamaki, Mansoor Yussuf Himid kama ilivyopendekezwa na Halmashauri Kuu ya chama hicho Mkoa wa Magharibi Zanzibar.

Monday, August 26, 2013

VIONGOZI SASA KUPEKULIWA KAMA ABIRIA WENGINE UWANJA WA NDEGE...

KULIA: Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dar es Salaam. KUSHOTO: Dk Harrison Mwakyembe.
Kuanzia sasa viongozi wote serikalini watakaopita kwenye viwanja vya ndege nchini, watakuwa wakikaguliwa kama abiria wengine, isipokuwa Rais, Makamu wake, Waziri Mkuu, Jaji Mkuu na Spika wa Bunge.

MSICHANA ALIYEGEUZWA MTUMWA WA NGONO AANIKA 'UCHAFU' WA KANALI GADDAFI...

KUSHOTO: Kanali Muammar Gaddafi. KULIA: Tingatinga likibomoa makazi yake ya mjini Tripoli.
Kanali Muammar Gaddafi aliamuru kutekwa kwa wasichana wa shule ambao baadaye walishikiliwa kama watumwa wa ngono kwenye eneo lake, kwa mujibu wa kitabu kuhusiana na dikteta huyo.

JICHO LA TATU...


MWANDISHI WA KIKE ALIYEBAKWA NA KUNDI LA WANAUME 'ATOA KALI' HOSPITALINI...

Maandamano kulaani vitendo vya ubakaji.
Mwandishi-mpigapicha ambaye alibakwa na kundi la wanaume watano mjini Mumbai amesema anataka kurejea kazini mapema iwezekanavyo.

BINTI ALIYEKAMATWA NA DAWA ZA KULEVYA PERU AONJA MACHUNGU YA JELA...

Mabinti hao, Melissa Reid na Michaella.
Melissa Reid ameandika barua kutoka gerezani kwenda kwa wazazi wake katika Siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake akiwaeleza 'niombeeni'.

Sunday, August 25, 2013

JWTZ LAFANYA MSAKO MKALI WA OFISA WAKE ALIYETOROKA MIEZI MINANE ILIYOPITA...

Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) linamtafuta popote alipo ndani na nje ya nchi ofisa wake, Luteni Kanali Celestine Seromba aliyetoroka jeshi zaidi ya miezi minane sasa.

JICHO LA TATU...


CHEKA TARATIBU...

Jamaa alikuwa akila mihogo na Mzungu kwenye banda moja maeneo ya Manzese. Wakati wakiendelea kula, ghafla muhogo ukamkaba jamaa kooni na maji anayo Mzungu.

WENYE MABASI 'WAMPIGA STOP' MNYIKA SAKATA LA WAPIGADEBE...

John Mnyika.
Chama cha Wamiliki wa Mabasi nchini (TABOA) kimemtaka Mbunge wa Ubungo, John Mnyika kutoingilia suala la uwepo wa wapigadebe katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo, kwa lengo la kutoathiri shughuli za utendaji kituoni hapo.

Saturday, August 24, 2013

MWANDISHI MPIGAPICHA WA KIKE ABAKWA NA KUNDI LA WANAUME AKIWA KAZINI...

Wapelelezi na maofisa wa polisi wakiwa eneo la tukio nyuma ya kiwanda hicho.
Mwandishi mpigapicha wa kike amebakwa wakati mwenzake wa kiume akifungwa na kupigwa kwenye kitovu cha biashara nchini India cha Mumbai, polisi walisema.

UFISADI!! BILIONI 9/- ZATEKETEA BANDARI KWA VIKAO VIWILI TU VYA WAFANYAKAZI...

Bandarini Dar es Salaam.
Kamati ya Bunge Hesabu za Serikali (PAC) imemwagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu  wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, kukagua maeneo matatu ya matumizi katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ili kubaini mianya ya ubadhirifu, ikiwa ni pamoja na matumizi ya Sh bilioni 9 kwa ajili ya vikao viwili tu kwa mwaka.

AFUNGIWA PANGONI KWA MIAKA 30 NA WAZAZI WAKE KWA KUONESHA DALILI ZA UKICHAA...

KUSHOTO: Dong Watou akionesha kovu refu pajani mwake. KULIA: Dong Hai akiwa amejikunyata (kulia) pangoni mwake.
Mwanaume ambaye alionesha dalili za matatizo ya kiakili wakati akiwa kijana mdogo alifungiwa pangoni na wazazi wake kwa miaka 30.

CHEKA TARATIBU...

Baba mmoja alikuwa akila chakula na binti yake mezani. Mara simu ikaita na baba huyo kwenda nje kuongea.

ALIYETHIBITISHWA KUFA NA KUZIKWA AIBUKA AKIWA HAI SIKU 13 BAADAYE...

KUSHOTO: Sharolyn Jackson. KULIA: Mahali ambako mwili uliodhaniwa ni wake ulipozikwa.
Mwanamke mmoja wa Philadelphia amejitokeza akiwa hai siku 13 baada ya familia yake kumzika kwenye mazishi yaliyovuta hisia kali.

MAREHEMU DAUDI MWANGOSI SASA AGEUZWA MTAJI WA KISIASA...

KUSHOTO: Marehemu Daudi Mwangosi. KULIA: Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa akiweka shada la maua kwenye kaburi la Mwangosi.
Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari nchini (UTPC), umekionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) dhidi ya kutumia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Wanahabari mkoani Iringa (IPC), Daudi Mwangosi kama mtaji wa kisiasa.

JICHO LA TATU...


MTOTO ASIMULIA ALIVYOISHIWA PUMZI SHAMBULIO LA GESI YA SUMU ILIYOUA WATU 1,700...

Baadhi ya watoto walionusurika wakipatiwa hewa ya oksijeni hospitalini.
Mvulana wa miaka 13 ameelezea jinsi 'pumzi zake zilivyokatika' wakati harufu yenye sumu ilivyokuwa ikitapakaa kwenye nyumba yao mjini Damascus wakati wa shambulio la gesi linalodaiwa kufanywa na vikosi vya serikali ya Syria.

Friday, August 23, 2013

MOTO MITAMBO YA UMEME SONGAS KUIWEKA DAR GIZANI WIKI NZIMA...


Mmoja wa askari wa zimamoto akizima moja ya mitambo hiyo jana asubuhi.
Moto mkubwa uliozuka katika mitambo ya kuzalisha umeme ya Songas Ubungo, Dar es Salaam,  umeathiri mitambo na vifaa vya umeme na kusababisha baadhi ya maeneo ya Jiji hilo, kukosa umeme, hali inayotarajiwa kuchukua zaidi ya wiki.

JICHO LA TATU...


NDEGE YATUA KWA DHARURA NDANI YA ZIWA MANYARA...

Ndege hiyo ililazimika kutua Ziwa Manyara (pichani).
Ndege ndogo aina ya Vich Grave, imelazimika kutua majini katika Ziwa Manyara kwa dharura, baada ya kupata hitilafu na kushindwa kutua katika viwanja vya ndege.

Thursday, August 22, 2013

RAIS KIKWETE AWAPANGUA MAKATIBU WAKUU WA WIZARA...

Ombeni Sefue.

Rais Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya makatibu wakuu wa wizara na naibu wao, kwa kupandisha cheo naibu katibu wakuu wengi, kuwa makatibu wakuu, kuteua wapya, kuwabadilisha wizara na wengine kusubiri kupangiwa kazi maalumu.

WAHUDUMU HOSPITALINI WADAIWA KUFANYA MAPENZI NA WAGONJWA NZEGA...

Watumishi wawili katika zahanati ya Mwanhala wilayani Nzega, wamekumbwa na kashfa ya kufanya mapenzi na wagonjwa hospitalini.

MKE WA LIYUMBA AMPANDISHA MUMEWE MAHAKAMANI...

Amatus Liyumba.

Mke wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu (BoT), Amatus Liyumba, Aurelia Ngowi amefungua kesi ya madai akipinga mumewe kuuza mali za familia na kumfukuza kwenye nyumba wanayoishi.

JICHO LA TATU...


ASKOFU WA KKKT APINGA WACHAGGA KUZIKANA MAJUMBANI...

Dk Martin Shao.

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Dk Martin Shao, amekosoa utamaduni wa wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro, ambao wengi ni Wachaga, wa kuzikana nyumbani (vihamba) na kusema ni utaratibu wa hovyo.

VIWANJA 7,800 VINAMILIKIWA NA WAMILIKI HEWA...

Kabwe Zitto.

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imebaini kuwapo wamiliki hewa wa viwanja 7,800 nchini, ambavyo vimetolewa na kupewa hati. 

Wednesday, August 21, 2013

MBUNGE WA CHADEMA ATIWA MBARONI KWA TUHUMA ZA UCHOCHEZI...

Ezekiah Wenje.
Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje  (Chadema) anashikiliwa na Polisi mkoani Mwanza kwa tuhuma za kuchochea maandamano yasiyo na kibali.

WATOTO 11 WAKAMATWA KWA BIASHARA YA NGONO SINGIDA...

Watoto 11 kutoka familia  tofauti wamekamatwa  mjini Singida,  wakidaiwa kufanya vitendo vya ngono kwenye nyumba moja usiku wa kuamkia juzi.

ALIYEBAMBWA NA DAWA ZA KULEVYA 'AIRPORT' DAR APANDISHWA KIZIMBANI...

Edwin Monyo.
Mtuhumiwa  Edwin Monyo (39) anayedaiwa kusafirisha dawa za kulevya zenye thamani ya Sh milioni 68, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashitaka hayo.

JICHO LA TATU...


MSAFARA WA MBIO ZA MWENGE WAPATA AJALI DODOMA...

Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Kiongozi wa Mbio hizo Kitaifa, Juma Ali Simai (kushoto) hivi karibuni. Simai na wenzake 9 wamejeruhiwa kwenye ajali hiyo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa, Juma Ali Simai (32) amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma baada ya kujeruhiwa kwenye ajali, iliyotokea kwenye msafara wa mbio za mwenge mjini hapa.