Showing posts with label Magazeti. Show all posts
Showing posts with label Magazeti. Show all posts
Thursday, October 16, 2014
YASEMAVYO MAGAZETI YA LEO ALHAMISI - OKTOBA 16
Labels:
Magazeti,
MagazetiLeo,
Magazetini,
Vichwa
This is a blog that brings you hot news that aims to educate the community about various things including sports, culture, art, entertainment and social. This blog does not involve political issues at all. We ask for your cooperation and to contribute opinions on the various information we bring to you.
WAWEKEZAJI WA GESI NA MAFUTA WAMIMINIKA ZANZIBAR
Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar imesema taasisi mbalimbali za kimataifa
zinazojishughulisha na masuala ya mafuta na gesi zimeanza kujitokeza kuomba
fursa ya kuwekeza katika sekta hiyo.
Maombi hayo
yamekuja kutokana na suala la mafuta na gesi kuondolewa katika orodha ya mambo
ya Muungano katika mchakato uliomalizika hivi karibuni wa Katiba
Inayopendekezwa na Bunge Maalumu la Katiba.
Hayo
yalisemwa na Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Iddi wakati alipozungumza
na wananchi wa jimbo la Kitope huko Kichungwani mkoa wa Kaskazini Unguja, baada
ya kushiriki kazi za usambazaji majisafi na salama.
Balozi Iddi
ambaye ni mbunge wa jimbo hilo alisema miongoni mwa mambo ambayo yalikuwa
yakipigiwa kelele na wananchi wengi wa Zanzibar kuondolewa katika orodha ya
Muungano ni suala la mafuta na gesi.
“Wananchi
mambo ambayo tumeyapigania kwa nguvu zote kuhakikisha kwamba yanaondolewa
katika orodha ya mambo ya Muungano ni suala la mafuta na gesi,” alisema.
Alisema
hatua hiyo imeanza kuleta manufaa makubwa kutokana na baadhi ya wawekezaji,
taasisi na mashirika ya kimataifa yanayojishughulisha na kazi za utafutaji wa
nishati hiyo kuwasilisha maombi yao.
Aidha,
balozi aliwataka wananchi kutokubali kuyumbishwa na kudanganywa na wanasiasa
ambao hivi sasa wamekuwa wakifanya kazi kubwa kuwababaisha wananchi na kupita
kila sehemu wakidai kwamba katiba inayopendekezwa haina maslahi kwa wananchi wa
Zanzibar.
This is a blog that brings you hot news that aims to educate the community about various things including sports, culture, art, entertainment and social. This blog does not involve political issues at all. We ask for your cooperation and to contribute opinions on the various information we bring to you.
KACHERO WA KENYA ATOA USHAHIDI MAHAKAMANI DAR
Mkuu wa Uchunguzi wa Maandishi
wa Jeshi la Polisi Kenya, John Kimani ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
jijini Dar es Salaam kuwa saini zinazodaiwa kusainiwa na Ramadhani Balenga
katika hati ya uhamishaji umiliki wa kiwanja pamoja na mkataba wa mauziano ni
za kughushi.
Kimani alidai hayo katika mahakama
hiyo wakati akitoa ushahidi katika kesi ya kughushi inayomkabili Mkurugenzi wa
Hoteli ya Rick Hill, Hans Macha.
Katika kesi hiyo,
mfanyabiashara huyo anakabiliwa na mashitaka ya kughushi hati ya kiwanja chenye
namba 183, Block A kilichopo Kigogo.
Akitoa ushahidi mbele ya Hakimu
Mkazi, Devotha Kisoka, Kimani alidai alifanya uchunguzi baada ya Polisi nchini
kumpelekea nyaraka, ikiwemo mkataba wa mauziano na nyaraka za uhamishaji
umiliki wa kiwanja kwa ajili ya kuzifanyia uchunguzi.
Aliieleza mahakama kuwa baada
ya uchunguzi wao uliotumia vifaa vya utaalamu, walibaini kuwa saini zilizopo
kwenye nyaraka hizo siyo za Balenga ni za kughushi.
Alidai wakati wanafanya
uchunguzi walizingatia mambo mengi ikiwamo kuangalia mgandamizo wa kalamu,
saini zote zilizokuwa na utata kwa kutumia kifaa maalumu.
Katika hatua nyingine,
mpelelezi wa kesi hiyo, Inspekta Lugano Mwampeta alisema aliwahoji watu
mbalimbali kuhusu jalada hilo, akiwemo Msajili wa Hati katika Ofisi ya Wizara
ya Ardhi, na kubaini hati hiyo ina utata katika saini.
Aidha, alisema alifika katika
eneo la kiwanja hicho ambacho kimejengwa ghorofa, na kugundua jengo hilo
haliwezi kuuzwa kwa Sh milioni 20.
Hakimu Devotha, aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 6,
mwaka huu kwa ajili ya kuendelea kusikiliza ushindi wa upande wa Jamhuri.
This is a blog that brings you hot news that aims to educate the community about various things including sports, culture, art, entertainment and social. This blog does not involve political issues at all. We ask for your cooperation and to contribute opinions on the various information we bring to you.
MAONESHO YA BIASHARA YA TIBA ASILI YA MWAFRIKA YAJA
Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji
wa Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Tiba Asili ya Mwafrika yatakayofanyika
kuanzia Novemba 16, mwaka huu kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
Maonesho hayo yatakayofanyika nchini
kwa mara ya kwanza yameandaliwa na Jukwaa la Tiba Asili Tanzania kwa
kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Mamlaka ya Maendeleo ya
Biashara Tanzania (Tantrade).
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati
ya Maandalizi ya Maonesho hayo, Boniventure Mwalongo, wadau mbalimbali wa tiba
asili na tiba mbadala wanatarajia kushiriki katika Maonesho hayo.
Mwalongo alisema washiriki hao ni
pamoja na watabibu wa tiba asili, watengenezaji wa dawa asili, wakunga wa tiba asili,
kampuni za dawa asili na vipodozi vya dawa asili, wasambazaji wa tiba
asili na tiba mbadala, watengenezaji wa vyakula asili, kliniki za tiba asili na
tiba mbadala.
Aidha, Mwalongo alisema wanaendelea
na taratibu za kufanya maongezi na wadhamini mbalimbali ambapo watatoa taarifa
rasmi baada ya kufikia tamati ya maongezi, ikiwa ni pamoja na kutoa ratiba
nzima ya maonesho hayo. Wadau wasiopungua 280
wameonesha nia ya kushiriki.
This is a blog that brings you hot news that aims to educate the community about various things including sports, culture, art, entertainment and social. This blog does not involve political issues at all. We ask for your cooperation and to contribute opinions on the various information we bring to you.
Monday, October 13, 2014
YASEMAVYO MAGAZETI YA LEO JUMATATU - OKTOBA 13
Labels:
Magazeti,
MagazetiLeo,
Magazetini,
Vichwa
This is a blog that brings you hot news that aims to educate the community about various things including sports, culture, art, entertainment and social. This blog does not involve political issues at all. We ask for your cooperation and to contribute opinions on the various information we bring to you.
Sunday, October 12, 2014
YASEMAVYO MAGAZETI YA LEO JUMAPILI - OKTOBA 12
Labels:
Magazeti,
MagazetiLeo,
Magazetini,
Vichwa
This is a blog that brings you hot news that aims to educate the community about various things including sports, culture, art, entertainment and social. This blog does not involve political issues at all. We ask for your cooperation and to contribute opinions on the various information we bring to you.
WANAWAKE 200 WAJITOKEZA AGA KHAN KUCHUNGUZWA SARATANI YA MATITI
Wanawake zaidi ya 200 jana walijitokeza katika kambi ya bure ya uchunguzi wa saratani ya matiti katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es salaam, kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi pamoja na kupata ushauri kuhusu saratani ya matiti.
Akizungumza katika kambi
hiyo jana, Daktari Bingwa wa magonjwa ya saratani, Dk Amyn Alidina alisema
hospitali ya Aga Khan inaadhimisha mwezi wa ufahamu wa saratani ya matiti
duniani kwa kutoa huduma ya uchunguzi kwa wanawake bila malipo.
Dk Alidina alisema kambi hiyo ni sehemu ya
kampeni ya hospitali hiyo yenye kaulimbiu “Usisubiri hadi Oktoba” iliyolenga
kuhamasisha umma kuchukua hatua ya kutunza afya zao sasa badala ya kusubiri
muda maalumu wa mwaka.
Dk Alidina alisema
saratani ya matiti inachangiwa na sababu mbalimbali ikiwemo historia ya
saratani katika familia, mfumo wa kazi unaoweza kusababisha kansa, mfumo
wa maisha kama vile uvutaji wa sigara, mfumo wa kula, historia ya maambukizi ya
virusi, na saratani iliyopita.
Kwa upande wake
Mkurugenzi wa Hospitali ya Aga Khan, Dk Mustaafa Bapumia alisema kuwa hospitali
hiyo imeona umuhimu wa kuweka kambi hiyo ili kuwasaidia wanawake baada ya kuona
kwamba tatizo hilo linawakumba wanawake
wengi na wanashindwa kujitambua mapema kutokana na kukosa huduma ya
uchunguzi.
This is a blog that brings you hot news that aims to educate the community about various things including sports, culture, art, entertainment and social. This blog does not involve political issues at all. We ask for your cooperation and to contribute opinions on the various information we bring to you.
Subscribe to:
Posts (Atom)







