Showing posts with label Hadithi. Show all posts
Showing posts with label Hadithi. Show all posts

Saturday, April 5, 2014

JICHO LA TATU...


SITTA AVUNJA KAMATI YA UONGOZI BUNGENI...

Samuel Sitta akiongoza Bunge la Katiba.
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta ametengua uteuzi wake wa awali wa nafasi tano za Kamati ya Uongozi ili kuifanya kamati hiyo kuwa na uwakilishi mpana.

Friday, April 4, 2014

HAPANA KUKOSA ONESHO HILI...


MKUU WA MKOA AMTOLEA NJE MNYIKA KUHUSU BODABODA...

Said Meck Sadik.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadik amesema hawezi kusitisha agizo lake la pikipiki na bajaj kuingia  katikati ya jiji, kwani hana mamlaka hayo, kwani anasimamia sheria.

NYONGEZA YA MSHAHARA WA WABUNGE YAZUSHA BALAA...

Wabunge wa Bunge la Uganda juzi wamezua tafrani baada ya kuibua hoja ya kutaka waongezewe mishahara, ambapo tayari mshahara yao ni mara 60 ya mshahara wa mfanyakazi wa umma.

KURA THELUTHI MBILI ZAKWAMISHA UAMUZI KAMATI ZA BUNGE...

Wajumbe wa Bunge la Katiba ambao baadhi yao wanaunda kamati mbalimbali.
Hatua ya kufanya uamuzi wa kupitisha vifungu vya rasimu ya Katiba mpya katika ngazi ya kamati za Bunge, ilifikiwa jana huku changamoto ya kutopatikana kwa theluthi mbili ya kura kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, ikijitokeza katika kamati nyingi.

JICHO LA TATU...


Thursday, April 3, 2014

IKULU YAANIKA POSHO ALIZOLIPWA JAJI WARIOBA NA WENZAKE...

Jaji Joseph Warioba (wa pili kutoka kulia).
Tume ya Mabadiliko ya Katiba haikufukuzwa kazi, isipokuwa siku ya ukomo iliwekwa kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.

BODABODA, BAJAJI MARUFUKU KUBEBA MTOTO WA MIAKA TISA...

Mtindo huu sasa ni marufuku kabisa.
Kanuni mpya za uendeshaji usafiri wa pikipiki na bajaj maarufu bodaboda, zimeainishwa zikisisitiza waendeshaji wa vyombo hivyo, kutekeleza masharti, ikiwemo linalokataza kupakia mtoto mwenye umri wa miaka tisa na  chini yake.

KESI DHIDI YA SHEKHE PONDA YAKWAMA...

Shekhe Ponda Issa Ponda akisindikizwa na askari mahakamani.
Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mkoa wa Morogoro jana imeshindwa kuanza kusikiliza kesi  ya Katibu wa Jumuiya ya Waislamu  Tanzania, Shehe Ponda Issa Ponda.

KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUTAKA KUMUUA TRAFIKI...

Mkazi wa Kijitonyama, Cresence Nguzo (25) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashitaka ya kujaribu kumuua askari wa kikosi cha usalama barabarani.

Wednesday, April 2, 2014

NHC YAWEKA SOKONI NYUMBA ZAKE 118 ZA MAKAZI...

David Shambwe.
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa mara nyingine jana limezindua mradi mpya wa mauzo ya nyumba za makazi ya familia 118 katika Mtaa wa Wakulima, Hananasif, wilayani Kinondoni.

MKUU WA MKOA CHUPUCHUPU MTEGO WA SIKU YA WAJINGA...

Dk Rajab Rutengwe.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi , Dk Rajab Rutengwe  ametoa ushuhuda wake  jinsi  alivyoponea chupuchupu,  kuhadaiwa  na mkazi mmoja  mjini Mpanda jana asubuhi,  ambayo ilikuwa Siku ya Wajinga Duniani.

WATU WANNE WAUAWA, 9 WALAZWA KWA MAPIGANO IGUNGA...

Mmoja wa majeruhi wa mapigano hayo akiwa amelazwa hospitalini.
Watu wanne wamekufa na  wengine tisa  wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya hiyo mkoani Tabora, kutokana na mapigano kati ya wakulima na wafugaji, yaliyotokea  katika Kijiji cha Isakamaliwa wilayani Igunga.

Tuesday, April 1, 2014

YASEMAVYO MAGAZETI YA LEO JUMANNE















WAJUMBE WAPIGWA BUTWAA KUVUNJWA BUNGE MAALUMU LA KATIBA...

Lango Kuu la kuingilia katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Ukimya mkubwa umetanda kwenye viwanja vya Bunge kwa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kushindwa kuamini wanachokisoma kwenye tangazo lililobandikwa katika lango kuu la kuingilia ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.

BABA AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 65 JELA KWA KUMPA MIMBA BINTI YAKE...

Mkazi wa Mtaa wa Uhamila katika mji mdogo wa  Rujewa, mkoani Mbeya, amehukumiwa miaka 65 jela kutokana na makosa matatu  tofauti, yaliyotokana na kumpa ujauzito mwanawe wa kumzaa.

MTOTO ASABABISHA FUMANIZI HOSPITALI YA MWANANYAMALA...

Wagonjwa wakisubiria huduma Hospitali ya Mwananyamala.
Tafrani ilizuka usiku wa kuamkia jana katika Hospitali ya Mwananyamala, Kinondoni jijini Dar es Salaam, ikihusisha wanandoa baada ya mke aliyekuwa amempeleka mtoto kutibiwa, kumbamba mumewe akimleta anayedaiwa kuwa kimada pia kupata matibabu hospitalini hapo.