Wednesday, July 31, 2013

MWALIMU WA HISABATI ABAMBWA CHINI YA KITANDA CHA MWANAFUNZI WAKE WA KIKE...

Mwalimu huyo akiwa amefungwa pingu chini ya ulinzi wa polisi.
Mwalimu wa somo la Hisabati amebambwa akiwa amejificha chini ya kitanda cha mmoja wa wanafunzi wake mwenye umri wa miaka 16.

DODOMA YAONGOZA KWA KUZALISHA OMBAOMBA WENGI DAR...

Baadhi ya ombaomba wakiwa wamepiga kambi kando ya moja ya mitaa ya Dar es Salaam na watoto wao.
Mkoa wa Dodoma unadaiwa kuongoza kwa kutoa idadi kubwa ya watoto wanaoomba  mitaani  katika Jiji la Dar es Salaam wakiwa na wazazi wao.

SAKATA LA KODI ZA SIMU KURUDISHWA BUNGENI AGOSTI...

Waziri wa Fedha, William Mgimwa alipokuwa akiwasilisha Bajeti ya Serikali 2013/2014 bungeni Dodoma.
Sakata la kodi ya simu ya Sh 1,000 kwa kila laini ya simu kwa mwezi, inayolipwa na watumiaji wa simu, litamalizwa bungeni kisheria.

JICHO LA TATU...


MAWAKILI WA SERIKALI KUPIGIWA SALUTI MAHAKAMANI...

Frederick Werema.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema, ameagiza utaratibu wa zamani wa mawakili wa Serikali kupigiwa saluti, urejeshwe ili Dola iheshimiwe wakati wa kuendesha kesi.

VIONGOZI WAFUNGIWA GHALA LA KOROSHO NA KUMWAGIWA UPUPU MTWARA...

Mmea wa upupu shambani.
Viongozi wa Chama cha Msingi cha Ushirika wa Mazao na Masoko Lenganelo na Diwani wa Mchemo, Mshamu Chituta, wamekamatwa na wanachama, wakafungiwa katika ghala la korosho na kumwagiwa upupu.

Tuesday, July 30, 2013

MWANAMKE AOZWA KWA NGUVU NA KUBAKWA NA KUNDI LA WANAUME SIKU YA HARUSI...

Waandamanaji wakiwa wameshikilia mabango kulaani vitendo vya ubakaji.
Mwanamke wa India mwenye miaka 24 amelazimishwa kuolewa na kubakwa na kundi la wanaume kama adhabu ya 'heshima' baada ya kaka yake kutoroka na rafiki yake wa kike, imebainika jana.

WALIOMMWAGIA TINDIKALI MAMA NA WANAWE HUKU WAKICHEKA WAFUNGWA MIAKA 44 JELA...

JUU: Yannick Ntesa. KATIKATI: Abdul Motin. CHINI: Ahad Miah. KULIA: Shule ya Msingi ya Upton Cross.
Kundi moja ambalo lilikuwa likicheka huku wakimlowesha mwanamke mmoja kwa tindikali wakati mama huyo akiwasindikiza nyumbani watoto wake mapacha wenye miaka sita kutoka shuleni, wamehukumiwa kifungo cha jumla ya miaka 44 jela.

MKENYA AHUKUMIWA KIFO KWA KUSAIDIA MAHARAMIA WA SOMALIA KUTEKA, KUUA WATALII...

KUSHOTO: Bi Judoth Tebbutt akiwa amedhoofu baada ya kuachiliwa huru. KULIA: Ali Babitu Kololo akivishwa pingu.
Mfanyakazi wa hoteli moja jana alihukumiwa kifo nchini Kenya baada ya kutiwa hatiani kwa kusaidia kutekwa mtalii wa Uingereza, Bi Judoth Tebbutt wakati wa shambulio ambalo mume wa mtalii huyo alipigwa risasi na kufa.

JICHO LA TATU...


UKATILI WA 'MEMORY CARD' WAFYEKA MAISHA YA WANAWAKE 14 MARA...

Moja ya mitaa ya mkoani Mara.
Ukatili mpya wa kijinsia unaojulikana kama ‘Memory Card’ umezuka mkoani Mara na kusababisha mauaji ya wanawake zaidi ya 14 katika kipindi cha kuanzia Desemba mwaka jana hadi Julai, mwaka huu.

BENITEZ AFARIKI DUNIA KWA MARADHI YA MOYO...

KUSHOTO: Christian Benitez akifanya vitu vyake uwanjani. KULIA: Chritian Benitez.
Mshambuliaji wa zamani wa Birmingham City, Christian Benitez amefariki ghafla kwa kile kinachodhaniwa matatizo ya moyo akiwa na umri wa miaka 27.

AJIFUNGUA MTOTO SAA 15 BAADA YA KUJIGUNDUA KUWA NI MJAMZITO...

Amanda Ross akiwa amembeba mwanae. Kushoto ni mumewe, Paul Dean.
Mwanamke mmoja amejifungua mtoto wake wa kwanza masaa 15 tu baada ya kujigundua alikuwa mjamzito.

Monday, July 29, 2013

HATIMA YA KESI YA RUSHWA DHIDI YA HAKIMU MKAZI ILALA KUJULIKANA LEO...

Pamela Kalala.
Hatima ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Pamela Kalala  anayekabiliwa na kesi ya kuomba rushwa ya Sh milioni tatu, itajulikana leo Mahakama itakapotoa uamuzi kama ana kesi ya kujibu au la.

JICHO LA TATU...


MITUNGI YA GESI MAJUMBANI YADAIWA KUFUNGULIWA NA KUFUNGWA KIENYEJI...

Mitungi ya gesi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.
Mitungi ya gesi ya kupikia kutoka kwenye kampuni zinazotambulika inadaiwa kuhujumiwa na baadhi ya watu kwa kuifungua na kupunguza malighafi hiyo kisha kuifunga kienyeji.

MAGUFULI AWASHITAKI KWA RAIS KIKWETE WANAOKATAA FIDIA...

Dk John Magufuli.
Serikali imeonya kuwa haitaruhusu watu wachache wakwamishe juhudi za Serikali za kuunganisha nchi na mtandao wa barabara za lami.

Sunday, July 28, 2013

HAUSIBOI ALIYELAWITI BINTI WA MIAKA MINNE AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA...

Mahakama  ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imemhukumu kijana, Baraka  Juma (22) mkazi wa kijiji cha Nkungwi  wilayani humo, kifungo cha maisha jela  baada ya kupatikana  na hatia  ya  kosa la kumlawiti mtoto wa kike mwenye umri  wa  miaka minne  baada  ya kumhadaa na  kumlewesha bia.

MBUNGE NASSARI ASOTA POLISI KWA MADAI YA KUMPIGA KADA WA CCM...

Joshua Nassari.
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari jana alishikiliwa na jeshi la polisi mkoani Arusha kwa saa tatu na nusu kwa tuhuma za kumshambulia kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hussein Warsama siku ya uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Makuyuni, wilayani Monduli.

JICHO LA TATU...

MATOKEO... Uganda 3 - Taifa Stars (Tanzania) 1.  Uganda imesonga mbele kwa jumla ya mabao 4-1.

Saturday, July 27, 2013

IMEBAINIKA: USAIN BOLT HUZALISHA NISHATI MARA 50 ZAIDI YA RISASI INAPOFYATUKA...

Mwanariadha Usain Bolt akiweka pozi lake maarufu baada ya kushinda mbio.
Bingwa wa Olimpiki Usain Bolt anazalisha nishati mara 50 zaidi ya ile ya risasi iliyofyatuka kutoka kwenye bunduki wakati wa moja ya mbio zake za mita 100 alizovunja rekodi, wanasayansi wamebainisha.

SAJENTI WA KIKE ATIMULIWA KAZI KWA KUPIGA PICHA CHA UCHI KAZINI...

Penny Dane katika pozi tofauti.
Sajenti wa polisi ameacha kazi baada ya uchunguzi kukuta picha zake akiwa uchi kwenye kompyuta yake ya kazi na mitandao ya ngono ambayo anadaiwa alikuwa akitazama wakati wa kazi.

WAHITIMU VYUO VIKUU SASA WATENGEWA MABILIONI YA SHILINGI WAJIAJIRI...

Baadhi ya wahitimu wa moja ya vyuo vikuu hapa nchini.
Wasomi watakaohitimu vyuo vya elimu ya juu nchini kuanzia mwaka huu watakopeshwa mabilioni ya fedha ili waanzishe miradi itakayowawezesha kujiajiri.

BABA AKUTANA NA BINTIYE ALIYEDHANI AMEKUFA MIAKA 45 ILIYOPITA...

Charles Lutzow (kulia) akiwa na binti yake, Keri Abercrombie.
Baba mmoja wa Alabama ameungana na binti yake aliyepotea muda mrefu baada ya kuwa ameamini alikufa kwa takribani nusu karne.

MKULIMA ATUHUMIWA KUWAUA WATOTO WAKE WAWILI KASULU...

Kamanda Fraiser Kashai.
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma linamshikilia mkulima mkazi wa kijiji cha Mvugwe, Kasulu, Thobias Majuto kwa kuua watoto wawili kwa makusudi.

Friday, July 26, 2013

MWANAFUNZI WA KIKE AJIUA KWA SUMU BAADA YA KUBAKWA SUMBAWANGA...

Moja ya aina za sumu ya panya.
Mwanafunzi wa kidato cha nne, Flora Athanas (18) wa sekondari Mzindakaya wilayani hapa amejiua kwa sumu ya panya, baada ya kubakwa na mtu asiyefahamika.

MKE ALIYEPANGA KUMUUA MUMEWE ARUSHA APANDISHWA KIZIMBANI...

Sehemu ya jiji la Arusha.
Mke wa mfanyabashara maarufu wa madini mkoani Arusha, Janeth Jackson (32) anayedaiwa  kupanga njama za kumuua mumewe wa ndoa na mtoto wa mume huyo,  amepandishwa katika mahakama ya wilaya ya Arusha pamoja na mtuhumiwa mwingine.

JICHO LA TATU...


WAGANGA WA KIENYEJI SAUZI WAMTAMBIKIA MZEE MANDELA...

Hospitali alikolazwa Mzee Mandela mjini Pretoria.
Kundi la waganga wa kienyeji kutoka mkoa wa Gauteng, wameamua kutambika nje ya hospitali aliyolazwa Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela.

JWTZ IKO TAYARI KWA VITA, NCHI ITAKAYOTHUBUTU ITAKIONA CHAMOTO...

Rais Jakaya Kikwete akiweka silaha kama ishara ya kuwambuka mashujaa, jana.
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete amewatoa hofu Watanzania akiwataka walale usingizi kwa kuwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakati wowote lipo tayari kulinda nchi kwa gharama yoyote.

Thursday, July 25, 2013

MWANAMKE ALIYESITISHA NDOA ADAI KATEKISTA ALIMSUKUMA KWENYE NGAZI ZA KANISA...

Mwanamke huyo akiwa amevalia vazi lililozusha tafrani yote hiyo. Nyuma yake ni Kanisa la Mt. Peter, Dar es Salaam.
Wakati mwanamke wa kivazi kilichositisha ndoa kanisani kwa dakika kadhaa akidai hakuwa na tatizo kuvaa vile, Katekista wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Peter, Yohane Maboko, amesisitiza kuwa alikiuka maadili ya Kanisa.

MZAHA WA LEO...

****************************************************
Ukiona mpenzi wako hapokei simu, mtumie meseji yenye namba za vocha lakini ondoa tarakimu moja ya mwisho. Ndani ya dakika chache utaona anakupigia akilalamika: "Mpenzi mbona haikubali?"
****************************************************

JICHO LA TATU...


MAREKANI YAIONYA RWANDA KUACHA KUSAIDIA WAASI WA M23...

KUSHOTO: Waasi wa M23 wakiwa wametega silaha zao. KULIA: Msemaji wa Ikulu ya Marekani, Jen Psaki.
Marekani imeitaka Rwanda kuacha kusaidia waasi wa kundi la M23 ambalo linaendesha mapambano dhidi ya Serikali ya nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

AFA BAADA YA BUNDUKI YAKE KUJIFYATUA GHAFLA AKIWINDA SUNGURA...

Carl Rubisch (kushoto). Kulia ni shamba walikokuwa wakiwinda sungura.
Baba wa watoto wawili amefariki baada ya kujipiga risasi mwenyewe kwa bahati mbaya wakiwa katika safari usiku kuwinda sungura akiwa na rafiki yake.

Wednesday, July 24, 2013

CHEKA TARATIBU...

Mama wakati akiandaa chakula mezani kamwagiza mwanae ampigie simu kumwita baba yake aliyekwenda matembezini.

MKE ADAIWA KUPANGA NJAMA ZA KUMUUA MUMEWE ARUSHA...

Kamanda Liberatus Sabas.
Mke wa ndoa wa mfanyabiashara wa madini Arusha, Jackson Manjuru, amekamatwa na Polisi kwa tuhuma za kupanga njama za kuua mumewe.

ASKARI KUTOKA ZANZIBAR WALIOUAWA DARFUR WAZIKWA...

Askari wakiwa wamebeba moja ya majeneza yenye miili ya wanajeshi hao.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein jana   aliungana na viongozi mbalimbali wakiwemo wa vikosi vya ulinzi na usalama wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja na wafiwa na wananchi katika maziko ya wanajeshi wa Zanzibar waliouawa Darfur, Sudan.

ZANZIBAR WAPINGA MFUMO WA SERIKALI TATU...

Mandhari ya Zanzibar.
Baadhi ya wajumbe wa mabaraza ya Katiba, wamepinga muundo wa Muungano wa serikali tatu kwa hoja kadhaa, ukiwamo uwezekano wa muundo huo kuzorotesha Muungano na umoja wa kitaifa.

JICHO LA TATU...


MWANAMKE ALIYEVAA NGUO YA WAZI AKWAMISHA NDOA KANISANI DAR...

Katekista Yohane Maboko (kulia) akimsihi mwanamke huyo kutoka nje ya kanisa.
Kivazi cha ndugu wa maharusi, kimesababisha patashika katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Peter, baada ya Paroko Msaidizi wa Kanisa Hilo, Padri Paulo Haule, kusitisha ibada mpaka mhusika atoke akavae vizuri.

Tuesday, July 23, 2013

ASKARI SABA WA JWTZ WALIOUAWA DARFUR WALIPAMBANA KWA MASAA MAWILI...

Baadhi ya askari wa JWTZ wakipita mbele ya miili ya wenzao waliouawa mjini Darfur, kutoa heshima zao za mwisho kwenye viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi, Dar es Salaam jana.
Majeneza yenye miili ya askari hao yakiwa yamepangwa tayari kwa zoezi la kutoa heshima za mwisho.
Wanajeshi saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), waliouawa wakati wakilinda amani  Darfur nchini Sudan, walipigana kwa saa mbili wakati wakijitetea kabla ya kufikwa na mauti.

BABA AUA MTOTO WAKE WA MIAKA MIWILI KWA KUMBAMIZA UKUTANI. KISA? ALITAPIKA...

KUSHOTO: Mtoto Jayden Morales Villegas. JUU: Angel Villegas. CHINI: Vanessa Morales.
Mtoto wa miaka miwili amefariki baada ya baba yake kudaiwa kumtupa kitandani - na kusababisha mtoto huyo wa kiume kujibamiza kichwa chake ukutani - kwa sababu alitapika.

WASEMA MISHAHARA MIPYA YA WATUMISHI WA NDANI HAITEKELEZEKI...

Baadhi ya watumishi wa ndani wakiwa katika moja ya semina waliyoandaliwa.
Baada ya Serikali kuweka kisheria mshahara wa kima cha chini kwa watumishi wa ndani, Chama cha Wafanyakazi wa Hifadhi, Hoteli, Majumbani, Huduma za Jamii na Ushauri (CHODAWU), kimeeleza kuwa utekelezaji wa sheria hiyo ni mgumu.

JICHO LA TATU...


MTU MWENYE UMRI MKUBWA ZAIDI DUNIANI ALIYE HAI AIBUKA INDIA, ANA MIAKA 141...

Feroz-un-Din Mir (kushoto) na Jiroemon Kimura.
Mwanaume mmoja nchini India anadai ana umri wa miaka 141 - ambao utamfanya awe binadamu mzee zaidi duniani ambaye bado yuko hai.

MAHAKAMA YAMTAKA MWENZAKE NA LWAKATARE 'KUFUNGA MDOMO'...

Ludovick Joseph.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imemwonya mshitakiwa mwenza wa Mkurugenzi wa Ulinzi wa Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare, Ludovick Joseph, kutozungumza na vyombo vya habari wala mitandao ya kijamii.

Monday, July 22, 2013

WANAUME SITA WALIOMBAKA MTALII WA USWISI WAFUNGWA MAISHA JELA...

Mahakama ya India juzi imewahukumu kifungo cha maisha jela wanaume sita waliopatikana na hatia ya kumbaka mwanamke raia wa Uswisi, katika moja kati ya kesi kadhaa za hivi karibuni ambazo zimechochea maandamano ya kulaani ongezeko kubwa la matukio ya ubakaji nchini India.

ASKARI WA JWTZ WALIOUAWA DARFUR KUAGWA LEO MAKAO MAKUU YA JESHI DAR...

Miili ya askari hao ilipowasili jijini Dar es Salaam juzi.
Askari saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), waliouawa katika jimbo la Darfur nchini Sudan, wanatarajiwa kuagwa leo kwenye viwanja vya makao makuu ya jeshi hilo.