Thursday, January 7, 2016

SERIKALI YAITOLEA NJE UDA NAULI MPYA MABASI YAENDAYO HARAKA

Serikali imekataa viwango vya nauli mpya vilivyopendekezwa na Kampuni ya Uda Rapid Transit (UDA-RT), itakayotoa huduma ya usafiri wa mabasi yaendayo haraka Dar es Salaam.

MAFURIKO YAKOSESHA MAKAZI KAYA 2,857

Kaya 2,857 wilayani Kilosa zimekosa makazi kutokana na nyumba 379 kubomoka na nyingine 997 kuzingirwa na maji yaliyotokana na mafuriko yaliyokumba wilaya hiyo ya Mkoa wa Morogoro.

BUNGE LAWAHALALISHA MAWAZIRI WA MAGUFULI


Mawaziri walioteuliwa na kuapishwa na Rais John Magufuli kabla ya kula kiapo cha ubunge, wanaruhusiwa kushiriki shughuli za Bunge kama wabunge wateule.

ATUHUMIWA KUBAKA NA KUMPA UJAUZITO DADA YAKE

Polisi mkoani Kagera, wanamshikilia mkazi wa wilaya ya Misenyi mwenye umri wa miaka 19 kwa tuhuma za kumbaka dada yake  mwenye umri wa miaka 15 (majina yanahifadhiwa) na kumpa ujauzito.

Monday, January 4, 2016

MAFURIKO YAANGAMIZA WANANE WA FAMILIA MOJA, YUKO IGP MSAIDIZI

Watu wanane akiwemo Msaidizi  wa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali (IGP), Gerald Ryoba  pamoja na familia yake,  wamekufa maji baada ya gari walilokuwa wakisafiria kusombwa na maji katika mkondo mpana wa mto unaotenganisha Kibaigwa na Pandambili, mkoani Dodoma.

Waishauri serikali kufufua Nasaco

Jumuiya ya Mabaharia nchini (JMT), imeiomba serikali kufufua Shirika la Taifa la Wakala wa Meli Tanzania (Nasaco), ili kuwa na chombo cha kitaifa kitakachosimamia maslahi ya nchi kwenye sekta hiyo na kuondokana na ubadhirifu unaofanywa bandarini.

Wadau kujadili nauli mabasi yaendayo haraka

Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) wiki ijayo inakutana na wadau kujadili nauli zitakazotumika kwa mabasi yaendayo kasi.

Afya ya Kardinali Pengo yaimarika

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete anaendelea vizuri na anaweza kuruhusiwa wiki ijayo.

BINTI WA MIAKA 15 MBARONI KWA MAUAJI YA MAMA YAKE NA BABA WA KAMBO


Msichana mwenye umri wa miaka 15 amekamatwa kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi na rafiki wa kiume wa mama huyo kwa kile alichodai kubakwa na mwanaume huyo, polisi wamesema.

MAGUFULI: A ‘PROFET’ STRUGGLES TO FIND DISCIPLES IN A NEW TANZANIAN DISPENSATION


Tanzania’s new President John Pombe Magufuli has been a big hit among social media pundits in the East Africa owing to his tough stance on corruption and government official excesses.