Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam,
Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya
Kikwete anaendelea vizuri na anaweza kuruhusiwa wiki ijayo.
Pengo amelazwa katika taasisi hiyo iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam kuanzia usiku wa Desemba 31, mwaka jana na ametolewa katika chumba cha uangalizi maalumu na kuwekwa katika wadi ya kawaida.
Akizungumza
jana, Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Mohamed Janabi, alisema afya
ya Pengo inaendelea vizuri na kwamba endapo hali ikiendelea hivyo anaweza
kuruhusiwa kutoka hospitali wiki ijayo.
Kuhusu
ugonjwa unaomsumbua, Janabi alisema kwa mujibu wa taaluma yao hawana sababu ya
kuzungumzia ugonjwa wake labda mwenyewe akipona anaweza kuelezea ugonjwa
uliokuwa ukimsumbua.
Juzi,
Rais John Magufuli akiongozana na mkewe, Janeth Magufuli walimtembelea Pengo ili kumjulia
hali, kumpa pole na kumuombea afya njema ili aweze kuendelea na shughuli zake
za kutoa huduma za kiroho kwa wananchi.
No comments:
Post a Comment