Monday, June 30, 2014

10-MAN COSTA RICA BEAT GREECE ON PENALTIES

Goalkeeper Keylor Navas was Costa Rica's hero as his penalty shoot-out save put ten-man Costa Rica into the World Cup quarter-finals after a 1-1 draw in extra time against Greece.
Los Ticos will face Netherlands in the last eight following a hard-earned shoot-out win at the end of a tense, cagey match between two of the surprise qualifiers for the knockout phase.
Bryan Ruiz scored seven minutes into the second half when he spotted Greek goalkeeper Orestis Karnezis out of position and simply side-footed the ball into the bottom right corner from the edge of the box.
Oscar Duarte was then sent off 14 minutes later for a second yellow card - a decision he accepted without a murmur - but the Central American side appeared to have held on until Greek defender Sokratis chose the perfect moment to score his maiden international goal, an equaliser shinned into the goal from a rebound in injury time.
Only a fine save from Navas prevented Greece from pinching it at the death - and Navas was again the hero with a brilliant save from Theofanis Gekas in an otherwise-perfect shootout, with Michael Umana converting Costa Rica's fifth penalty to put his side into the last eight.
 
KEY MOMENTS
PRE-MATCH:
Campbell and Samaras lead the attacks: It's Arsenal's starlet, Joel Campbell versus Celtic's Georgios Samaras in the battle of two sides no-one predicted to face-of in the last 16. Costa Rica pick the same team that beat Italy 1-0 in the Group stage while Greece bow to social media pressure with Kostas Katsouranis left out.
7' - COSTA RICA CHANCE! Ruiz picks up a loose ball 40 yards out and plays in Bolanos who sears a shot past the near upright.
38' - STUNNING SAVE! A wonderful ball from the left is met by Salpingidis at the far post, but Navas somehow keeps it out.
52' - GOAL! COSTA RICA 1-0 GREECE. Ruiz opens the scoring with a shot from the edge of the area after Bolanos picked him out from the left. It lacked pace but completely fooled the keeper who thought it was going to fizz towards his right-hand post. It didn't and Cost Rica lead!
54' - PENALTY SHOUT - It should be a penalty as a cross from the right is touched by the hand of Torosidis. Greece with a great escape!
66' - RED CARD! Duarte sent off! It's a second yellow for a late tackle on Holebas. Costa Rica down to 10-men.
88' - GREECE CHANCE. CLOSE! Christodoulopoulos glides to the right byline and drills a low ball towards Motroglou who can't convert and Navas is able to gather.
90+1' - GOAL! COSTA RICA 1-1 GREECE. They've done it!!!!! Papastathopoulos pounces on the rebound after Gekas' shot on the turn was beaten out by the keeper. Extra time beckons.
90+3' - GREECE CHANCE! Mitroglou glances a header at goal and Navas tips it over the top!
107' - COSTA RICA CHANCE. Brenes gets in behind a complacent Greek defence but hammers his right-foot shot wide of the upright.
108' - GREECE CHANCE. Katsouranis slips a slide-rule pass into the left channel for Gekas but Navas comes off his line to thwart the forward.
113' - GREECE CHANCE. Five Greeks break on two defenders from the corner... it's played to Christodoulopoulos who drills a shot at the keeper. They should have walked that in!
120' - GREECE CHANCE. Mitroglou latches onto a flick on and sees his shot brilliantly saved by the keeper! Astonishing stuff.

TALKING POINT: Can Costa Rica keep surprising us? Ticos topped a group containing the more fancied England, Italy and Uruguay and no-one is expecting them to go much further. But they have a never-say-die spirit that continues to see them prevail and despite playing an hour with 10-men they held on for penalties. Even the blow of conceding a last-gasp equaliser in normal time couldn't knock them out of their stride. Holland will be huge favourites to make the last four, but in this tournament in the spiritual home of football, anything seems possible.

KEY STATS
Oscar Duarte is the first Costa Rica player to be sent-off at the World Cup.
Bryan Ruiz scored with Costa Rica’s only shot on target in the match.
Sokratis’ goal was the first Costa Rica had conceded from open play in the 2014 World Cup.
Sokratis scored the 145th goal of the 2014 World Cup. The 2010 World Cup featured 145 goals in total.
The Greeks have scored five goals in 10 World Cup games.
Greece had 70% of possession in the second half of the match.
Greece enjoyed more possession in the whole game (60%) than in any other World Cup match in their history.
This match featured the joint most cards in a game at this World Cup (7: 6Y 1R), the same as Brazil v Chile.
There were just two shots on target in extra-time (both from Greece).
Costa Rica have remained unbeaten in four World Cup games for the very first time (W2 D2).
Greece have drawn two of their last three World Cup matches (W1); having drawn none of the first seven (W1 L6).
Only Alexis Sanchez (24) has been fouled more than Georgios Samaras (21) and Joel Campbell (19) so far at the World Cup.
The last team from CONCACAF to go further than the last 16 at the World Cup were the USA in 2002.

MAN OF THE MATCH
Keylor Navas (Costa Rica):
It could only be one man. A stunning save in the first half was followed by a one man mission to keep his country in it during extra-time as he produced a series a fine stops. Made the key block to keep out Gekas spot kick in the shoot-out, allowing Umana to win it.

PLAYER RATINGS
Greece:
Karnezis 6, Maniatis 6, Manolas 6, Samaris 6, Karagounis 7, Salpingidis 6, Torosidis 7, Lazaros 6, Sokratis 7, Cholevas 6, Samaras 7. Subs: Mitroglou 7, Gekas 7, Katsouranis 6.
Costa Rica: Navas 9, Gonzalez 7, Duarte 4, Gamboa 7, Umaña 7, Diaz 7, Borges 7, Bolanos 7, Tejeda 6, Ruiz 7, Campbell 7. Subs: Cubero 7, Acosta 6, Brenes 7.
Mshambuliaji wa Uholanzi, Arjen Robben akiwa ameangushwa chini na hivyo kuipatia timu yake penalti dhidi ya Mexico katika mechi ya Kombe la Dunia hatua ya 16 Bora jana. Penalti hiyo ilipigwa kiufundi na Klaas-Jan Huntelaar na kuivusha Uholanzi hatua ya Robo Fainali ambapo itapambana na Costa Rica iliyoitoa Ugiriki kwa penalti 5-3.

DUTCH BREAK MEXICAN HEARTS WITH LATE DOUBLE

The Netherlands pulled off a staggering late comeback to beat Mexico 2-1 in Fortaleza and make the quarter-finals of the World Cup.
A stunning goal from Giovani Dos Santos and a string of magical saves from Guillermo Ochoa got Mexico to within two minutes of a spot in the last eight.
But Louis van Gaal's decision to replace Robin van Persie with Klaas-Jan Huntelaar paid off, as the sub was at the heart of the astonishing late comeback as the Netherlands pulled off an unforgettable victory.
Huntelaar nodded down from a corner for Wesley Sneijder with just two minutes left, and the Galatasaray playmaker drilled a stunning low shot into the bottom left corner.
Extra time seemed the Oranje's reward, but the game took another twist as Arjen Robben won a penalty almost three minutes into the six minutes of added time.
Robben was adjudged to have been felled in the area by Rafael Marquez; replays suggested it was a highly theatrical dive from the Dutchman, but he had been wrongly denied a clear penalty earlier so justice was probably done in the end.
And it was Huntelaar who stepped up and sent the ever-impressive Ochoa the wrong way from the penalty spot.
Mexico had controlled most of the match and should probably have pressed their superiority further, but it was a bitter blow for Miguel Herrera's spirited side - and in particular Ochoa, whose brilliance made him one of the heroes of the World Cup.

KEY MOMENTS

PRE-MATCH:
RVP returns, ton up Dirk. Robin van Persie returns from suspension to partner Arjen Robben in attack for Holland while Dirk Kuyt joins an elite group of Dutchman to make a century of appearances for his country, playing in a wing-back role as part of what looks like a 5-3-2 formation. Augsburg's Paul Verhaegh also features. For Mexico, Carlos Salcido comes into the midfield for the suspended Jose Juan Vazquez. Giovani Dos Santos and Oribe Peralta forge the attack in a 5-3-2 system.
17' - MEXICO CHANCE! A high ball into the area is chested down by Peralta who manages to work the ball across goal. It finally comes to Herrera who drags his shot from 10 yards agonisingly wide of the post.
20' - MEXICO CHANCE! Herrera bursts past Vlaar in the area and then sees his attempt to nod it into his own path stopped by a dangerously high boot from the Aston Villa man. Mexico want a penalty, but they aren't going to get it. Certainly a decent shout.
32' - COOLING BREAK! The players all race to the touchline to have some much-needed fluid given how hot it is - almost 30 degrees in the tropical northern city of Fortaleza.
42' - MEXICO CHANCE! Dos Santos is sent racing into the left side of the area but sees his low shot from a tight angle beaten away by Cillessen.
45+2' - HOLLAND PENALTY SHOUT! A mistake means the 'Oles' catch in the fans' throats and RVP looks to release Robben. The Bayern man gets in but Marquez appears to recover and sends him tumbling. Was that a penalty? Marquez doesn't win the ball and neither does Moreno who follows through.
48' - GOAL! HOLLAND 0-1 MEXICO. El Tri lead! Dos Santos latches on to a weak headed clearance, chests it into his stride and lashes a low shot from 25 yards into the corner. Cue huge celebrations with his teammates in front of the Mexico fans.
58' - GREAT SAVE OCHOA! Guillermo Ochoa is at it again with another sensational save onto the post from point-blank range to keep out the volley!
75' - MORE OCHOA BRILLIANCE! Another great save from Ochoa as he beats away the low shot from Robben after another surging run from the forward.
88' - GOAL! HOLLAND 1-1 MEXICO. Holland are level! Sneijder breaks Meixcan hearts when a 10th corner of the match is nodded down into his path and he does the rest with low shot into the bottom corner. Saviour!
90+4' - GOAL! HOLLAND 2-1 MEXICO. Holland are going through to the last eight! Huntelaar had to wait a long time but kept his nerve to hammer his penalty low into Ochoa's right-hand corner wrong way. The kick as the keeper dived the wrong way. The kick was given after Marquez appeared to foul Robben by the right byline.

KEY STATS

The Netherlands’ first shot on target in the game came in the 57th minute, Guillermo Ochoa dramatically saving a Stefan de Vrij effort from close range.
Wesley Sneijder has scored five goals in his last five knock-out stage games at World Cup finals.
The Netherlands have converted all nine World Cup penalties they have taken (exc. shoot-outs).
The Netherlands have now turned their last four World Cup games in which they fell behind in regular time (90 mins, not inc. ET) into a victories.
Seven different players have scored for the Netherlands at this World Cup, more than any other side in the tournament.
Four of last five World Cup knock-out stage goals conceded by the Netherlands have come from outside the box. (all except Iniesta’s goal in the final).
Mexico have lost four and drawn one of their last five encounters with the Netherlands, conceding at least two goals on each of these occasions.
Mexico have been knocked out of the World Cup finals at the second round stage in all six editions since 1994; no team has been knocked out at this stage as often as this.
Netherlands have won 10 of their last 11 World Cup matches, with the only blip in this run being their 2010 final defeat against Spain.
Mexico have scored a goal in each of their last 12 World Cup matches against European nations.
11 of the last 13 World Cup goals scored by Mexico have come after half time, while the Netherlands have scored 10 of their last 11 World Cup goals in the second half.
Ron Vlaar completed all 37 passes he attempted in this game, no Dutch player has made as many and completed them all in a World Cup game since 1966.
Four of the last five Dutch goals at this World Cup have been scored by substitutes.

TALKING POINT: Can the Dutch win it with such reliance on Robben and individual brilliance? Mexico will feel really hard done by as they restricted the Netherlands to scraps for long spells. A wonder goal from dos Santos and some goalkeeping heroics from Ochoa looked to have done the job, but a great goal from Sneijder and the run from Robben for the penalty turned the game on its head. The Dutch will need to play much better if they want to end their quest for a first title.

MAN OF THE MATCH

Guillermo Ochoa (Mexico): The stand-out goalkeeper of the tournament looked to have helped his team into the last eight with a series of sensational saves. He could do little with the two late Dutch goals but will leave Brazil with his reputation soaring through the roof.

PLAYER RATINGS

Netherlands:
Cillessen 6, De Vrij 6, Vlaar 5, Verhaegh 5, Blind 7, Kuyt 6, Wijnaldum 6, De Jong 5, Sneijder 7, Robben 8, van Persie 6. Subs: Martins Indi 6, Depay 7, Huntelaar 8.
Mexico: Ochoa 9, Rodriguez 6, Salcido 6, Marquez 6, Moreno 6, Aguilar 6, Herrera 7, Guardado 6, Layun 7, Peralta 6, Dos Santos 7. Subs: Reyes 6, Aquino 6, Hernandez 5.
Mshambuliaji wa Mexico, Giovanni Dos Santos akishangilia bao aliloifungia timu yake katika dakika ya 48 dhidi ya Uholanzi katika mechi ya Kombe la Dunia hatua ya 16 Bora jana mjini Fortaleza. Hata hivyo bao hilo halikutosha kuivusha timu yake na kujikuta ikichezea kichapo cha mabao 2-1.

Wachezaji wa Costa wakishangilia mara baada ya mwenzao kufunga penalti ya mwisho na hivyo kuindosha mashindanoni Ugiriki kwa jumla ya penalti 5-3 baada ya timu hizo kutoka sare ya bao 1-1 katika dakika 120 za mechi hiyo jana.

Mshambuliaji wa Uholanzi, Wesley Sneidjer akishangilia baada ya kuifungia timu yake bao la kusawazisha katika dakika ya 88 dhidi ya Mexico katika mechi ya Kombe la Dunia hatua ya 16 Bora jana. Uholanzi ilishinda mabao 2-1 na hivyo sasa katika hatua ya Robo Fainali watakutana na Costa Rica ambayo iliiondosha mashindanoni Ugiriki kwa mikwaju ya penalti 5-3.

JICHO LA TATU


LAPF YAMWAGA MIKOPO KWA WANAOSOMA VYUO VIKUU

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (LAPF) umeanzisha huduma mpya ambayo itasaidia wananchama wake wenye mipango ya kupata elimu ya juu kuweza kujipatia mikopo kwa ajili ya kufanikisha adhama hiyo.
Huduma hiyo itawawezesha kujiendeleza vyuo vikuu vya hapa nchini na nje ya nchi.
Akizungumza ofisini kwake Mkurugenzi Mtendaji Eliudi Sanga, alisema lengo la kuanzisha utaratibu huo ni kumnufaisha mwanachama kielimu.
Pamoja na kutoa maelezo hayo aliwataka wanachama na wananchi kwa ujumla kuchangamkia mikopo hiyo ya elimu ya juu.
Aidha alisema kwamba mfuko huo utatoa huduma kwa wanachama, watumishi wa umma,wafanyabiashara na wajasirimali mbalimbali ambao wanaweka akiba zao za uzeeni katika mfuko huo.
Kwa sasa mfuko huo unatoa mikopo ya nyumba ikiwa lengo ni kuboresha maisha ya wanachama wake.
LAPF pia hutoa mikopo kwa vyama vya ushirika vya kuweka na kukopa ambavyo vina wanachama wachangiaji katika mfuko huo.
Naye Mkurugenzi wa Huduma kwa wanachama, Valerian Mablangeti amesema  mfuko umeweka kiwango cha chini cha riba kwa mikopo yake ikiwa ni juhudi za kuwanufaisha wanachama wake kwa kujipatia mikopo hiyo.
Mfuko huo pamoja na kutoa mikopo hiyo kiwemo ya makazi pia inatoa mafao ya uzazi. Fao hilo ni moja ya mafao sita yanayotolewa kwa mujibu wa sheria.
Mkurugenzi wa Uwekezaji wa LAPF, Rose Metta amesema kwamba mfuko huo umewekeza katika majengo ya biashara. Majengo hayo ni pamoja na Millennium Tower, LAPF tower na Mwanza Comercial Complex ambalo bado linajengwa kwa ushirikiano wa LAPF na jiji la Mwanza.

MADEREVA WA MABASI KANDA YA ZIWA WAGOMA

Abiria waliokuwa wanasafiri kwa mabasi kutoka Kanda ya Ziwa kuelekea mikoa ya Pwani na Kaskazini, juzi walijikuta wakilazimika kuchelewa kufika mjini Singida kwa zaidi ya saa tatu kutokana na mgomo wa madereva wao.
Madereva hao, walimlalamikia Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoani Singida, Mohammed Likwata kwamba eneo lote la barabara kuu ya Singida limejaa alama zinazoonesha mwendo kasi wa kilomita 50 tu kwa saa na hakuna vibao vinavyofuta ukomo huo wa mwendo; hivyo kusababisha kukamatwa kwao kila wanapoendesha mwendo wa zaidi ya km 50.
Walimweleza Kamanda Likwata walipowasili mkoani Singida madai yao mengine kuwa ni pamoja kukithiri kwa rushwa na faini zisizofuata haki.
Walidai kuwa askari usalama barabarani mkoani Singida huwadai malipo ya Sh 200,000/- kwa kosa la mwendo kasi lakini risiti inayotolewa huwa ya Sh 30,000/- tu.
Lakini pia walalamikia tozo ya Sh 10,000 kila basi linapotoka getini katika vituo mbalimbali wanavyopitia katika safari zao na kusema kuwa hawajui fedha hizo ni kwa ajili ya shughuli gani kwa kuwa
hawapewi stakabadhi.
Abiria hao walendelea kumweleza wandishi wa habari hizi kwamba kutokana na uonevu wa askari wa usalama barabarani mkoani Singida wanaowakamata madereva kwa madai ya kwenda mwendo kasi, walipofika eneo la Malendi,  mpakani mwa Singida na Tabora, walipunguza sana mwendo wao.
Kutokana na madereva hao kuendesha  kwa mwendo wa taratibu kwa kile walichodai kuogopa kumulikwa na 'tochi' ya askari wa usalama barabarani, mabasi hayo zaidi ya 50 yaliingia mjini Singida saa tisa mchana badala ya muda wake wa kawaida wa saa sita mchana.
Katika kikao chao na Kamanda Likwata aliwasihi madereva hao kuendelea nasafari na kwamba malalamiko yao yatashughulikiwa wiki hii, pendekezo amblo lilikubaliwa na madereva na kisha kuendela na safari.

BABA WA MAREHEMU ASUSA KUMZIKA MWANAWE

Baada ya vuta nikuvute  iliyosababisha uhasama mkubwa  baina ya familia mbili mjini hapa  wakigombea  kuuzika mwili  wa mtoto  mwenye umri  wa mwaka mmoja na nusu,  hatimaye  familia ya  baba mzazi wa marehemu  imekubali 'yaishe' na kuruhusu  familia  ya mama  mzazi  kumzika mtoto huyo.
Shangazi ya marehemu, Evelyne Komba amebainisha kuwa  maamuzi  hayo yalifikiwa juzi baada ya  kuusindikiza  mwili wa marehumu  ili uhifadhiwe  katika  chumba  cha maiti  katika Hospitali ya  Wilaya  ya Mpanda,  chini ya ulinzi mkali  wa Jeshi  la Polisi  kupitia  Kikosi  cha Kutuliza  Ghasia (FFU).
Aliongeza kuwa vurugu zilizotokea  makaburini  kwa  ndugu  wa baba mzazi wa marehemu  kucharazwa  fimbo  na  kudungwa 'mangumi' baada ya familia ya mama wa marehemu  kufukia  kaburi lililochimbwa na  familia ya  baba mzazi wa  marehemu  ndio  kulikochochea  uhasama  mkubwa  baina yao.
Shangazi huyo wa marehemu alisema ndipo walipolazimika kuita Polisi ambao waliweka ulinzi mkali  nyumbani  kwa  bibi  ya marehemu  mtaa wa Kawajense   Madukani, ukifanyiwa tarartibu  za  maziko na kuamuru mwili huo kurejeshwa  katika  chumba cha maiti  hospitalini.
"Mwili huo hatimae   ulichukuliwa  na  'defender' (gari la polisi)  la Polisi  nyumbani kwetu  nasi  upande  wa  familia ya baba wa marehemu  tulipanda  gari hilo na kuusindikiza   mwili  huo  mpaka  uliohifadhiwa  mochwari. Ndipo hapo hapo  tulipokutana na kufikia maamuzi hayo,"  alisema Evelyne.
Hata hivyo alikiri kuwa  wao  familia  ya  baba  wa  marehemu wote  walizira kuhudhuria maziko  ya mtoto  huyo  wakihofia  usalama wa maisha yao.
"Hatukuweza kuhudhuria  maziko  ya mtoto Junior  kwa  sababu  bado kuna uhasama mkubwa baina ya familia  hizi  mbili  sasa kule  kuna  vifaa  vya kuchimbia  kaburi  vikiwemo  sepetu, majembe  vingeweza  kutumika  na wenzetu kutudhuru.Tuliona  tuepushe  dhahama hiyo  kwa kutokwenda kuhudhuria  maziko  ya  mtoto  huyo,"  alisema  kwa  hisia kali .
Akizungumza na mwandishi  wa  habari hizi,  baba  wa marehemu Joseph Bacho (26),  alikiri kuwa amejisikia huzuni kubwa kwa kukosa  kuhudhuria maziko ya mwanae Junior akidai anafikiria kuwachulia hatua zaidi  za kisheria hata hivyo hakuzifafanua.
"Najisikia huzuni kubwa  nilihofia usalama  wa maisha yangu, hivyo sikuweza kuhudhuria maziko  ya mwanangu  Junior. Ujue  uhasama  wa  wakwe zangu uliibuka  baada ya Junior kufariki  dunia,  wakidai eti  hawanitambui kama  baba  yake mzazi  marehemu  kwa  sababu zijatoa  posa. Sasa kwa nini wadai baada ya mtoto kufikwa na umauti badala ya kunidai  akiwa bado yu hai?" anahoji  Joseph .
Baadhi ya wanandugu  waliohojiwa na  mwandishi,  kwa masharti  ya
kutoandikiwa  wamekiri  kuwa   familia ya  mama mzazi  wa marehemu iliuchukua mwili  huo  saa  nane mchana,  katika  chumba cha kuhifadhia maiti  hospitalini hapo  na  kuustiri  saa  12 jioni jana.
Familia hizo mbili  zote  zikiishi  mtaa mmoja wa Kawajense Madukani, mjini hapa, zilijikuta zikiingia katika uhasama mkubwa hivi kiasi cha kupigana fimbo na ngumi makaburini katika ugomvi wa kugombea kuzika mwili wa mtoto Junior  Bacho.
Sababu kubwa ya mpasuko huo imeelezwa kuwa ni mahari, kwani wazazi upande wa mama wa mtoto huyo walikuja juu na kumzuia baba wa mtoto, Joseph Bacho asishiriki katika shughuli zozote za maziko ya mtoto wake wakidai hawamtambui kwa kuwa hajatoa mahari kwa binti yao.
Inaelezwa kuwa, Joseph na mzazi mwenzake, Anna Kizo (20) walimzaa mtoto Junior Bacho nje ya ndoa, ambapo hadi umauti unamfika mtoto huyo, baba yake mzazi alikuwa hajajitambulisha kwa upande wa mwanamke wala kutoa mahari.
Na kwamba, tangu kuzaliwa kwa mtoto huyo, alikuwa akiishi na kulelewa na mama yake mzazi, Anna nyumbani kwa wazazi wake.
Kwa mujibu wa mashuhuda vurugu hizo ziliibuka baada ya upande wa ndugu wa baba wa mtoto kuweka msiba nyumbani kwao na kuandaa taratibu za kumzika mtoto huyo.
Hata hivyo, kitendo hicho kilipingwa na upande wa mama wa mtoto, ukisema ndio wenye haki ya kumzika mtoto huyo ambaye hawakuwahi kumtambua kisheria baba yake mzazi.
Ndugu wa upande wa baba ulifanikiwa kuchimba kaburi, kuutoa mwili mochari na kuufikisha nyumbani tayari kwa maziko, lakini vurugu za upande wa pili ikiwa pamoja na ndugu upande wa mama kufukia kaburi, zilisimamisha shughuli zote, huku malumbano yakishika hatamu hadi askari wa jeshi la polisi kupitia Kikosi chake cha Kuzuia Fujo (FFU) kilipolazimika kuingilia kati na kusimamia shughuli na kuurudisha mwili katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda.
Inaelezwa kitendo cha upande wa mama wa mtoto kufukia kaburi ndiko kulikochangia kuchochea vurugu hadi FFU walipoingia kati.
Ilivyoanza Mkasa mzima unadaiwa kutokea mtaani hapo Alhamisi wiki iliyopita, siku ambayo mtoto huyo alifariki dunia katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda alikokuwa akiuguzwa na shangazi yake, Evelyne Komba na bibi yake mzaa baba, Teddy Francis.
Inaelezwa kuwa, wakiamini wana haki zote za kumzika mtoto huyo, waliuchukua mwili na kuweka msibani nyumbani kwao, jambo lililopingwa na upande wa mama wa mtoto waliokuja juu na kusema hawamtambui baba wa mtoto kwa kuwa hakuwa ametoa mahari.
Inadaiwa Joseph aliamua kumchukua mwanae huyo Juni 18 , mwaka huu kwa nguvu kutoka kwa mama yake mzazi na kumpeleka hospitalini alikolazwa kwa matibabu baada ya kubainika kuwa anasumbuliwa na utapia mlo mkali .
Kwa mujibu wa mashuhuda ndipo upande wa ndugu wa mama mzazi wa marehemu walipozira ikidaiwa kuwa hawakuweza kufika hata siku moja kumjulia hali mtoto huyo aliyekuwa akiuguzwa hospitalini hapo na shangazi yake Evelyne na bibi yake Teddy hadi umauti ulipomfika .
Licha ya upande wa ndugu wa mama mzazi wa marehemu kushushiwa tuhuma na lawama hizo nzito waliendelea na msimamo wao kwamba walikuwa na haki ya kumzika marehemu hivyo nao wakaamua kuweka msiba nyumbani kwa mama wa marehemu katika.
Ndipo , Juni 27 wazee wa Mtaa wa Kawajense waamua kuingilia kati mgogoro huo kwa kuzikutanisha pande hizo mbili zilizokuwa zikivutana na kufikia uamuzi kuwa msiba uwe nyumbani kwa baba wa marehemu.
Kufutia uamuzi huo shangazi wa marehemu aliongoza ndugu zake akiwemo baba mzazi wa marehemu hadi chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya wilaya ya Mpanda mjini hapa na kuuchukua mwili wa marehemu kisha kuupeleka nyumbani kwa bibi ya marehemu kwa ajili ya maandalizi ya maziko yake.
Maziko ya mtoto huyo yalipangwa kufanyika katika makaburi ya Kawajense ÐMsufini, ambako upande wa ndugu wa baba mzazi wa marehemu walichimba kaburi katika eneo hilo, lakini muda mfupi baada ya kukamilisha kuchimba kaburi hilo ndugu wanaodaiwa wa upande wa mama mzazi wa marehemu waliwawavamia wachimba kaburi na kuwalazimisha kulifukia .
Waombolezaji waliokuwa msibani nyumbani kwa bibi ya marehemu baada ya kutaarifiwa tukio hilo,lililotokea makaburini walitimua mbio na kuelekea makaburini na kukuta baadhi ya wanandugu upande wa mama wakimalizia kufukia kaburi hilo.
Walipoulizwa sababu za kufukia kaburi hilo, walianza kufoka ndipo inadaiwa kundi la ndugu wa mama wa marehemu waliibuka na kuanza kuwashambulia kwa kuwacharaza fimbo ndugu wa baba mzazi wa marehemu .

MWILI WA NG'WANAKILALA KUZIKWA KESHO

Mwili  wa nguli katika tasnia ya habari, Nkwabi Ng'wanakilala unatarajia kuwasili leo jioni kutokea hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza, na kuzikwa kesho shambani kwake Kibamba CCM, jijini Dar es Salaam.
Ng'wanakilala ambaye hadi mauti yanamkuta alikuwa  Mhadhiri Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT), alifariki juzi usiku wa kuamkia Jumamosi katika hospitali ya Bugando.
Akizungumza na HabariLeo kuhusiana na taratibu za mazishi, mtoto wa marehemu, Fumbuka Ng'wanakilala, alisema mwili wa mwanahabari huyo, utawasili leo jioni na kesho utazikwa shambani kwake.
"Wanandugu tuko huku shambani kwake tukiendelea na taratibu nyinginezo za mazishi ili kuhakikisha tunauhifadhi mwili wa mzee," alisema Fumbuka na kuongeza kuwa Misa kwa ajili ya mazishi itafanyikia hapo hapo shambani kabla ya kuzika.
Wakati wa uhai wake, Ng'wanakilala aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Radio Tanzania Dar es salaam (RTD),sasa TBC na lililokuwa Shirika la Habari Tanzania (Shihata).
Kadhalika wakati wa uhai wake alifanya kazi katika tasnia ya habari na kushiriki katika masuala mbalimbali ya habari kama mhadhiri, mtafiti, mshauri na mwandishi na mchapishaji binafsi wa vitanu ma majarida mbalimbali.

ZITTO KABWE ATAKA BUNGE KUDHIBITI WATENDAJI SERIKALINI

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe amesema Bunge lina kila sababu kupitia sheria yake ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kulinda hadhi yake kutoka kwa watendaji.
Taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa jana, kuhusu madai ya kwamba kiasi cha Dola za Marekani milioni 250 zilizopaswa kuendelea kuwapo katika akaunti ya 'Tegeta Escrow Account' na sio kulipwa katika akaunti ya PAP.
Alidai kwamba watendaji wanatoa matamshi ya kuonyesha kwamba chombo hicho ni chombo cha watu wasiofaa na kwamba watu wanaofaa wanazungumza nje ya Bunge.
Zitto alisema watendaji  wa aina hiyo kama wana ushahidi wa rushwa dhidi ya mbunge ama yeyote hawapaswi kupayuka ovyo; bali kwa nafasi zao wanaweza kuwasiliana na vyombo vya dola kama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na polisi ili kuchunguza na kuchukua hatua.
Alisema ipo haja ya kufumbua macho kuona na kuondoa  hisia binafsi zenye kubebwa na itikadi, chuki na misimamo ya kisiasa na kuwa wazalendo katika kusimamia utaifa.
Zitto alisema inatarajiwa kwamba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), atafichua ukweli wa suala hilo na TAKUKURU iwafikishe mahakamani wahusika bila kujali nyadhifa zao
serikalini.
Kadhalika alisema uchunguzi huo ni muhimu ukawalenga vigogo na wanasiasa wakubwa wakiwamo watendaji waandamizi wa Wizara ya Nishati na Madini.

WAJAWAZITO 900 WAJIFUNGULIA KWA WAKUNGA WA JADI

Wajawazito wapatao 900 wamejifungilia kwa wakunga wa jadi  wilayani Kalambo katika mkoa wa Rukwa kwa kipindi kilichoanzia Januari  hadi Mei mwaka huu.
Mganga Mkuu wa Wilaya  ya Kalambo, Dk Akilimali Mponzemenya alisema wanawake hao hao  waliojifungulia kwa wakunga wa jadi  kwa kipindi  hicho  cha miezi  takribani mitano,  ni asilimia 25  ya akina  mama 2,685  waliojifungua  katika  vituo  vya kutolea  huduma ya afya wilayani  humo.
Kwa upande wa huduma ya wagonjwa  majumbani, Dk Mponzemenya  alieleza kuwa idadi ya  wagonjwa 560 ambao wanaishi na Virusi Vya Ukimwi, wanahudumiwa majumbani na kati yao  wanaume  ni 218  na wanawake 342.
Alizitaja baadhi ya changamoto zinazoikabili sekta ya Afya wilayani humo kuwa ni pamoja na baadhi ya akina mama kuendelea kujifugulia kwa wakunga wa jadi  badala  ya  kwenda  kwenye vituo  vya kutolea  huduma ya afya.
Changamoto  zingine alizitaja kuwa  ni  uhaba wa watumishi  wa afya wenye taaluma  katika  vituo vingi  vinavyotoa huduma pamoja na upungufu  wa vyombo  vya  usafiri  yakiwemo  magari na pikipiki .
Pia  kitengo  cha  dawa  wilayani  humo  hakina  stoo  ya kudumu  kwa ajili ya  kuhifadhia na hivyo dawa kutunzwa eneo lisilo rasmi.

COSTECH YAFADHILI MAKUNDI BUNIFU 26 YA UZALISHAJI

Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH) imetoa zaidi ya Sh milioni 200 kusaidia kongano bunifu  26 zinazozalisha na kutengeneza bidhaa za aina mbalimbali  hapa nchini kwa kipindi cha miaka minne iliyopita.
Msaada huo unalenga kuchochea ubunifu na ushindani wa soko kwa kuwezesha kutengeneza bidhaa za aina mbalimbali zikiwa na ubora na viwango vya kimataifa.
Hayo yalisemwa na Mtafiti ambaye pia ni Mratibu wa Mafunzo kutoka  Tume hiyo Furaha Kabuje juzi mjini hapa kabla ya Mkuu wa Mkoa huo, Joel Bendera, kufunga mafunzo ya kongano bunifu wa bidhaa za aina mbalimbali nchini.
Kabuje alisema tume hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha sayansi na teknolojia inawasaidia wananchi,  na kwamba  kongano zitakazoonyesha juhudi binafsi ndizo zinazosaidiwa kwa kupatiwa Sh milioni nane kila moja ili ziwasaidie kutekeleza mipango ya kuendeleza kongano zao.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa Bendera, aliwataka washiriki hao kutumia ujuzi na maarifa waliyoyapata katika kuendeleza kongano mbalimbali nchini, ili waingie katika ushindani wa biashara utakaokidhi viwango vya  soko la kimataifa.
Alifafanua kwamba Serikali itaendelea kuunga  mkono na kushiriki
kikamilifu katika juhudi za kuendeleza kongano kwa kuwa zimeonyesha mafanikio makubwa  katika kuongeza pato la taifa , ajira na maendeleo ya jamii.
Naye mwakilishi wa kongano la mafuta ya alizeti kutoka mji mdogo wa Kibaigwa, wilayani Kongwa, mkoani Dodoma, Ringo Iringo, aliipongeza Tume hiyo kwa kufadhili mafunzo hayo ambayo ni chachu ya mabadiliko ya kibiashara yatakayolenga uzalishaji ubora wa bidhaa.
Mafunzo hayo ya siku nne, yaliwashirikisha wawakilishi wa kongano za ubunifu wa bidhaa mbalimbali kutoka mikoa ya Arusha, Kigoma, Dodoma, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Kilimanjaro na Morogoro.

YASEMAVYO MAGAZETI YA LEO JUMATATU - JUNI 30

USAGAJI SEMBE NYEUSI WAFANYIWA MAJARIBIO

Sembe nyeusi itakayokuwa ikizalishwa katika kinu kikubwa cha kusaga na kuhifadhi nafaka cha mjini Iringa inatarajiwa kuingia sokoni wakati wowote kuanzia sasa baada ya jaribio la usagaji wake kufanyika juzi kwa mafanikio makubwa.
Kazi ya kusaga sembe hiyo kwa mujibu wa Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), Charles Walwa utafanywa na NRFA baada ya kukabidhiwa jukumu hilo na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko iliyokabidhiwa kinu hicho na serikali kutoka kwa lililokuwa Shirika la Usagishaji la Taifa (NMC).
Tani tano za mahindi zilitumika katika jaribio hilo lililochukua zaidi ya saa moja mbele ya ushuhuda wa maafisa mbalimbali wa bodi hiyo, wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula na wafanyakazi wa kinu hicho pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dk Christine Ishengoma.
"Kama mlivyoona jaribio limefanikiwa katika mchakato wa kukifanya kinu hiki kianze uzalishaji, hiyo ni baada ya kusimama uzalishaji mwanzoni mwa miaka ya tisini; unga umezalishwa kama mlivyouonaÉhatua inayofuata ni kuchunguza ubora wake," Walwa alisema.
Alisema unga huo utapelekwa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Shirika la Viwango Tanzanoa (TBS) ili kuhakiki ubora wake kabla ya uzalishaji wake kuanza rasmi kwa ajili ya kuingizwa sokoni.
Dk Ishengoma alisema kufufuliwa kwa kiwanda hicho kutaongeza
uhakika wa soko la nafaka zinazozalishwa na wakulima wa mkoa ya Iringa na ile ya jirani na hivyo kuongeza wigo wa ajira katika sekta ya kilimo.
Meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wa NFRA, Abdillah Nyangasa, alisema kinu hicho kimerudi katika hali yake ya kawaida ya uzalishaji baada ya kufanyika kwa matengenezo na ukarabati uliogharimu zaidi ya Sh Milioni 132.
Alisema matengenzo na ukarabati huo ulihusisha pia ununuzi wa mtambo maalumu wa kudhibiti mfumo wa umeme katika kinu hicho. Tayari wamiliki wa kinu hicho wana tani 10,000 zitakazotumika kama mtaji wa awali.

TIB YAWAKOPESHA TREKTA WAKULIMA BUNDA

Benki ya TIB imetoa mkopo wa trekta tatu zenye thamani ya zaidi ya Sh   milioni 83, kwa wananchama watatu wa chama cha kuweka akiba na kukopa (Chiringe Saccos) kilichoko mjini Bunda ili waweze kuendesha kilimo vizuri na hatimaye kujiunua kiuchumi.
Mkopo huo umekabidhiwa jana na Afisa Ushirika wa wilaya ya Bunda, Saulo Lunyeka, kwenye hafla fupi iliyofanyika katika ofisi za chama hicho mjini Bunda.
Akikabidhi mkopo huo Lunyeka alisema kuwa, umetolewa na benki hiyo ili wakulima hao ambao ni wanachama wa Saccos waweze kufanya kazi yao ya kilimo kwa ufanisi zaidi, badala ya kulima kwa kutumia majembe ya mikono.
Aliwaasa wanachama hao kurejesha mkopo huo kwa muda muafaka, ili wanachama wengine nao waweze kukopeshwa na kuongeza kuwa wananchi wanapaswa wajiunge kwenye vikundi na vyama vya kuweka akiba na kukopa ili waweze kupata fursa ya kukopesheka na vyombo vya kifedha.
"Mimi nipende tu kuwaasa ndugu wanachama kwamba zingatieni
msharti ya mkopo huu, rejesheni kwa wakati muafaka ili wnzenu pia waweze kukopesheka, lakini pia nitumie fursa hii kuwaambia wananchi wengne wajiunge kwenye vikundi na Saccos kama hii ili waweze kupata fursa ya kukopesheka kwenye vyombo vya kifedha," alisema.
Mwenyekiti wa Saccos hiyo, Robert Masatu, alisema walianza
mchakato wa kuomba mkopo huo mwaka 2012 na kwamba trekta hizo zitawasaidia wakulima kulima maeneo makubwa ya mashamba na kwa wakati muafaka kulingana na msimu wa mvua ulivyo.
Masatu alisema kuwa matarajio yao ni kuhakikisha wanachama wote wa Chiringe Saccos ambao ni 69, wanapata mkopo huo wa trekta kwani wengi wao ni wakulima, ili waweze kulima kwa kutumia teknorojia hiyo badala ya kutumia majembe ya mikono, ambayo hutumia muda mwingi kulima na kuwachosha kwa
haraka.
Wakulima waliopata trekta hizo ni Robert Masatu, Opigi Ocharo na Nyerere Odera, ambao wote ni wakazi wa wilayani Bunda, na kwamba watarejesha mkopo huo kwa muda wa miaka minne, ambapo kila miezi mitatu watakuwa wanarejesha kiasi cha Sh milioni 3.9.

MOROGORO YAWEZESHA VIKUNDI VYA WANAOSHI NA HIV

Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro,imetoa hundi yenye thamani ya Sh milioni 22 kwa vikundi vya Wajasiriamali vya watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (WAVIU) viendeleze shughuli za uzalishaji mali utakaowapatia vipato na maisha bora.
Mratibu wa Ukimwi katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Florence Mwambene, alisema kutolewa kwa fedha hizo ni  kuviwezesha vikundi hivyo kujitegemea kiuchumi.
Hata hivyo alivitaja vikundi vilivyokabidhiwa fedha ni pamoja na Mtandao wa Watu wanaishi na VVU wilaya ya Morogoro uliopatiwa hundi ya Sh milioni 20, Tushikamane Vijana Sh milioni moja sambamba  na Tushikamane Wanawake  waliopatiwa kiasi kama hicho.
Kwa mujibu wa Mratibu wa Ukimwi wa Halmashauri hiyo, kwa
kushirikiana na jamii pamoja na Asasi zingine ilianza uundaji wa vikundi vya watu wanaoishi na VVU tangu mwaka 2008/2009.
"Tulianza na vikundi vitatu ambavyo ni Waviumka Kata ya  Mkambarani, Waviunge Kata ya Ngerengere na Upenzo Moro V Kikundi cha watumishi," alisema Mratibu huyo.
Hata hivyo alisema, katika Halmashauri hiyo kuna vikundi 160 kati ya hivyo 100 vya wanawake na 60 vya vijana vinajishughulisha na kazi mbalimbali za uzalishaji mali.
Mratibu huyo Ukimwi wa Halmashauri ya wilaya hiyo, alizitaja shughuli hizo ni pamoja na ufugaji, kilimo na kufanya biashara kwenye masoko na kwamba miradi hiyo itawawezesha kukabiliana na kuondokana na utegemezi na kubadilishana uzoefu wao kwa wao.

CRDB YAHADHARISHA WATEJA KUWA MAKINI NA MITANDAO

Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi, kutoa taarifa zao muhimu za kibenki, jambo ambalo linahatarisha usalama wa fedha zao zinazohifadhiwa na benki hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki CRDB, Dk Charles Kimei, alisema hayo Dar es salaam mwishoni  mwa wiki,  katika mkutano uliohusu  uboreshwaji wa huduma za benki kupitia simu za mikononi 'simbanking' na njia za wateja kujilinda na uhalifu kwa njia ya mtandao.
Kuhusu matapeli wa mitandao, alisema kumeibuka mchezo kwa baadhi ya mitandao ya kijamii, ikijaribu kuwalaghai wateja kwa kuwaomba taarifa za akaunti zao ili kufanya uhalifu.
"Huduma ya simbanking ni salama na imepitia viwango vyote vya kiusalama jambo muhimu ni kuwasisitiza wateja kutunza vizuri taarifa za akaunti zao ikiwemo kadi zao na namba za siri ili kujiepusha na matapeli hao," alisema Dk Kimei.
Alisema wananchi wanatakiwa kuwa makini na kundi hilo, wasikubali kudanganyika kwa kutoa taarifa zinazohusiana na nyaraka za benki zao na kusisitiza kuwa ni marufuku kutoa taarifa hizo hata kwa wafanyakazi wa benki.
Dk Kimei alisema pamoja na kwamba benki hiyo inawapigia simu wateja wao wakiwataka kukamilisha usaili wao kuhusiana na kuingia katika  mfumo wa simbanking, watambue kuwa hawatoulizwa kutoa taarifa zozote za akaunti zao.
Kuhusu mbinu wanazotumia matapeli, Mkurugenzi wa Idara Hatarishi, James Mabula, alisema, huwapigia simu wakijifanya kuwa wakurugenzi ama wafanyakazi wa benki hiyo na kisha kuwaghilibu kwa kutaka kupatiwa namba za siri za akaunti husika.

Sunday, June 29, 2014

JICHO LA TATU


MAHARI YAZUA BALAA, BABA WA MTOTO AZUIWA KUZIKA

Familia mbili mjini hapa zimejikuta zikiingia katika uhasama mkubwa, kiasi cha kupigana fimbo na ngumi makaburini katika ugomvi wa kugombea kuzika mwili wa mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu.
Sababu kubwa ya mpasuko huo imeelezwa kuwa ni mahari, kwani wazazi upande wa mama wa mtoto huyo walikuja juu na kumzuia baba wa mtoto, Joseph Bacho mkazi wa Mtaa wa Kawajense- Madukani   mjini  hapa asishiriki katika shughuli zozote za maziko ya mtoto wake wakidai hawamtambui kwa kuwa hajatoa mahari kwa binti yao.
Inaelezwa kuwa, Joseph  na mzazi  mwenzake,  Anna Kizo ambaye pia ni mkazi  wa Mtaa wa Kawajense –Madukani  walimzaa mtoto  Junior Bacho nje  ya ndoa  ambapo  hadi  umauti unamfika  mtoto  huyo, baba yake  mzazi  alikuwa  hajajitambulisha  kwa  upande wa mwanamke wala kutoa mahari.
Na kwamba, tangu kuzaliwa kwa mtoto huyo, alikuwa akiishi na kulelewa na  mama  yake mzazi, Anna  nyumbani kwa wazazi wake katika Mtaa  wa Kawajense.
Kwa mujibu wa waombolezaji ambao hata hivyo hawakuwa tayari kutajwa majina, vurugu hizo ziliibuka baada ya upande wa ndugu wa baba wa mtoto kuweka msiba nyumbani kwao na kuandaa taratibu za kumzika mtoto huyo.
Hata hivyo, kitendo hicho kilipingwa na upande wa mama wa mtoto, ukisema ndio wenye haki ya kumzika mtoto huyo ambaye hawakuwahi kumtambua kisheria baba yake mzazi.
Ndugu wa upande wa baba ulifanikiwa kuchimba kaburi, kuutoa mwili mochari na kuufikisha nyumbani tayari kwa maziko, lakini vurugu za upande wa pili ikiwa pamoja na ndugu upande wa mama kufukia kaburi, zilisimamisha shughuli zote, huku malumbano yakishika hatamu hadi askari wa jeshi la polisi kupitia kikosi chake cha kuzuia fujo (FFU) kilipolazimika kuingilia kati na kusimamia shughuli za kuurudisha mwili katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda.
Inaelezwa kitendo cha upande wa mama wa mtoto kufukia kaburi ndiko kulikochangia kuchochea vurugu hadi FFU walipoingia kati.
Kamanda  wa Polisi  wa Mkoa  wa Katavi, Dhahiri Kidavashari  amethibitisha kutokea  kwa mkasa huo  kwamba  hakuna  mtu  yeyote aliyejeruhiwa katika  vuta nikuvute  hiyo  pia  hakuna  ayekamatwa  kuhusiana na tukio hilo  ambalo ni la kijamii  zaidi.
Mkasa mzima unadaiwa kutokea mtaani hapo Alhamisi wiki hii, siku ambayo mtoto huyo alifariki dunia katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda alikokuwa akiuguzwa na shangazi yake, Evelyne Komba na bibi yake mzaa baba, Teddy Francis.
Inaelezwa kuwa, wakiamini wana haki zote za kumzika mtoto huyo, waliuchukua mwili na kuweka msibani nyumbani kwao, jambo lililopingwa na upande wa mama wa mtoto waliokuja juu na kusema hawamtambui baba wa mtoto kwa kuwa hakuwa ametoa mahari.
“Ujue  katika  mila na desturi  zetu  mtu  kama  amezaa na  msichana  bila kuoana  huwa hatambuliwi  na  upande wa mzazi  wa kike  mpaka  atakapolipa mahari  hapo  ana kuwa na haki  zote  kwa  mwanae …sasa kwa upande  wa Joseph  amezaa  tu  na binti  yetu  nje ya ndoa  hivyo  hatumtambui  mpaka  aje ajitambulishe  na  kulipa  mahari.
“Kwa  utaratibu  huo  Joseph  hana  kabisa  haki  ya  kuweka msiba  wa mjukuu  wetu  wala kumfanyia  maziko  mpaka  akamilishe  taratibu zote za mila na desturi  zetu  ikiwemo  kulipa  mahari  kwa wakwe zake “ alisisitiza mmoja  wa  wanandugu  upande  wa  mama mzazi  wa marehemu .
Licha ya kurushiana maneno  makali  pande  hizo  mbili,  upande wa  ndugu wa  baba mzazi  wa marehemu  waliibuka  na  kumshutumu  mama  na  ndugu zake kushindwa  kumhudumia  mtoto  huyo  wakati alipougua .
Inadaiwa mama  wa marehemu  hakumruhusu kabisa  mzazi mwenzake  kumwona mwanae  alipokuwa   mgonjwa  na kuuguzwa  nyumbani  kwa mama yake  katika Mtaa wa  Kawajense – Madukani  .
“Joseph kila  alipofika  nyumbani  kwa mzazi  mwenzake  ili  kumjulia  hali mwanae  aliyekuwa mgonjwa  hakuruhusiwa kuingia  ndani  kwa mdai  kuwa mtoto alikuwa  amelala  “  anadai  mtoa  taarifa .
Inadaiwa  Joseph  aliamua kumchukua mwanae  huyo Juni  18 , mwaka huu   kwa  nguvu kutoka kwa mama  yake  mzazi  na kumpeleka  hospitalini  alikolazwa kwa  matibabu  baada ya kubainika kuwa  anasumbuliwa na utapia mlo mkali .
Kwa mujibu  wa  mashuhuda  ndipo  upande  wa  ndugu  wa mama mzazi  wa marehemu  walipozira   ikidaiwa kuwa  hawakuweza kufika  hata siku  moja  kumjulia  hali  mtoto  huyo aliyekuwa akiuguzwa  hospitalini hapo  na shangazi  yake Evelyne na  bibi  yake Teddy  hadi  umauti  ulipomfika .
Licha  ya upande  wa  ndugu wa mama mzazi  wa marehemu  kushushiwa  tuhuma na  lawama  hizo  nzito  waliendelea  na msimamo  wao   kwamba walikuwa na  haki ya  kumzika marehemu  hivyo nao  wakaamua kuweka msiba  nyumbani  kwa mama wa marehemu  katika Mtaa  huo  wa Kawajense.
Ndipo juzi , Juni 27 wazee  wa Mtaa  wa Kawajense  waamua kuingilia kati mgogoro  huo  kwa  kuzikutanisha pande  hizo  mbili  zilizokuwa  zikivutana na kufikia uamuzi  kuwa  msiba  uwe nyumbani  kwa  baba  wa marehemu.
Kufutia uamuzi huo shangazi wa marehemu aliongoza ndugu  zake akiwemo  baba mzazi  wa marehemu  hadi  chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali  ya  wilaya ya Mpanda mjini hapa  na kuuchukua mwili wa marehemu kisha kuupeleka nyumbani  kwa  bibi  ya marehemu  kwa ajili  ya maandalizi  ya maziko  yake .
Maziko  ya mtoto  huyo  yalipangwa  kufanyika  katika makaburi  ya Kawajense –Msufini  ambako  upande  wa ndugu wa baba mzazi  wa marehemu walichimba  kaburi katika eneo  hilo,  lakini muda mfupi  baada ya kukamilisha  kuchimba  kaburi  hilo  ndugu  wanaodaiwa  wa upande wa mama  mzazi  wa marehemu waliwawavamia  wachimba  kaburi na kuwalazimisha kulifukia .
Waombolezaji  waliokuwa msibani  nyumbani  kwa bibi ya marehemu baada ya kutaarifiwa  tukio hilo lililotokea makaburini  walitimua mbio  na kuelekea makaburini  na kukuta baadhi ya wanandugu upande wa mama wakimalizia kufukia  kaburi  hilo.
Walipoulizwa sababu za kufukia kaburi hilo,  walianza kufoka ndipo inadaiwa  kundi la ndugu wa mama wa marehemu  waliibuka na  kuanza kuwashambulia kwa kuwacharaza fimbo  ndugu wa baba mzazi  wa marehemu .
Hadi  sasa  mwili  wa mrehemu  huyo umehifadhiwa  mochari  katika Hospitali  ya Wilaya ya Mpanda  hadi  hapo  pande  hizo  mbili  zinazovutana zitakapoafikiana  ndipo  ufanyiwe maziko .

WAHASIBU, WAKAGUZI WA MADENI FEKI KUTIMULIWA KAZI

Muswada wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2014 umepita jana huku Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, akitoa onyo kwa wahasibu watakaopeleka madai ya madeni yaliyochakachuliwa kuwa atawafukuza kazi.
Akichangia hoja jana, Nchemba alisisitiza kuwa Serikali italipa madeni yote lakini baada ya kufanya uhakiki na wakigundua kuwa yaliongezwa, mhasibu na mkaguzi wa mahesabu waliopitisha madai hayo, watafute kazi zingine.
“Hapa kwa kweli tuko tayari kuondoa timu nzima ofisini na kuweka mpya…wako vijana wana shida ya kazi hawajaanza kupasha bora tuwape wao na kama kuna shida ya kisheria, Mama Kombani (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi, Celina), lete sheria  ili fedha za Serikali ziheshimiwe,” alisema.
Alikumbushia mfano uliotolewa na Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum, kuwa katika uhakiki walibaini madeni feki yaliyoletwa Hazina kwa ajili ya malipo.
Katika mfano huo alisema kuna deni lilipelekwa Hazina la Sh milioni 600 kwa ajili ya malipo lakini uhakiki ulipofanyika, deni halisi lilibainika ni Sh laki sita tu. Mfano mwingine ni wa deli la Sh trilioni 1.5 na uhakiki ulipofanyika ikakutwa deni halisi ni la Sh milioni 150.
Naye Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, akizungumzia nidhamu ya fedha za Serikali, alitolea mfano wa Kodi ya Majengo, ambapo alisema nyumba 50 za Dar es Salaam katika mitaa kama ya Oysterbay, Masaki, Msasani na Mikocheni, zinaweza kulipa kodi hiyo katika mji mzima kama wa Mbeya.
“Sasa hizi hazikusanywi, idara za ardhi katika halmashauri kama zimeshindwa kazi hapa ndipo Mwigulu anasema, watoke waingie wengine wafanye kazi,” alisema Malima.
Nchemba pia alitetea uamuzi wa Serikali kwa mashirika yote ya umma na tasisi zinazokusanya maduhuli wapeleke bajeti zao kwa Mlipaji Mkuu wa Serikali ili zidhibitiwe.
“Hivi mnajua leo hii kuna timu nzima ya Shirika inasafiri kwenda nje kufanya semina na wote wanapanda ndege daraja la kwanza na la pili…tunataka semina hizo Mlipaji Mkuu wa Serikali azizuie,” alisema Nchemba.
Pia aliagiza taasisi hizo kuanza kukusanya maduhuli  kwa kutumia mfumo wa kielektroniki, ili kila wanachokusanya  kionekane huku akisisitiza kuwa haiwezekani  Serikali inawataka wafanyabiashara wadogo kutumia mashine za kodi za kielektroniki (EFDs), wakati taasisi za Serikali zinatoa na kutumia risiti za kuandika kwa mkono. 
Kuhusu misamaha ya kodi, Nchemba alimpongeza Waziri wa Fedha Saada kwa kujiondolea madaraka ya kusamehe kodi na kusema huo ni ujasiri mkubwa.
Alisema hata kwa misamaha ambayo imeshatolewa, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), atakwenda kuikagua ili kubaini kama ilitumika kama ilivyokusudiwa.
“Silaha ya fedha ya kupunguza pengo la walionacha na wasionacho ni kutoza kodi kwa matajiri na kumpa huduma masikini…ukimtoza masikini na kumsamehe tajiri, masikini ataendelea kuwa masikini na tajiri ataendelea kuwa tajiri,” alisema Nchemba.
Naye Waziri Mkuya katoka suala la misamaha ya kodi, alisema pamoja na Muswada wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na Muswada wa Menejimenti ya Kodi kusogezwa mbele, Serikali itairejeshwa tena Bunge la Novemba.
“Katika misamaha ya kodi ya mafuta, hakuna siku hata moja faili la misamaha ya kodi linakaa mezani kwangu kwa siku mbili, inauma na inasikitisha sana, tunawapa ruzuku hawa wawekezaji wakati wanapata faida,” alisema Saada.
Nchemba katika hilo, alisema aliwahi kuzungumza na mwekezaji mmoja kuhusu msamaha wa kodi, akamuuliza ni wapi kwingine duniani kitu hicho kinafanyika, akamjibu hakuna lakini kwa kuwa Tanzania tuliweka katika sheria kuwa wanastahili msamaha, ndio maana wanafuatilia stahili yao hata kama wanapata faida.
Kuhusu Ushuru wa Ujuzi na Maendeleo (SDL) ambao unakwenda katika Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu, ambayo baadhi ya wabunge walipendekeza ipunguzwe, Nchemba alisema haitapunguzwa.
“Hiki ndio chanzo muhimu cha fedha za Bodi mnataka kipunguzwe wakati mwaka jana zaidi ya wanafunzi 12,000 walikosa mkopo?
“Mtoto anasomeshwa kwa vitumbua mpaka anafika kidato cha sita na mimi ningependa kila anayekubalika kujiunga na chuo apate mkopo, si fedha za bure ni mkopo ambao akimaliza shule analipa, hapa wanakosa si haki,” alisema huku akitetea kuwa kodi hiyo isipunguzwe.

PAPA FRANCIS ATIMUA ASKOFU KWA KUDHALILISHA WATOTO

Balozi wa zamani wa Vatican katika nchi ya Jamhuri ya Dominica, Monsinyori Jozef Wesolowski ametiwa hatiani na Mahakama ya Kanisa Katoliki kwenye tuhuma za kudhalilisha watoto.
Kutokana na kutiwa hatiani huko amepokwa upadre wake. Monsinyori Wesolowski amekuwa kiongozi wa juu kuteuliwa na Papa kutiwa hatiani na kupewa adhabu hiyo ya kupokwa upadri.
Taarifa ya Vatican ilisema Monsinyori Wesolowski alikutwa na hatia na Mahakama hiyo ya Usharika wa Mafundisho ya Imani katika siku za hivi karibuni: kwa adhabu hiyo ina maana hataweza kutekeleza majukumu yake kama Padre.
Wesolowski amepewa miezi miwili ya kukata rufaa.
Lakini pia anakabiliwa na mashtaka katika Mahakama ya Makosa ya Jinai ya Vatican. Kwa kuwa ni Mwanadiplomasia wa Kipapa yeye ni raia wa mji wa nchi hiyo.
Papa alimrejesha Vatican, Wesolowski ambaye ni mzaliwa wa Poland Agosti 21, 2013 na kumfuta kazi baada ya Askofu wa Santo Domingo, Kadinali Nicolas de Jesus Lopez kumueleza Papa Francis kuhusu kuwepo kwa tetesi kuwa Wesolowski aliwadhalilisha watoto wa kiume akiwa Jamhuri ya Dominica.
Mamlaka za Dominican hatimaye zilianza uchunguzi  lakini hazikumshtaki. Poland, pia ilianza uchunguzi dhidi ya Wesolowski.
Wesolowski ni Ofisa wa Juu Vatican kuchunguzwa kwa tuhuma za udhalilishaji watoto na kesi yake iliibua waswali iwapo Vatican, kwa kumuondoka katika mamlaka ya Dominica ilikuwa ni kumlinda na kuanzisha uchunguzi wake kabla ya mamlaka za taifa hilo la Caribbean.
 Hata hivyo Vatican haijawahi kusema iwapo Wesolowski alishawahi kujitetea kuhusiana na tuhuma hizo na hajawahi kutoa mawasiliano yoyote kwa mawakili wake.
Kesi hiyo imekuwa ikichukuliwa kwa umakini kwani Wesolowski alipewa upadirisho wake na Uaskofu na  Papa St John Paul 11 ambaye pia ni Raia wa Poland.

DC AMWAGA CHOZI KWENYE MKUTANO WA HADHARA

Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Elibariki Kingu, juzi aliwashangaza wengi baada ya kuangusha machozi mbele ya wananchi waliofurika kumsikiliza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Mtunguru, Kata ya Bukoko wilayani hapa.
Kingu alianza kutokwa na machozi hata kabla ya mkutano, baada ya kuoneshwa na Mwenyekiti wa kijiji hicho, Siminzaga Mange nyumba ya mwalimu iliyojengwa kwa nguvu za wananchi zaidi ya miaka minane lakini mpaka sasa haijamaliziwa kwa kupauliwa.
Nje na nyumba ya mwalimu, Kingu aliendelea kutokwa na machozi alipoambiwa kuna jengo la nyumba ya mganga ambalo nalo limejengwa kwa nguvu za wananchi lakini bado halijapauliwa mabati na serikali licha ya wananchi kuchangia nguvu zao.
Mkuu huyo, baada ya kutembea katika kijiji hicho kwa miguu kwa zaidi ya kilomita 30 akijionea miradi mbalimbali ya maendeleo, alikaribishwa na Mwenyekiti wa kijiji azungumze na wananchi ili awahamasishe kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
Akizungumza, huku akiendelea kutokwa na machozi, alisema: “Ndugu zangu wananchi wa kijiji cha Mtunguru mimi nimesikiliza maelezo ya mwenyekiti wenu wa kijiji na kujionea mengi, nimeumizwa sana…haiwezekani wananchi wanachangia nguvu zao halafu sisi kama serikali tunashindwa kukamilisha majengo hayo hii ni aibu kubwa kwa serikali.
“Kwa kuanzia, mbao zote 670 zilizokamatwa na maliasili zitatumika kupaua nyumba ya mwalimu pamoja na nyumba ya mganga na mtu yeyote atakayehoji mimi nitajibu kwa niaba ya serikali.
“Mabati na saruji nitatoa mimi mwenyewe, hivyo lazima watendaji wa vijiji na vitongoji msimamie kwa makini mbao hizo, mabati na saruji nitakavyovileta. Atakayeonekana kukwapua vitu hivi nawaambieni sitasita kumkamata na kumpeleka katika vyombo vya sheria.”
Kutokana na kauli hiyo, wananchi walishangilia na wamempongeza mkuu huyo kwa uamuzi aliouchukua.

UVCCM YAPINGA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA ZANZIBAR

Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) imesema kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar si tiketi itakayoweza kumsaidia Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad kushinda na kuwa Rais wa Zanzibar katika  uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015.
Naibu Katibu Mkuu wa  UVCCM Zanzibar, Shaka Hamdu Shaka alisema hayo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Binti Amran Jimbo la Mpendae, Kisiwani Unguja .
Shaka alisema si jambo  rahisi kama inavyofikiriwa na baadhi ya viongozi wa CUF kudai   Maalim Seif  mwaka 2015  atashinda kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao.
Katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya sasa, Maalim Seif ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Katika mkutano huo, Shaka alizungumzia pia masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuitaka Serikali kuwakabili na kuwaasa viongozi wanaochanganya dini na siasa ili  kwa kutumia nafasi zao wasiweze kuleta madhara kwa jamii.
Akizungumzia  matukio ya uhalifu katika ukanda wa Afrika Mashariki sambamba na milipuko ya mabomu katika miji ya Mombasa, Arusha na Zanzibar, Shaka alivitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha wanafanya kazi kwa ushirikiano  ili kukabiliana na tishio hilo.
Aliviomba vikosi vya ulinzi na usalama kuwa makini katika kipindi hiki kigumu kuliko wakati wowote,  kufanya kazi kwa pamoja ili kubaini mitandao ya kihalifu akisema ikiwa mazingira ya utulivu na amani yatatoweka, hakutakuwa na mipango ya maendeleo aidha ya kiuchumi, kisiasa au kijamii.

MATUMIZI YA NISHATI YA MAGOGO YAKERA WADAU

Wakati Serikali ya Tanzania ikiungana na nchi za Kenya na Uganda na Umoja wa Mataifa kupiga vita biashara ya magogo katika nchi za ukanda wa maziwa makuu, uongozi wa kiwanda cha kutengeneza nguo cha Sunflag cha jijini hapa umeendelea kutumia magogo kuendeshea mitambo ya kiwanda hicho kikongwe nchini.
Katika azimio lililopitishwa Alhamisi wiki hii jijini Nairobi nchini Kenya na  Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEA), nchi za Tanzania, Kenya na Uganda zilikubaliana kwa pamoja kuungana na umoja wa Mataifa kupinga uvunwaji wa magogo katika nchi hizo ili kunusuru uharibifu mkubwa wa mazingira ambao unaelezwa kufanyika katika ukanda wa maziwa makuu.
Kwa mujibu wa Msemaji wa kiwanda cha Sunflag, Harun Mahundi, kiwanda hicho kimekuwa kikitumia magogo kwa miaka kadhaa sasa baada ya kuacha kutumia mafuta mazito kutokana na upatikanaji wake na gharama zake kuwa kubwa.
Meneja wa shamba la miti la Serikali la Olmotony lililoko Arumeru, jijini Arusha, Khadija Kiimu alipoulizwa kuhusu uuzaji wa magogo hayo licha ya kupigwa marufuku, alikiri ofisi yake kuuza magogo yanayotokana na miti inayozalishwa katika msitu wake kwa wafanyabiashara mbalimbali ijapokuwa hakuwa na uhakika wa mahali ambapo magogo hayo yamekuwa yakipelekwa.

KILA KATA TARIME KUPATA GAWIO SHILINGI MILIONI 30

Halmashauri Mama ya Wilaya Tarime yenye Kata 24, imepitisha na kupendekeza mgawo wa sh milioni 30 kwa kila Kata ikiwa ni sehemu ya mgawo wa mrabaha kutoka mgodi wa dhahabu wa North Mara.
Mrabaha huo wa dola 800,000, sawa na sh bilioni 1.2 unatokana na malimbikizo ya deni ambayo mgodi huo ulikuwa nayo kati ya mwaka 2002 na 2005. Aidha, Halmashauri ya Mji wa Tarime iliyogawanywa kutoka Halmashauri Mama ya Tarime, itapata sh milioni 100.
Hayo yalisemwa juzi na Mkurugenzi wa Halmashauri Mama ya Tarime, Athuman Akalama katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika juzi kwenye Ukumbi wa Halmashauri na kuongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Sylvester Kisyeri.
Akalama alisema: “Tumepata dola laki nane za Kimarekani sawa na shilingi 1,279,200,000, fedha hizo tumezigawa katika makundi 5 yakiwemo ya kumalizia maboma ya majengo ambayo hajayakamilika kama zahanati, madarasa, nyumba za walimu na pia tumezingatia upungufu wa madawati, vitabu vya kufundishia katika shule za msingi na Sekondari. Tutapinguza pia madeni ya wazabuni na watumishi wanaoidai Halmashauri.”
Alisema katika mgawo huo, Kata 24 katika halmashauri hiyo kila moja itapata sh milioni 30.
Baadhi ya Madiwani akiwemo wa Kata ya Pemba, Mgesi Paradiso walitaka madiwani kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuchangia kasi ya maendeleo.

WAASWA KUTOBAGUA WANAOTIBIWA KWA BIMA YA AFYA

Serikali mkoani Kagera imewataka watoa huduma wa idara ya afya kuacha tabia ya kuwabagua wagonjwa wenye kadi za bima ya afya husani wazee pindi wafikapo hospitalini na vituo vya afya kupata huduma.
Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Mstaafu Fabian Massawe katika hotuba yake aliyoitoa wakati wa uzinduzi wa mkutano wa siku ya wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mjini Bukoba,
Alisema yapo malalamiko ya wagonjwa wanachama wenye kadi za NHIF na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ya kuwa wanabaguliwa wanapokwenda kupata matibabu  kwenye hospitali na vituo vya afya vilivyotengwa kwa ajili ya kutoa huduma hiyo na kuonekana kama wagonjwa wa daraja la mwisho kwa kuwa hawana fedha taslimu.
Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa ameliomba Bunge kutunga sheria na pia katika katiba mpya iwemo sheria ya kuwa kila mwanachi ajiunge na NHIF au CHF ili kupata matibabu bora na ya gharama nafuu.
Alisema hiyo itasaidia tabia ya watu kutapatapa wanapougua kiasi cha kugeuka wasumbufu kwa ama ndugu au wenyewe kujikuta wakiuza mali zao kwa bei ya kutupa ili tu wapate fedha za kujiuguzia.

WAFUGAJI NYUKI GAIRO SASA KUNEEMEKA

Wafugaji wa mazao ya nyuki katika wilaya ya Gairo , wameanza kufaidika baada ya Wakala wa Huduma za Misitu Wilayani  Gairo, Mkoa wa Morogoro kuanzisha  shamba darasa la kisasa la ufugaji nyuki.
Mpango huo  ulianza  Machi mwaka huu , na  jumla ya mizinga 40 imetundikwa eneo la msitu wa mradi huo ambapo tayari mizinga 10 kati ya hiyo ina nyuki.
Ofisa Nyuki wa Wilaya ya Gairo, Elizabeth Njau, alisema hayo juzi  eneo la  mradi huo katika  Kijiji cha Msingisi. kilichopo wilayani humo.
Alisema, mradi huo umegharimu sh: milioni 5.6 ambapo sh: milioni 4 zikitolewa na Serikali kuu , wakati sh: milioni 1.6 ni thamani ya eneo la ardhi inayomilikiwa na Halmashauri chini ya utunzaji wa msitu wa asili uliotundikwa mizinga hiyo.
Hata hivyo alisema, shamba darasa la ufugaji nyuki limeanzishwa kwa lengo la kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wafugaji nyuki wilayani humo ili kuwawezesha kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya nyuki asali n anta.
Kwa mujibu wa Ofisa Nyuki wa wilaya hiyo, mafunzo yanatolewa yanahusu ufugaji wa nyuki, uvunaji na ufungishaji wa kisasa wa asali ili kuhifadhi misitu.
“ Hadi sasa wawakilishi 20 wawili kutoka kila kikundi kutoka vikundi 10 vilivyoundwa hapa Gairo wamepatiwa mafunzo kwa vitendo ya ufugaji nyuki kwa njia ya kisasa” alisema na kuongeza.

WAHANDISI WAELEZA CHANGAMOTO ZA UADILIFU

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Edwin Ngonyani amesema wahandisi wanakabiliwa na changamoto ya kutakiwa na waajiri wao kufanya kazi kwa matakwa yao na si kufuata taaluma ya kihandisi.
Ngonyani (pichani kushoto) alisema hayo jana jijini Dar es Salaam katika mahojiano na gazeti hili baada ya kiapo chake kama mhandisi, akiwa mmoja wa wahandisi 250 waliofanya hivyo katika Viwanja vya Karimjee baada ya utaratibu huo kuanzishwa na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli mwaka jana.
Alisema wahandisi wengi wanakuwa na nia ya kutekeleza kazi zao kulingana na taaluma zao na kiapo walichokula lakini wanapata shinikizo kutoka kwa waajiri wao jambo linalopekea majengo mengi kujengwa chini ya viwango.
Waziri Magufuli amelazimika kuanzisha kiapo cha utii kwa wahandisi wote nchini kitakachotumika kumfutia leseni ya taaluma Mhandisi mara atakaposhindwa kuwajibika ipasavyo katika kusimamia miradi husika.
Hatua hiyo inatokana na kuwapo na kashfa ya kuanguka kwa baadhi ya maghorofa, ujenzi wa barabara na vivuko usiokidhi kiwango, kwa mujibu wa Magufuli, Serikali haifurahishwi na majengo kuporomoka kwa vile inajenga sifa mbaya kwa wanataaluma hao huku jamii ikikosa imani na taaluma hiyo.

MKE WA MFALME MSWATI II KUFUNGUA MAONESHO SABASABA

Maonyesho ya 38 ya kimataifa yanayofanyika katika Viwanja vywa Mwalimu Nyerere Kilwa yaliyopo barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam maarufu kama Sabasaba yaliyoanza jana yanatarajia kufunguliwa rasmi Jumatano ijayo na Malkia wa Swaziland, Nomsa Matsedula.
Maonesho hayo ambayo kwa mwaka huu yatatembelewa na viongozi mbalimbali wa nje ya nchi,yameanza huku kukiwa na changamoto ya mabanda mengi kutomaliza maandalizi.
Akizungumza na waandishi wa habari,Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara,Uledi Mussa alisema ufunguzi rasmi utafanyika Julai 2, mwaka huu  na kufunguliwa na mmoja wa wake wa Mfalme Mswati II wa nchi hiyo aliyefungua maonesho hayo mwaka jana.
Alisema katika maonesho hayo makampuni 498 kutoka nje ya Tanzania yanashiriki, huku ya ndani yakiwa 1,700, achilia mbali mikoa 10 na mashirika mbalimbali na taasisi 10.
“Maonesho haya ya mwaka huu yanafanyika kwa kuhakikisha kila anayetembelea anapata fursa za kibiashara,mauzo pamoja na kupata mawakala wa biashara nje ya nchi,” alisema
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), Jacqueline Maleko alisema katika maonesho ya mwaka huu wameimarisha ulinzi kwa kuweka mashine za CCTV katika maeneo muhimu.
Pia eneo la kuegesha magari limeongezwa,huku kufuatia kugundulika kwa mafuta na gesi nchini makampuni makubw aya nchi wameweka vifaa vyoa ili kuonesha jinsi ya kutumia rasilimali hizo kwa maendeleo ya nchi.
Maleko alisema kuchelewa kwa maandalizi kunatokana na tabia ambayo wamezoea washiriki kwani walitakiwa kuyakamilisha kufikia Juni 25, lakini wengi walikuwa hawajakamilisha malipo hivyo kushindwa kufanya maandalizi hayo.

YASEMAVYO MAGAZETI YA LEO JUMAPILI - JUNI 29



Saturday, June 28, 2014

Mshambuliaji wa Chile, Alexis Sanchez akishangilia baada ya kuifungia timu yake bao la kusawazisha dhidi ya Brazil na kufanya matokeo kusomeka 1-1 katika mechi ya Kombe la Dunia hatua ya 16 Bora iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mineirao, huko mjini Belo Horizonte. Brazil ilisonga mbele kwa mikwaju ya penalti 3-2 ambapo upande wa Chile, Sanchez alikuwa miongoni mwa waliokosa penalti.
Mshambuliaji wa Brazil, Hulk akituliza mpira kabla ya kuifungia timu yake bao la pili dhidi ya Chile katika mechi ya Kombe la Dunia hatua ya 16 Bora iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mineirao, mjini Belo Horizonte. Hata hivyo bao hilo lilikataliwa na mwamuzi Howard Webb kwa madai mpira huo ulitua mkononi mwa Hulk kabla hajafunga na hivyo kupeleka mechi hiyo kwenye muda wa nyongeza na kisha penalti ambapo Brazil ilifanikiwa kusonga mbele kwa mikwaju 3-2.
Kiungo wa Brazil, David Luiz akipongezwa na wenzake baada ya kuifungia bao la kuongoza dhidi ya Chile katika mecho wa hatua ya 16 Bora ya Kombe la Dunia iliyochezwa usiku huu kwenye Uwanja wa Mineirao, mjini Belo Horizonte. Brazil ilishinda kwa penalti 3-2 baada ya mechi hiyo kuchezwa kwa dakika 120 na matokeo kubaki 1-1.

BRAZIL SURVIVE CHILE SHOOTOUT TO MAKE QUARTER-FINALS



Brazil came through their last-16 match in breathtaking fashion as they beat Chile 3-2 in a penalty shootout in Belo Horizonte.
The host nation earned a meeting with either Colombia or Uruguay after seeing off Chile in a pulsating clash which saw both sides have chances to clinch it.
The teams were deadlocked at 1-1 after extra time, with Alexis Sanchez having cancelled out David Luiz’s opener for Brazil - though whether Luiz should be credited with the goal is a matter of some debate, given that it appeared to be deflected goalward off the shin of Gonzalo Jara.
Brazil went ahead early on in the shootout, but Chile levelled it at 2-2 after four spot kicks - only for Neymar to bury the fifth after a stuttering run-up to make it 3-2.
And Jara once again tasted terrible luck as his final spot kick for Chile rattled against the left post to send the hosts through.
A controversial decision from English referee Howard Webb ruled out a Hulk goal in the second half for use of the arm, while Chile almost won it at the death as substitute Mauricio Pinilla saw his shot cannon back of the bar with Julio Cesar well beaten.
The lottery of the penalty shoot-out saw further drama as Julio Cesar saved from Pinilla and Sanchez, whilst Willian and Hulk both missed for Brazil.
But with the shoot-out set for sudden death, Jara’s miss means that Brazil qualify for the World Cup quarter-finals for the sixth consecutive time. 

KEY MOMENTS 
PRE-MATCH: Hulk, Fred and Neymar all start for Brazil in an extremely attacking line-up and Fernandinho comes in to replace Paulinho in the only change. The good news for Chile is that Medel and Vidal start after missing training through injury on Thursday. Thiago Silva wins his 50th cap for Brazil. 
12’ – PENALTY SHOUT BRAZIL: Hulk powers into the box and goes down under a challenge from Isla. Howard Webb is unmoved. 
18’ – GOAL BRAZIL: Silva flicks on Neymar’s corner and David Luiz looks to have bundled in his first for Brazil but replays show it came off Jara’s foot. Luiz still claims the goal anyway - that will be one to sort out later. 
25’ – CHANCE NEYMAR: He forges into the box and it’s a good chance but he drags his shot wide. 
32’ – GOAL CHILE: It’s really slack defending from Hulk who loses out to Vargas. He feeds Sanchez who finishes excellently past Cesar. 
35’ – GREAT DEFENDING SILVA: He deflects Oscar’s cross from under Neymar’s nose. 
42’ – GOOD SAVE BRAVO: He tips over Alves’ dipping drive. 
54’ – HULK GOAL RULED OUT: A really controversial decision from Howard Webb as the ball looks to have come of Hulk’s shoulder from Marcelo’s ball before he slotted home. Instead he is booked. 
65’ – GREAT SAVE CESAR: He gets down brilliantly to save from Aranguiz. 
74’ – GREAT DEFENDING MENA: He stretches to turn it away as Jo is about to slot home. 
83’ – GREAT SAVE BRAVO: Hulk dances through the defence but Bravo palms away his shot destines for the corner. 
103’ – GOOD SAVE BRAVO: He blocks out Hulk’s fierce drive. 
107’ – CHANCE BRAZIL: A free header for Jo but he heads over from Neymar’s corner. 
120’ – PINILLA HITS THE BAR: He almost wins it for Chile but his shot cannons back off the bar. 

KEY STATS 
Brazil have now qualified for the World Cup quarterfinals for the sixth consecutive time. The last time the Seleção missed out the last eight was in 1990, when they lost 1-0 against Argentina. 
In each of the four World Cups in which Chile reached the knockout stages (1962, 1998, 2010, 2014), they have been eliminated by Brazil.
Chile never had a World Cup match which went into extra time previously. 
Brazil have had six previous matches that went into extra time. They only lost/eliminated in one of these six matches, when they lost the penalty shoot-out against France in 1986.
The three World Cup PSO for Brazil previously: lost against France in 1986 (4-3, miss by Sócrates and Julio Cesar), won 1994 final against Italy and 1998 semifinal against Netherlands. 
PSO in World Cup by home nations previously: 1986 Mexico lost against West Germany, 1990, Italy lost against Argentina, 1998 France won against Italy, 2002, Korea won against Spain and 2006, Germany won against Argentina (making it 3 of 5 wins by home nation, now four of six wins after today's match).
David Luiz played his 40th international match and scored his first goal for Brazil. 
Brazil have now scored 25 World Cup goals in the round of last 16, most of all countries in World Cup history. Germany are next with 23 goals. 
This was Brazil's first goal from a set piece other than a penalty this World Cup.
For the first time since 1998, Brazil conceded a goal in the round of last 16. On 27 June 1998, Chile forward Marcelo Salas was the last player to score against the Seleção in the last 16. 
Alexis Sánchez became the first player from Chile to score at least twice in a single World Cup since Marcelo Salas scored four in 1998. 

TALKING POINT 
Did Brazil have a penalty? Howard Webb can thank his luck stars Brazil are through as he denied Hulk a goal for the use of his arm. Replays show he may have been right. Just. 

MAN OF THE MATCH: Alexis Sanchez (Chile). At the heart of Chile’s most creative moments and scored a great equaliser. A shame that his missed spot kick may have cost his side dear. 

PLAYER RATINGS  
Brazil: Julio Cesar 7, Dani Alves 6, Thiago Silva 7, David Luiz 6, Fernandinho 6, Marcelo 7, Hulk 7, Fred 5, Neymar 7, Oscar 6, Luiz Gustavo 6. SUBS: Ramires 6, Willian 6, Jo 6.  
Chile: Bravo 7, Mena 7, Isla 6, Silva 6, Sanchez 8, Vidal 7, Vargas 6, Medel 7, Jara 7, Aranguiz 6, Dias. SUBS: Pinilla 7, Rojas 6, Gutierrez 6.