Sunday, July 13, 2014

MSICHANA ACHINJWA KAMA KUKU MANYONI


Watu wasiojulikana wilayani Manyoni wamemchinja mithili ya kuku binti mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 16.
Diwani wa Kata ya Manyoni Mjini, Hamis Masabuni alisema tukio hilo lilitokea juzi asubuhi katika eneo la Mitoo kwenye mashamba ya Magereza, Uwanja wa Ndege wa zamani.
Alisema siku ya tukio, yeye alipata taarifa ya simu kutoka kwa raia wema hivyo ikambidi aende  huko kushuhudia kulikoni na mara alipofika eneo hilo alikuta  mwili wa marehemu ukiwa umelala chini na kuchinjwa mithili ya kuku.
Diwani huyo amelitaka  jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo ili kubaini wauaji wa binti huyo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.
Muuguzi wa zamu katika hospitali ya wilaya ya Manyoni, Getruda Njughuda  amekiri kuupokea mwili wa binti huyo.
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela alisema  kuwa polisi inaendelea  na uchunguzi kuhusu tukio hilo.

No comments: