Idara ya
Ardhi, Maliasili na
Mazingira katika Halmashauri ya Wilaya
ya Mpanda imekusanya zaidi Sh milioni
260 katika kipindi cha mwaka mmoja
kilichoanzia Julai mwaka jana
hadi Juni mwaka huu.
Hayo yalielezwa juzi na Kaimu Ofisa Ardhi, Maliasili na Mazingira wa halmashauri hiyo, Josephina Rupia wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za idara hiyo kwa kipindi cha mwaka 2013 na 2014 katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichoketi mjini hapa. Alisema idara hiyo ilikusanya kiasi cha Sh 265,290,050 kama mapato ya ndani. Alisema Sh 260,780, 000 zilitokana na ushuru wa leseni za mbao na Sh 210,750 ilikuwa ni makusanyo ya ushuru wa magobole.
Alisema Sh 296,500 ni ushuru wa asali na kuingia porini, Sh 914,000 zilikuwa ni ada ya fomu za viwanja na Sh 3,868,800 zilitokana na ushuru wa uwindaji wa kienyeji.
Alisema katika kipindi hicho cha mwaka mmoja idara hiyo imeweza kufanya doria mbili kubwa na kufanikiwa kukamata mbao na magogo yaliyovunwa bila kibali pamoja na magunia 369 ya mkaa na wanashikilia baiskeli tisa ambazo wavunaji haramu wa maliasili walikimbia na kuzitelekeza.
Pia idara hiyo ilikamata ng’ombe 280 ambao walikuwa wameingizwa katika msitu wa Hifadhi wa Nkaba kinyume cha sheria ambapo wamiliki watatu wa mifugo hiyo wamekamatwa na kufikishwa mahakamani.
Rupia alilieleza baraza hilo lililokuwa likiongozwa na Mwenyekiti wake, Yassin Kibiriti kwamba idara hiyo ilifanya operesheni ya kuondoa makazi holela na watu 361 wameondolewa kwa nguvu na kati yao 15 wamefikishwa mahakamani.
Hayo yalielezwa juzi na Kaimu Ofisa Ardhi, Maliasili na Mazingira wa halmashauri hiyo, Josephina Rupia wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za idara hiyo kwa kipindi cha mwaka 2013 na 2014 katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichoketi mjini hapa. Alisema idara hiyo ilikusanya kiasi cha Sh 265,290,050 kama mapato ya ndani. Alisema Sh 260,780, 000 zilitokana na ushuru wa leseni za mbao na Sh 210,750 ilikuwa ni makusanyo ya ushuru wa magobole.
Alisema Sh 296,500 ni ushuru wa asali na kuingia porini, Sh 914,000 zilikuwa ni ada ya fomu za viwanja na Sh 3,868,800 zilitokana na ushuru wa uwindaji wa kienyeji.
Alisema katika kipindi hicho cha mwaka mmoja idara hiyo imeweza kufanya doria mbili kubwa na kufanikiwa kukamata mbao na magogo yaliyovunwa bila kibali pamoja na magunia 369 ya mkaa na wanashikilia baiskeli tisa ambazo wavunaji haramu wa maliasili walikimbia na kuzitelekeza.
Pia idara hiyo ilikamata ng’ombe 280 ambao walikuwa wameingizwa katika msitu wa Hifadhi wa Nkaba kinyume cha sheria ambapo wamiliki watatu wa mifugo hiyo wamekamatwa na kufikishwa mahakamani.
Rupia alilieleza baraza hilo lililokuwa likiongozwa na Mwenyekiti wake, Yassin Kibiriti kwamba idara hiyo ilifanya operesheni ya kuondoa makazi holela na watu 361 wameondolewa kwa nguvu na kati yao 15 wamefikishwa mahakamani.

No comments:
Post a Comment