Saturday, June 21, 2014

WAJAWAZITO 1,031 WAKUTWA NA VIRUSI VYA UKIMWI


Wajawazito 1,031 wamegundulika kuwa na virusi vya Ukimwi kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Desemba mwaka jana.
Hayo yalisemwa juzi na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk  Ezekiel Mpuya wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kutokomeza virusi ya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Dk Mpuya alisema katika kipindi cha Januari hadi Desemba mwaka jana,  Mkoa uliwapima wajawazito 66,555, ambapo kati yao 1,031 waligundulika na virusi vya Ukimwi ikiwa ni sawa na asilimia 1.5.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Neema Rusibamaila alisema Ukimwi unasababisha asilimia sita ya vifo vya watoto walio chini ya miaka mitano.
Hata hivyo Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Tunajali, Dk Joseph Mweshemi alisema lengo la mradi huo ni kutokomeza maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Alisema mradi huo ulioanza mwaka 2007 umefanikiwa kutekeleza mambo mengi ikiwemo kupunguza maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Watoto wengi walioathirika na VVU ni wale waliopatikana kutokana na mimba zisizotarajiwa.

No comments: