Treni ya abiria ya bara inatarajiwa kuanza tena huduma zake
wiki ijayo baada ya kukamilika ukarabati wa daraja eneo la Bonde la Mto Ruvu,
mkoani Pwani.
Taarifa iliyotolewa na uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) jana, imesema
safari zitaanza Jumanne, ijayo saa 11 jioni kutoka Stesheni ya Dar es Salaam.
Kwa
mujibu wa taarifa hiyo ya Ofisi ya Uhusiano ya TRL kwa niaba ya Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji , Elias Mshana, muda
wa kuondoka treni kwa siku za Jumanne na Ijumaa kutoka Stesheni ya Dar kwenda
Kigoma na Mwanza utakuwa saa 11 jioni.
Aidha
muda wa treni ya kutoka Kigoma na Mwanza kwenda Dar es Salaam katika siku za
Alhamisi na Jumapili ni saa 11 jioni
kutoka Kigoma na saa 12 jioni
kutoka Mwanza.
Uongozi
huo umeshukuru wateja wake kwa ushirikiano na uvumilivu waliouonesha wakati
wakisubiri kukamilika kwa kazi ukarabati wa njia ya reli baada ya safari
kutangazwa kusitishwa hivi karibuni.
Katika
hatua nyingine, huduma za usafiri wa treni ya abiria jijini Dar es Salaam
zimesitishwa kwa muda tangu jana kwa
sababu zilizotajwa kwamba ni za kiufundi.
“Uongozi
wa TRL unasikitika kuwataarifu wananchi
na wateja wake wa huduma ya treni ya Jiji kuwa hiyo imesitishwa kwa muda wa siku tatu kuanzia
kesho (jana) hadi Jumammosi (kesho). Aidha huduma hiyo itaanza
tena hapo Jumatatu kwa kufuata ratiba yake ya kawaida,” ilisema taarifa ya
uongozi.
Uamuzi
huo unatokana na sababu za kiufundi ikiwemo kufanyiwa matengenezo vichwa vyote
viwili ambavyo vimekuwa vikihudumia treni hiyo ya Jiji.
Taarifa
hiyo ya ofisi ya Uhusiano ya TRL, ilisema vichwa hivyo vinapaswa kufanyiwa
ukarabati katika Karakana Kuu ya TRL Morogoro na kwamba vitarejeshwa jijini
keshokutwa.

No comments:
Post a Comment