Thursday, February 7, 2013

MSICHANA MWENYE MIAKA TISA AJIFUNGUA KITOTO CHA KIKE...


Kichanga hicho kikiwa chini ya uangalizi maalumu.

Msichana wa miaka tisa amejifungua mtoto wake mwenyewe, mamlaka za nchini Mexico zimebainisha jana.
Kichanga hicho cha kike kilizaliwa Januari 27 katika Hospitali ya Zoquipan, mjini Zapopan, kwenye jimbo la Jalisco lililoko magharibi mwa Mexico. Alizaliwa akiwa na uzito wa kilo 2.7.
Mama wa msichana huyo, aliyefahamika kwa jina moja la Dafne, aliwaeleza maofisa wa polisi: "Msichana huyo walikuwa amezidi kidogo miaka minane ndipo alipopata ujauzito. Baba wa kichanga hicho ni mvulana ambaye ana miaka 17, lakini hatujamuona, tangu alipotoweka kusikojulikana."
Jorge Villasenor kutoka ofisi ya waendesha mashitaka wa serikali, alisema: "Tunamsaka kijana huyo kupata taarifa zake sababu msichana hafahamu chochote kilichotokea.
"Hii ni kesi ya ubakaji au udhalilishaji watoto kijinsia."
Wasichana wote hao wameruhusiwa kutoka hospitali mwishoni mwa wiki iliyopita, kwa sasa wanaendelea vema lakini hospitali hiyo ilisema italazimika kufanya ufuatiliaji wa karibu na wa mara kwa mara kufuatia umri mdogo wa mama huyo mpya.

MAMA WENYE UMRI MDOGO ZAIDI DUNIANI:

1. Lina Medina, kutoka Ticrapo nchini Peru, alijifungua mtoto wa kiume aliyemwita Gerardo kwa upasuaji akiwa na miaka mitano na miezi saba Mei, 1939. Wazazi wake walidhani alikuwa na uvimbe lakini alipopelekwa hospitali, akagundulika kuwa na ujauzito wa miezi saba.

2. Yelizaveta "Liza" Gryshchenko, ndio alikuwa ametimiza tu miaka sita wakati akijifungua mtoto njiti wa kike nchini Urusi Agosti, 1934. Baba wa kichanga hicho alikuwa ni baba mzazi wa Liza aliyekuwa na miaka 69. Familia hiyo ihama baada ya kashfa hiyo.

3. Msichana wa miaka sita, aliyefahamika kama 'H' alijifungua kichanga cha kike kwa upasuaji Juni, 1972 mjini Delhi, India. Mwanzoni alilazwa hospitali kwa kile kilichodhaniwa kuwa ni uvimbe usio wa kawaida.

4. Msichana wa India ambaye hakufahamika alifariki wakati akijifungua, sambamba na kichanga chake Agosti 1933. Alikuwa na miaka minane tu.

5. Griseldina Acuna kutoka Colombia, aliripotiwa kuwa alianza kupata hedhi akiwa na miaka mitatu na kujifungua kichanga cha kiume Septemba, 1936, akiwa na umri wa miaka minane na miezi miwili. Baba wa kichanga hicho anadhaniwa kuwa ni mmoja wa marafiki wa familia hiyo.

No comments: