Thursday, February 7, 2013

KIM KARDASHIAN AHATARISHA UJAUZITO WAKE



Madaktari wa Kim Kardashian wanadhani mtoto wake aliye tumboni anaweza kuwa katika hatari sababu ya mawazo yanayosababishwa na Kris Humphries kuchelewesha talaka yao … imefahamika.
Vyanzo vya habari vinavyofuatilia suala hilo kwa ukaribu vimesema … siku kadhaa zilizopita Kim alimwita daktari wake katikati ya usiku kwenda nyumbani kwake sababu alikuwa akisikia maumivu makali. Daktari huyo alimchunguza, lakini baadaye akaonya anaamini matatizo hayo kwa kiasi kikubwa yanatokana na mawazo.
Vyanzo vimesema … mawazo pekee kwa sasa katika maisha yake ni talaka. Na Jumanne masaa kadhaa kabla ya kukutana na mwanasheria wake, disso-queen Laura Wasser, maumivu ya Kim yalirejea tena kwa kishindo.
Madaktari wamemuonya Kim anahitaji kukabiliana na mawazo au vinginevyo kunaweza kuwa na 'athari za muda mrefu.' Daktari huyo hakufafanua, lakini imeelezwa mhemuko wa Kim kwa mtoto wake huyo mpya unaweza kumuweka hatarini.
Mama wa Kim, Kris Jenner akiwa katika kipindi cha "The View" jana, alisema, "Kim amekuwa akishughulikia suala lake hili la talaka kwa miezi. Amekuwa katika shinikizo kubwa sababu ya jambo hili na madaktari walimweleza amekuwa na wiki ngumu mno na mawazo yanaweza kuja kuwa tatizo endapo hatokuwa makini.

No comments: