TEJA MILIONEA LILILOVUNJIKA PUA LAHUKUMIWA KIFUNGO JELA...

KUSHOTO: James Brown. KULIA: Nyumbani kwake ambamo polisi pia walikuta kiasi kikubwa cha cocaine.
Milionea aliyetawaliwa na cocaine ambaye amestaafu nje ya nchi akiwa na miaka 36 tu baada ya kuchuma fedha nyingi amefungwa baada ya polisi kukuta furushi la dawa za kulevya likiwa limefichwa kwenye gari lake la kifahari.
Tabia ya James Brown ilikuwa mbaya kiasi kufikia pua yake kuharibika baada ya miaka tisa ya matumizi ya dawa za kulevya kila siku.
Mtu huyo ambaye sasa ana miaka 45 amehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela baada ya furushi la cocaine kukutwa limefichwa kwenye sehemu za kupitishia hewa na katika paa la kujikunja la gari lake la kifahari aina ya Bentley.
Brown alikamatwa na polisi akiwa ndani ya gari lake hilo aina ya Bentley Continental Convertible huku akiwa anaishi kwenye hoteli ya kifahari ambayo iliwahi kumilikiwa na nyota wa 'Men Behaving Badly', Neil Morrissey.
Hotelini alikutwa na cocaine zaidi na bunduki anazomiliki kinyume cha sheria .
Mwendesha mashitaka Craig Jones alisema: "Brown, kupitia shughuli zake za mali, alikuwa tajiri sana na akiwa na miaka 36 akastaafu nchini Ureno ambako alikuwa akijishughulisha na cocaine."
Mahakama ya Swansea ilielezwa jinsi Brown alivyotumia 'fedha zake halali' kuwezesha matumizi yake ya cocaine.
Lakini alivuta mno puani kiasi kikubwa cha cocaine katika utaratibu wa kila siku na kumsababishia maradhi ya wazimu, matatizo ya moyo na uharibifu mkubwa wa pua yake kutokana na dawa hizo kumtafuna kabisa tishu katika matundu yake ya pua.
Alisema Brown alikuwa na wazimu kuhusu usalama wake na kukamatwa na furushi la silaha zilizokatazwa kisheria.
John Hipkin akimtetea Brown, alisema: "Alikuwa akitumia kiasi cha kutisha cha cocaine kilichowezeshwa kwa njia halali.
"Alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya, baadhi ya vipodozi na baadhi, kama haya matatizo ya moyo, yanatishia.
"Hawezi kurejea tena kwenye aina ile ya maisha."
Polisi walikamata gar lake aina ya Bentley lenye thamani ya Pauni za Uingereza 120,000 na kukuta cocaine zimefichwa ndani ya sehemu za kuingizia hewa za gari hilo na sehemu za kukunjukia paa.

No comments: