Monday, May 21, 2012

BOBBI KRISTINA AMWAGA MACHOZI TUZO ZA BILLBOARD...



Binti wa Whitney Houston, Bobbi Kristina, hakutoa hotuba ndefu kwenye Sherehe za Tuzo za Muziki za Billboard  zilizofanyika usiku wa kuamkia leo mjini Las Vegas lakini akajielezea yeye mwenyewe kuwa "amebarikiwa kuishi katika maisha ya  mwanamke kama Whitney."
Bobbi Kristina alionekana kwa mara ya kwanza kwenye tukio kubwa tangu kifo cha mama yake wakati wa kupokea Tuzo ya Milenia baada ya  shoo za John Legend na Jordan Sparks.
Wakati John Sparks akimbo limbo wake we 'I Will Always Love You', kamera zilimgeukia Bobbi amble alikuwa akibubujikwa na machozi.
Bobbi Kristina alijumuika jukwaani na meneja wake, ambaye pia ni wifi wa Whitney, Pat Houston, ambaye alitoa utangulizi mfupi kabla ya kukabidhi kipaza sauti kwa Bobbi Kristina.

No comments: