Friday, March 30, 2012

KAZI KAPATA, USALAMA WAKE JE...?

Mama huyu anayefanya kazi ya kufagia barabara akijiandaa kuvuka Barabara ya Kawawa leo asubuhi maeneo ya Ilala Bomba jirani na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Ni kweli kazi amepata, lakini usalama wake uko mashakani kutokana na kukosa vifaa muhimu vya kazi. Hana buti, vifaa vya kujikinga na vumbi na hata vikombe maalumu vya alama ya barabarani kumkinga na magari wakati akitekeleza majukumu yake. Wahusika mpooo...? (Picha na ziro99blog).

No comments: