WALIOKUFA AJALI BASI NA TRENI MOROGORO WAFIKIA WATANO


Idadi ya watu waliokufa katika ajali iliyohusisha basi na treni katika eneo la Kibaoni, Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro imeongezeka na kufikia watano baada ya dereva wa basi kufariki wakati akipatiwa matibabu.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mussa Marambo amesema tukio hilo limetokea baada ya basi lenye namba za usajili T837 CTM lililokuwa likienda Morogoro kukatiza reli na kugonga treni.
Watu 25 wamejeruhiwa katika ajali hiyo baada ya  gari walilokuwa wakisafiria kugonga treni yenye nambari za usajili 88U3 ililokuwa linatokea mkoani Dodoma kuelekea Morogoro.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Dennis Ngaromba ameelezea hali za wagonjwa kuwa zinatofautiana ila bado wanaendelea na matibabu lakini pia ameeleza kuwa wanakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo matatizo ya umeme hali iliyofanya baadhi ya wagonjwa kuhamishwa hospitalini hapo.

No comments: