Dereva wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Juma Moshiamenusurika kufa maji baada ya gari alilokuwa akiliendesha kusombwa na mafuriko ya maji katika mto Malera, nje kidogo ya mji wa Karatu na yeye mwenyewe kupanda juu ya mti.
Juma alilazimika kutoka kwenye gari hilo aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili SU 36037 lililokuwa limesombwa na maji kwaumbali wa mita zipatazo 70 hivi kutoka barabarani, mapema alfajirijana, na alifanikiwa kujiokoa baada ya kupanda juu ya mti.
Alikumbwa na mkasa huo wakati akienda mjini Arusha kikazi.
Mkuu wa Idara ya Huduma ya Uhandisi wa NCAA, Isra Missana, pamoja na wafanyakazi wengine wa mamlaka hiyo wakishirikiana na wakazi jirani wa eneo hilo, walifanikiwa kumwokoa dereva huyo majira ya saa 12:30 asubuhi.
Katika hatua nyingine, mamia ya wasafiri waliokuwa wakitoka maeneo yaKaratu, na watalii waliokuwa wakitoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kwenda mjini Arusha, Dar es Salaam na maeneo mengine nchini jana walikwama kwa muda kuvuka Mto Kirurumo uliokuwa umefurika maji hadi kupita juu ya barabara hukuukiporomosha mawe makubwa kutoka milima Mbulumbulu.
Mto huo upo mpakani mwa Wilaya ya Monduli na Karatu.
Miongoni mwa abiria walioshindwa kusafiri jana ni wale waliokuwawasafiri kwa basi la Dar Express ambalo mapema asubuhi lilionekanalikirudi tena mjini Karatu baada ya kushindwa kuvuka katika mto huouliokuwa ukiporomosha mawe makubwa.
Abiria wengine waliotakiwa kusafiri kwa basi la Sai Baba halikuwezakuanza safari yake ya kwenda Dar es Salaam.
Mamia ya magari yaliyokuwa yakiwasafirisha watalii kutoka hifadhi zataifa yalikuwa miongoni mwa magari mengine mengi yaliyokwama katika eneo hilo.
Mto Kirurumo unamwaga maji yake katika Ziwa Manyara lililopo katika Hifadhi ya Taifa ya Manyara.
Mafuriko hayo yalitokana na mvua kubwa iliyonyesha maeneo ya Milima ya Mbulumbulu usiku wa kuamkia jana asubuhi.
Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Felix Ntibenda, akizungumza katika eneo latukio hilo alisema tatizo la mafuriko katika mto huo limekuwalikijirudia mara kwa mara.
Alisema serikali inafanya utafiti wa kutafuta ufumbuzi wa kudumu watatizo la mafuriko yanayoporomosha mawe na kuharibu barabara hiyo.
Juma alilazimika kutoka kwenye gari hilo aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili SU 36037 lililokuwa limesombwa na maji kwaumbali wa mita zipatazo 70 hivi kutoka barabarani, mapema alfajirijana, na alifanikiwa kujiokoa baada ya kupanda juu ya mti.
Alikumbwa na mkasa huo wakati akienda mjini Arusha kikazi.
Mkuu wa Idara ya Huduma ya Uhandisi wa NCAA, Isra Missana, pamoja na wafanyakazi wengine wa mamlaka hiyo wakishirikiana na wakazi jirani wa eneo hilo, walifanikiwa kumwokoa dereva huyo majira ya saa 12:30 asubuhi.
Katika hatua nyingine, mamia ya wasafiri waliokuwa wakitoka maeneo yaKaratu, na watalii waliokuwa wakitoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kwenda mjini Arusha, Dar es Salaam na maeneo mengine nchini jana walikwama kwa muda kuvuka Mto Kirurumo uliokuwa umefurika maji hadi kupita juu ya barabara hukuukiporomosha mawe makubwa kutoka milima Mbulumbulu.
Mto huo upo mpakani mwa Wilaya ya Monduli na Karatu.
Miongoni mwa abiria walioshindwa kusafiri jana ni wale waliokuwawasafiri kwa basi la Dar Express ambalo mapema asubuhi lilionekanalikirudi tena mjini Karatu baada ya kushindwa kuvuka katika mto huouliokuwa ukiporomosha mawe makubwa.
Abiria wengine waliotakiwa kusafiri kwa basi la Sai Baba halikuwezakuanza safari yake ya kwenda Dar es Salaam.
Mamia ya magari yaliyokuwa yakiwasafirisha watalii kutoka hifadhi zataifa yalikuwa miongoni mwa magari mengine mengi yaliyokwama katika eneo hilo.
Mto Kirurumo unamwaga maji yake katika Ziwa Manyara lililopo katika Hifadhi ya Taifa ya Manyara.
Mafuriko hayo yalitokana na mvua kubwa iliyonyesha maeneo ya Milima ya Mbulumbulu usiku wa kuamkia jana asubuhi.
Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Felix Ntibenda, akizungumza katika eneo latukio hilo alisema tatizo la mafuriko katika mto huo limekuwalikijirudia mara kwa mara.
Alisema serikali inafanya utafiti wa kutafuta ufumbuzi wa kudumu watatizo la mafuriko yanayoporomosha mawe na kuharibu barabara hiyo.

No comments:
Post a Comment