Thursday, February 7, 2013

MLEZI WA WATOTO WA MICHAEL JACKSON ALIA NJAA...



TJ Jackson hatoweza tena kuhudumia kama mzazi mbadala wa watoto watatu wa Michael Jackson bila kupata fidia kiasi fulani, hivyo Wasimamizi wa mali za Michael Jackson wanamtaka Jaji kumpatia TJ kiasi fulani cha pesa kuwezesha 'jahazi hilo' kuendelea na safari.
Wasimamizi hao wamefungua madai hayo -- ambayo yanasema TJ amekuwa akijitolea mno kwa Paris, Prince na Blanket tangu kifo cha Michael Jackson. TJ -- ambaye sasa ni mlezi wa watoto hao akishirikiana na Katherine Jackson -- anatumia masaa 40 kwa wiki akiwatunza watoto hao watatu.
Wasimamizi hao wanasema imekuwa vigumu mno kwa TJ -- ambaye ameoa na kufanikiwa kupata watoto wake watatu. Ingawa amekuwa mlezi mshirika tangu Julai, hajawahi kulipwa hata senti moja kutokana na huduma yake hiyo.
Wasimamizi hao wanamtaka jaji kuwaruhusu wamlipe TJ Dola za Marekani 9,000 kwa mwezi (zaidi ya Shilingi milioni 14.6 za Tanzania), kuanzia Julai mwaka jana. Waliongeza, kwa namna mwelekeo ulivyo sasa, TJ hatoweza kuendelea, hivyo fidia ni muhimu sana.

No comments: