![]() |
| Askofi Mkuu Alex Malasusa. |
Mkuu
wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Mkuu Alex Malasusa
anatarajia kukutana na wachungaji na wainjilisti wa Jimbo la Arusha Magharibi
Dayosisi ya Kaskazini Kati leo makao makuu ya Jimbo hilo Ngaramtoni nje kidogo
ya Jiji la Arusha.
Askofu
Malasusa yuko hapa kwa zaidi ya wiki moja sasa na amekuwa akikutana na viongozi
wa Kanisa hilo kwa lengo la kujua kiini cha mgogoro wa Dayosisi hiyo uliodumu
kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa na kufikia hatua ya kuunda Kamati ya Maaskofu
sita kuchunguza kiini cha mgogoro huo na kupata mapendekezo ya Kamati hiyo ili
kufia hatua ya kutoa uamuzi.
Kwa
mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Dayosisi hiyo zilisema kuwa kikao hicho kinatarajia
kufanyika leo kuanzia saa 4 asubuhi makao makuu ya Jimbo hilo na tayari taarifa
za kuwepo kwa kikao hicho zimesambazwa kwa wachungaji wote 13 wa Jimbo hilo.
Habari
zilisema kufanyika kwa kikao hicho ni kutaka Askofu Malasusa apate maoni ya
wachungaji na wainjilisti wa Jimbo hilo juu ya mgogoro huo.
Usharika
wa Ngateu uliopo Jimbo la Arusha Magharibi ndiko chimbuko kubwa la kuibuka kwa
mgogoro huo kwani Mchungaji Philemoni Mollel alikuwa Mchungaji Kiongozi wa
Usharika huo na kufikia hatua ya kufukuzwa kazi na kuzuiwa kufanya kazi za
kichungaji ndani ya Kanisa hilo hatua iliyopingwa na washarika wa Usharika huo
na kufikia hatua ya kutaka kuandamana hadi makao makuu ya Dayosisi hiyo.
Vyanzo
vilisema kuwa taarifa ya kufanyika kwa kikao hicho ilikuwa ikisambazwa jana na
juzi na Katibu wa Jimbo aliyetambulika kwa jina moja la Meidamei kwa njia ya
ujumbe wa simu za mikononi za wachungaji wa jimbo hilo.
Ujumbe
ulisomeka: ‘’Wapendwa wachungaji Shalom! Poleni na kazi. Nawaandikia kuwahimiza
wachungaji wote tarehe 6/02/2013 saa 4 asubuhi wote tuwe tumefika jimboni kila
mchungaji aje na wainjilisti kama mwaliko uliotangulia wa Katibu wa Jimbo
ulivyoelekeza. Kikao hiki ni muhimu sana kwa ajili ya kukutana na ujumbe wa
Kanisa (Mkuu wa jimbo),’’ ilimaliza sehemu ya ujumbe huo.
Habari
zilisema kabla ya ujio wa Askofu Mkuu wa Kanisa leo katika Jimbo hilo,
Jimbo lilipanga semina kwa wachungaji na wainjilisti hivyo semina hiyo ilifutwa
kutokana na ugeni huo.
Ujumbe
huo kwa wachungaji ni kutoka kwa Katibu wa Jimbo ulisomeka ifuatavyo:
‘’Wapendwa naomba niwajulishe kilichosababisha kuahirisha semina ya tarehe
6/02/2013 Jumatano saa 3 asubuhi, wachungaji na wainjilisti wote wanahitajika
kuonana na ugeni wa Kanisa wa Dayosisi hiyo, hivyo ugeni huu ni wa watu 155 tunaomba
kwa kusaidia mapokezi kila usharika utupe Sh 80,000 (kasima ya mapato mengine)
walio mbali mtume kwa M-pesa na mtakuta risiti zenu. Ahsanteni sana,’’ ilisema
sehemu ya ujumbe huo.
Jimbo
la Arusha Magharibi lina sharika 13 kutokana na ujumbe huo wa Katibu wa Jimbo
wa kutaka kila usharika kuchangia kiasi hicho ni Sh 1,040,000 zitakusanywa
iwapo kila usharika utatimiza.
Wakati
huo huo, jana katika shauri lililofunguliwa na Mchungaji Philemon Mollel
kupinga kufukuzwa kazi bila ya kufuata taratibu katika Tume ya Usuluhisho ya
Idara ya Kazi jijini Arusha dhidi ya Baraza la Wadhamini la Dayosisi ya
Kaskazini Kati, uongozi wa Dayosisi hiyo ukiongozwa na wakili wao Israel
Mwaluko uliweka pingamizi katika shauri hilo kwa mdomo hatua iliyopingwa na
Msuluhishi.
Kutokana na hali hiyo, Msuluhishi wa Tume hiyo
alimtaka Wakili Mwaluko kuwasilisha pingamizi hilo kwa maandishi kabla ya
Februari 11 na Mchungaji Mollel anapaswa kujibu pingamizi hilo kabla ya
Februari 18 na Februari 21 ni mwisho wa kuzipitia pingamizi hizo.
No comments:
Post a Comment