Wednesday, January 30, 2013

KAKA AKIRI HADHARANI KUHUSIKA NA KIFO CHA WHITNEY HOUSTON...

Michael Houston.
Kaka wa Whitney Houston amesema yeye ndiye wa kulaumiwa kwa kumuingiza mwimbaji huyo kwenye matumizi ya dawa za kulevya kama cocaine katika miaka ya 1980 … na sio Bobby Brown … na juzi  usiku alikuja akiwa nadhifu mbele ya Oprah.
Michael Houston aliketi chini akiwa na mama yake, Cissy na kuweka bayana uthubutu wake katika "Oprah's Next Chapter" … akikiri kwamba alikuwa mtu wa kwanza kutumia dawa za kulevya na Whitney.
Michael anasema anajihisi mwenye hatia mno kwa kifo cha Whitney -- lakini anasema hakufahamu jinsi gani dawa za kulevya zingeweza kuwa hatari hivyo pale mwanzoni alipomletea Whitney hadi mlangoni … akafafanua: "Unaelewa kwa wakati huo … miaka ya 1980 … ilikuwa ikiruhusiwa."
Michael anaongeza: "Inauma sana … Najihisi kuwajibika kwa kuacha iendelee kwa kipindi kirefu hivi."
Whitney alifariki mjini Beverly Hills Februari mwaka jana baada ya kutumia mseto wa dawa za kulevya uliojumuisha cocaine, Xanax na bangi.

No comments: