Wednesday, January 30, 2013

ALIYEMDHALILISHA MAMA KWENYE KICHAKA ATIWA MBARONI...

Kichaka ambapo mtuhumiwa huyo anadaiwa kutenda kosa hilo dhidi ya mama wa watoto watatu.
Raia wa Uingereza amekamatwa nchini Ufaransa kufuatia kufanya shambulio baya dhidi ya mama wa watoto watatu ambaye alikuwa akifanya mazoezi ya kukimbia.
Mtu huyo, ambaye hakutajwa jina lakini mwenye miaka 32 na mwenyeji kutoka Chatham mjini Kent, anaishi yadi 100 tu kutoka eneo la tukio la shambulio la Alhamisi iliyopita pembezoni mwa Nimes.
Polisi walianzisha msako kwenye mji mashuhuri wa kitalii baada ya ya mwili uliofunikwa kwa nguo sehemu ndogo wa Joudia Zimmat mwenye miaka 34 kukutwa kwenye kichaka. Alikuwa amedhalilishwa kijinsia, kuchomwa visu na kupigwa, polisi walisema.
Walimu wa shule wanayosoma watoto wake walitoa taarifa baada ya kushindwa kurejea kuwachukua watoto hao baada ya kumaliza masomo siku hiyo.
Kisu aina ya Stanley na mawe mawili yaliyotapakaa damu yalikutwa jirani na hapo, na vinaaminika kwamba vilitumiwa na muuaji huyo.
Ofisa mmoja wa polisi alisema: "Alikatwa na kupigwa kwa mawe magumu. Koo lake lilikatwa na uso wake ulikuwa hautambuliki. Alikuwa ameuawa kwa kukusudia."
"Mwanamke huyo alishambuliwa na kisha kuuawa kikatili," kilisema chanzo kingine cha polisi wa Nimes.
Chanzo hicho kiliongeza kwamba Joudia, ambaye alikuwa na rekodi ya uhamiaji kutoka Tunisia, alikuwa amedhalilishwa kijinsia.
Nguo zake zilikuwa zimechanwa kutoka mwilini mwake, lakini hakuwa amebakwa, msemaji wa polisi alisema.
Mtuhumiwa huyo, ambaye anaishi na mama yake, amejeruhiwa mkononi 'mikwaruzo ya mkwamba' na mwili wa muathirika huyo ulikutwa 'kwenye mikwamba iliyosongamana', chanzo hicho kiliongeza.
Nguo zake pia zinasemekana kuwa zilitapakaa damu. Mwingereza huyo alikamatwa na maofisa wa polisi kutoka mji wa kusini wa Montpellier, na anadaiwa kuwa ameacha ushahidi katika eneo la tukio la uhalifu huo, alisema mwendesha mashitaka wa Nimes Stephane Bertrand.
Hii inaaminika kuhusisha alama za DNA. Jana polisi walifanya msako nyumbani kwa mtuhumiwa, na yeye alikuwapo nyumbani hapo.
Alivikwa pingu huku akiwa kavaa koti la khaki, na kujificha uso wake kutoka kwa wapigapicha. Jirani wa mtu huyo aliyekamatwa alisema alikuwa 'mkarimu, mtu mwenye busara', ambaye  mara chache alionekana akitembea na mbwa wake kwenye eneo hilo.
Hivi karibuni alihamia Ufaransa akitokea Kent, jirani huyo aliongeza.
Muathirika huyo ni mama wa watoto wawili wa kike na mmoja wa kiume, na alikuwa akiishi na rafiki yake wa kiume.
Wakazi wa eneo hilo wamemuelezea Joudia kama 'mrembo na mwanamke rafiki', ambaye hivi karibuni alihamia kwenye nyumba yake katika eneo hilo akiwa na familia yake.
Msemaji wa polisi alisema: "Raia huyo wa Uingereza amekamatwa. Suala hilo sasa liko mikononi mwa polisi mjini Montpellier."

No comments: