Mbwiaji dawa za kulevya mmoja maarufu kama 'Teja' kaamua kumrudia Mwenyezi Mungu kwa kuanza kufunga Mwezi wa Ramadhani. Ilipofika mchana huku swaumu ikiwa imembana ile mbaya akawa anasikiliza kipindi cha kuchagua nyimbo redioni na maongezi yakawa hivi. Mtangazaji: "Enhe, mwenzangu unaitwa nani na ungependa nikupigie wimbo gani?" Teja: "Sitaki chochote ila tu nipigie Adhana ya Magharibi nifuturu zangu mie maana sijala tangu asubuhi!" Duh...

No comments:
Post a Comment