CHEKA TARATIBU...

Katika darasa wanafunzi wanaendelea na kipindi cha somo la Jiografia. Wakaanza kuulizwa maswali. MWALIMU: Mhimili wa Dunia ni nini? MWANAFUNZI: Mhimili wa Dunia ni mstari wa kufikirika ambao unapita kutoka ncha moja hadi nyingine, na ambamo dunia inazunguka. MWALIMU: Vizuri sana. Je, unaweza kuanika nguo kwenye huyo mstari MWANAFUNZI: Ndio, mwalimu. MWALIMU: Sawa. Je, ni aina gani ya nguo? MWANAFUNZI: Nguo za kufikirika, mwalimu!

No comments: