CHEKA TARATIBU...

Jamaa mmoja akiwa amelewa chakari kaingia baa na baada ya kumkodolea macho kwa muda mwanamke pekee aliyekuwa amekaa kwenye baa ile, akamfuata na kuanza kumbusu. Yule mwanamke akaruka na kumtandika vibao kadhaa. Jamaa kwa haraka akaomba radhi na kujieleza, "Samahani sana. Nilifikiri wewe ni mke wangu. Unafanana naye mno." Mwanamke akajibu kwa ukali, "Wewe ni mpuuzi tena kama huwezi pombe ni bora kuacha nazo!" Jamaa kwa sauti ya juu akasema, "Inashangaza sana! Yani hata unavyoongea kama yeye kabisaaa!" Duh...

No comments: