Thursday, August 9, 2012

MWIGIZAJI MKONGWE BOB HOSKINS ATANGAZA KUSTAAFU...


Mwigizaji mkongwe wa Uingereza, Bob Hoskins ambaye alicheza kama P.I. Eddie kwenye filamu ya "Who Framed Roger Rabbit?" na kama Smee kwenye filamu ya "Hook", ametangaza rasmi kustaafu kazi hiyo baada ya kugundulika kuwa na maradhi ya kiharusi.
Hoskins mwenye miaka 69 ametoa taarifa hiyo jana, akidai kuwa amegundulika kuwa na maradhi hayo. Pia amewashukuru mashabiki wake kwa msaada wao, akisema alikuwa na wakati mzuri sana kipindi chote cha uigizaji wake.
Bila masihara, kipindi chake cha uingizaji ameweza kucheza filamu zisizopungua 80, na mchango wake katika filamu za Uingereza kupitia "The Long Good Friday" na "Mona Lisa" ulimuwezesha kupata Tuzo za Cannes, Tuzo za Golden Globe kwa Mwigizaji Bora, Tuzo kadhaa za BAFTA na kuchaguliwa kushiriki kwenye Academy Award.
Kisha tena, Hoskins alicheza katika tukio la moja kwa moja mwaka 1993 kwenye "Super Mario Bros".

No comments: