Sunday, May 20, 2012

AKAMATWA AKISAFIRISHA MIILI YA VITOTO VICHANGA...


Raia wa Uingereza amekamatwa mjini Bangkok baada ya mimba changa sita kukutwa kwenye masanduku yake ya kusafiria.
Hok Kuen Chow mwenye miaka 28, Mwingereza aliyezaliwa Hongkong na wazazi wenye asili ya Taiwan, anashikiliwa eneo la Yaowarat mjini humo baada ya polisi kudokezwa.
Anatuhumiwa kujaribu kusafirisha kwa njia za panya mimba hizo za kati ya miezi miwili hadi saba kwenda Taiwan na kuuza kwa wateja zake matajiri kwenye mtandao.
Chow ameripotiwa kukiri kununua miili, ambayo imepigwa na kukaushwa na kisha kupakwa rangi ya dhahabu kwa bei ya Pauni za Uingereza 4,040.
Akifikisha Taiwan anaweza kuuza mara sita ya bei aliyonunulia kwa wateja zake matajiri wanaoamini mimba hizo changa zitawaletea neema zaidi. "Miili hiyo ni kati ya umri wa miezi miwili na saba," amesema Wiwat Kumchumnan wa kitengo cha polisi cha kulinda wanawake na watoto.
Chow amesema alipanga kuuza mimba changa kwa wateja ambao waliamini kuwa watakuwa wenye bahati na matajiri,
"Baadhi ilikutwa imefunikwa kwa rangi ya dhahabu."
Polisi wamesema miili hiyo ilikuwa imechorwa michoro ya dini mbalimbali na tatoo.
Haikufahamika jana miili hiyo, ambayo imehifadhiwa ndani ya masanduku sita, imetokea wapi au nani hasa aliyeikabidhi kwa Chow.
Inawezekana imepatikana kutoka kwenye mila za Thai katika zoezi la 'Kuman Thong' ambapo watoto wasiotakiwa wanatolewa kwenye miili ya mama zao kabla ikiwa ni sehemu ya sherehe hizo.
Badala ya kuzikwa, miili hiyo hupikwa hadi kukauka kabisa na kuzingirwa na  kabla haijapakwa rangi ya dhahabu.
Chow, amabye amekamatwa kwa tuhuma za kumiliki mabaki ya binadamu, alikuwa akiishi kwenye hoteli moja mjini Bankok wakati alipokamatwa.
Polisi walipenyezewa taarifa kwamba kuna mimba changa zinauzwa kwa wateja matajiri kwa njia ya matangazo ya kwenye mtandao yasiyo rasmi.
Chow atakabiliwa na kifungo cha mwaka mmoja jela na faini ya Pauni Za Uingereza 40 kama akipatikana na hatia.
Novemba mwaka 2010, wakaguzi wa afya walikuta mimba changa 2,000 kwenye jengo moja mjini Bangkok ambazo zilitolewa kinyume cha sheria.
Ofisi ya Mambo ya Nje na Jumuiya ya Madola jana ilithibisha kukamatwa kwa mtu huyo.
Msemaji alisema: "Tunathibitisha kukamatwa kwa raia wa Uingereza mjini Bangkok Mei 18.
"Tuko tayari kutoa ushirikiano wowote wa kibalozi."

No comments: