Ushindi wa mabao 4-0 ilioupata nyumbani kwa Coventry City umeirejesha moja kwa moja timu ya Southampton kwenye Ligi Kuu ya England.
Kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Nigel Adkins kilifahamu fika ushindi dhidi ya timu hiyo iliyoshuka daraja utaihakikishia Southampton nafasi ya pili nyuma ya vinara, Reading na kurejea Ligi Kuu kwa mara ya kwanza tangu iliposhuka daraja mwaka 2005, na dalili hizo zilianza kuonekana ndani ya dakika 20.
Mabao yaliyoibeba Southampton yaliwekwa kimiani na Billy Sharp dakika ya 16, Jose Fonte dakika ya 19, Jos Hooveid dakika ya 53 na Lallana katika dakika ya 63 na hivyo kuamsha shamrashamra za kuwashangilia 'Wakatatifu' hao kurejea Ligi Kuu.
Kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Nigel Adkins kilifahamu fika ushindi dhidi ya timu hiyo iliyoshuka daraja utaihakikishia Southampton nafasi ya pili nyuma ya vinara, Reading na kurejea Ligi Kuu kwa mara ya kwanza tangu iliposhuka daraja mwaka 2005, na dalili hizo zilianza kuonekana ndani ya dakika 20.
Mabao yaliyoibeba Southampton yaliwekwa kimiani na Billy Sharp dakika ya 16, Jose Fonte dakika ya 19, Jos Hooveid dakika ya 53 na Lallana katika dakika ya 63 na hivyo kuamsha shamrashamra za kuwashangilia 'Wakatatifu' hao kurejea Ligi Kuu.

No comments:
Post a Comment