Wednesday, April 25, 2012

NYOTA WA MIELEKA WCW APATA AJALI MBAYA, YU MAHUTUTI HOSPITALINI...


Nyota wa zamani wa mieleka ya WCW, Buff Bagwell yuko kwenye chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Atlanta baada ya gari lake aina ya Jeep kupinduka, ikisemekana kuvunjika mishipa kadhaa shingoni mwake.
Kwa mujibu wa hospitali hiyo, ajali hiyo ilitokea Jumatatu usiku ikimwacha nyota huyo mwenye miaka 42 akiwa amevunjika mifupa shingoni, usoni pamoja na kuvunjika taya lake.
Bagwell alisafirishwa hadi hospitali ya jirani ambako alilazwa chumba cha wagonjwa mahututi.
Taarifa zaidi zitafuatia...

No comments: