Mbwa waliokuwa wakipelekwa kuchinjwa na kusambazwa kwenye migahawa mbalimbali ya China wameokolewa baada ya lori walimobebwa kuzuiwa njiani na wanaharakati wa haki za wanyama.
Lori hilo lililokuwa limebeba mbwa wapatao 505 waliofungiwa kwenye vizimba 156, lilisimamishwa kwenye barabara kuu katika Jimbo la Yunnan likitokea Fumin kwenda Kunming kufuatia madereva wengine kushtukia mzigo huo haramu.
Idadi ya picha na maoni mbalimbali yalitumwa kwenye mtandao wa kijamii wa China unaofanana na Twitter, Weibo, wakishawishi polisi kulikamata lori hilo katika kizuizi kinachofuata.
Baada ya kukamatwa, lori hilo lilipelekwa kituo cha polisi kinachofuata ambapo wapenda wanyama waliovujisha taarifa hizo walianza kuwasili kituo hapo.
Kwa majonzi, kufuatia hali mbaya wengi wa mbwa hao walikuwa tayari wamekufa wakati walipogundulika.
Mmoja wa wanaharakati hao alisema: "Walirundikwa pamoja. Kizimba kimoja waliwekwa mbwa kati ya saba na nane. Tuliumia sana mioyo kuona tukio hili."
Wafanyakazi wa kujitolea walivunja vizimba hivyo ndani ya lori na walitumia usiku mzima kuwalisha, kuwanywesha na kuwatibu wanyama hao.
Wakielezea tukio hilo la kutisha, maofisa kutoka Idara ya Ukaguzi wa Wanyama ya eneo hilo inayochunguza tukio walifafanua kuwa usafirishaji mbwa ni ruksa.
Mtu anayewamiliki anayo leseni ya kufanya hivyo na polisi wameshindwa kufanyia kazi madai kuwa walikuwa wakipelekwa kwenye migahawa mbalimbali kwa ajili ya kuuzwa nyama.
Mwanaharakati mwingine ameongeza: "Hatuwezi kuwazuia kula mbwa, hasa kwa kuzingatia kuwa hatuna sheria za kulinda wanyama. Tunaimani Serikali itawadhibiti wanaojihusisha na mbwa kufanya biashara hiyo."
Hatahivyo, kituo binafsi cha kuokoa mbwa kimechukua hatua ya kuwakusanya mbwa wote kutoka kwa wamiliki wake kwa ghara ya Pauni za Uingereza 5,900. Wanyama hao watakaa chini ya uangalizi maalumu hadi watakapopata wamiliki wapya.
Mpaka sasa, nchi 11 duniani bado zinakula mbwa. Nchi hizo ni China, Indonesia, Korea, Mexico, Philippines, Polynesia, Taiwan, Vietnam, Arctic na Antatctic na miji miwili nchini Uswisi.
Lori hilo lililokuwa limebeba mbwa wapatao 505 waliofungiwa kwenye vizimba 156, lilisimamishwa kwenye barabara kuu katika Jimbo la Yunnan likitokea Fumin kwenda Kunming kufuatia madereva wengine kushtukia mzigo huo haramu.
Idadi ya picha na maoni mbalimbali yalitumwa kwenye mtandao wa kijamii wa China unaofanana na Twitter, Weibo, wakishawishi polisi kulikamata lori hilo katika kizuizi kinachofuata.
Baada ya kukamatwa, lori hilo lilipelekwa kituo cha polisi kinachofuata ambapo wapenda wanyama waliovujisha taarifa hizo walianza kuwasili kituo hapo.
Kwa majonzi, kufuatia hali mbaya wengi wa mbwa hao walikuwa tayari wamekufa wakati walipogundulika.
Mmoja wa wanaharakati hao alisema: "Walirundikwa pamoja. Kizimba kimoja waliwekwa mbwa kati ya saba na nane. Tuliumia sana mioyo kuona tukio hili."
Wafanyakazi wa kujitolea walivunja vizimba hivyo ndani ya lori na walitumia usiku mzima kuwalisha, kuwanywesha na kuwatibu wanyama hao.
Wakielezea tukio hilo la kutisha, maofisa kutoka Idara ya Ukaguzi wa Wanyama ya eneo hilo inayochunguza tukio walifafanua kuwa usafirishaji mbwa ni ruksa.
Mtu anayewamiliki anayo leseni ya kufanya hivyo na polisi wameshindwa kufanyia kazi madai kuwa walikuwa wakipelekwa kwenye migahawa mbalimbali kwa ajili ya kuuzwa nyama.
Mwanaharakati mwingine ameongeza: "Hatuwezi kuwazuia kula mbwa, hasa kwa kuzingatia kuwa hatuna sheria za kulinda wanyama. Tunaimani Serikali itawadhibiti wanaojihusisha na mbwa kufanya biashara hiyo."
Hatahivyo, kituo binafsi cha kuokoa mbwa kimechukua hatua ya kuwakusanya mbwa wote kutoka kwa wamiliki wake kwa ghara ya Pauni za Uingereza 5,900. Wanyama hao watakaa chini ya uangalizi maalumu hadi watakapopata wamiliki wapya.
Mpaka sasa, nchi 11 duniani bado zinakula mbwa. Nchi hizo ni China, Indonesia, Korea, Mexico, Philippines, Polynesia, Taiwan, Vietnam, Arctic na Antatctic na miji miwili nchini Uswisi.

No comments:
Post a Comment