Monday, April 30, 2012

CHEKA TARATIBU...

Nikiwa kwenye msiba nyumbani kwa binti mmoja jirani yetu maeneo ya Magomeni ambaye amefiwa na mwanae, mara ikasikika sauti ya mwanamke mmoja akilia kwa sauti na kutamka maneno mbalimbali. Nikashawishika kusogea kwa dirishani nione ni nani aliyekuwa akitamka maneno mazito hivyo. Aah, kumbe ni huyo binti mfiwa ambaye mtoto aliyefariki alisemekana kuzaa na Mchina. Katika kusema hili na lile ndipo binti huyo akatamka kwa uchungu, "Mie nilijua tu, siku zote nasema vitu vya Kichina havidumu...mmeona sasa?" Watu wote msibani midomo mwaaaa...

No comments: