Ama kweli, ushamba mzigo! Mmasai mmoja kaamka asubuhi na kwenda moja kwa moja zahanati ya jirani kupima akitaka kujua anasumbuliwa na nini. Alipofika kwa daktari, akawekewa chombo cha kupimia joto la mwili mdomoni kujua kama ana homa au la. Baada ya dakika kama ishirini hivi, daktari akamfuata kutaka kuchukua kile chombo ili aangalie joto limefikia kiasi gani. Kwa mshangao Mmasai akafungua mdomo lakini hakukua na kitu zaidi ya meno na ulimi wake tu. Ndipo daktari akauliza, "Kiko wapi kile chombo nilichokuwekea mdomoni?" Mmasai kwa kujiamini akajibu, "Imemesa yote! Mimi nasani ile kidonge mupya." Dah...

No comments:
Post a Comment