Wednesday, February 29, 2012
CHEKA TARATIBU...
Kulikuwa wa jamaa mmoja kwenye wodi ya vichaa Mirembe, Dodoma. Kila siku jamaa huyo alikuwa akitega sikio lake ukutani mithili ya mtu amayesikiliza kitu. Dokta aliyekuwa akiwahudumia alikuwa akiona tabia hii kila siku. Akaanza kufuatilia kwa karibu kila mara na kumkuta hivyo. Siku moja Dokta akaamua kuingia ndani na kwenda moja kwa moja kwenye ule ukuta na kutega sikio lake huku yule jamaa akimtazama kwa makini. Dokta akamgeukia yule jamaa na kusema, "Mbona sisikii chochote?" Ndipo yule jamaa akamjibu, "Kwa muda mrefu sasa hali iko hivyo hivyo." Duh!
This is a blog that brings you hot news that aims to educate the community about various things including sports, culture, art, entertainment and social. This blog does not involve political issues at all. We ask for your cooperation and to contribute opinions on the various information we bring to you.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment