Wednesday, December 31, 2014
Tuesday, December 30, 2014
Monday, December 29, 2014
MVUA KUBWA DAR MAJANGA, MTOTO ASOMBWA AKIWA AMELALA
![]() |
Hivi ndivyo hali ilivyokuwa jijini Dar es Salaam baada ya mvua kubwa kunyesha kwa takribani saa mbili mfululizo. |
![]() |
Mvua iliyonyesha jijini Dar es Salaam,
imeleta balaa baada ya kuua watu wawili, katika maeneo tofauti ya jiji,
likiwemo tukio la mtoto wa miaka minane kufa baada ya kuzidiwa na maji
yaliyoingia ndani ya nyumba aliyokuwa amelala.
DEREVA WA BODABODA AUAWA NA KUTUNDIKWA KWENYE MTI
Mwendesha
pikipiki (bodaboda), mkazi wa Kitongoji cha Buriba katika mji mdogo wa
Sirari wilayani Tarime mkoani Mara, Mrimi Nyabikwi (23), amekutwa amekufa na
mwili wake kukutwa umening'inizwa kwenye mti maeneo ya Makaburini.
Kamanda wa Polisi
Tarime/Rorya, Lazaro Mambosasa amethibitisha kifo hicho. Alisema habari kutoka
ndani ya familia ya mtu huyo zilidai
kuwa Mrimi alitoweka nyumbani kwake kuanzia Desemba 24, mwaka huu.
Alisema marehemu
alikuwa amekodisha pikipiki ya mkazi wa Sirari kwa kufanyia kazi ya kusomba
abiria, lakini hakurejea nyumbani hadi mwili wake ulipokutwa na wachungaji wa
mifugo maeneo ya makaburi katika mji huo wa Sirari. Mwili wa mtu huyo ulikuwa
umeanza kuharibika.
Alisema kuwa mwili wa
mtu huyo, ulifanyiwa uchunguzi katika Hospitali ya Wilaya na kisha kukabidhiwa
kwa ndugu zake kwa maziko.
Friday, December 26, 2014
BUBU AFANYIWA UNYAMA, ABAKWA NA WATU WATANO
Mkazi wa
kitongoji cha Chingale, kijiji cha Mtakuja kata ya Temeke katika Halmashauri ya
mji wa Masasi mkoani Mtwara ambaye ni bubu, Asumini Fakihi amebakwa na watu
watano wasiojulikana na kumsababishia majeraha na kulazwa katika Hospitali ya
Mkomaindo mjini Masasi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara, Agustino Ollomi alisema juzi saa 1:00 usiku wa mkesha wa Krismasi katika kitongoji cha Chingale, mama huyo alivamiwa na watu hao wasiofahamika waliofanikiwa kumfanyia kitendo hicho na kutokomea kusikojulikana.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara, Agustino Ollomi alisema juzi saa 1:00 usiku wa mkesha wa Krismasi katika kitongoji cha Chingale, mama huyo alivamiwa na watu hao wasiofahamika waliofanikiwa kumfanyia kitendo hicho na kutokomea kusikojulikana.
HOTUBA KAMILI YA RAIS KIKWETE ALIPOZUNGUMZA NA WAZEE WA DAR ES SALAAM
HOTUBA
YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE,
AKIZUNGUMZA NA WAZEE WA MKOA WA DAR ES SALAAM,
TAREHE
22 DESEMBA, 2014
Shukrani
Mheshimiwa
Makamu wa Rais;
Mheshimiwa
Makamu Mwenyekiti wa CCM;
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam;
Viongozi
wa CCM Mkoa;
Viongozi
Wenzangu;
Viongozi
wa Dini;
Wazee
Wangu;
Wananchi
Wenzangu;
Nawashukuru sana wazee wangu wa Dar es Salaam,
kwa kukubali mwaliko wangu na kuja kuzungumza nami siku ya leo. Natambua kuwa taarifa ilikuwa ya muda mfupi, lakini
mmeweza kuja kwa wingi kiasi hiki.
Naomba radhi kwamba ilikuwa tukutane Ijumaa lakini kwa sababu zilizo nje
ya uwezo wangu, tukaahirisha mpaka leo. Asanteni sana kwa uvumilivu wenu.
Kama mjuavyo, kila ninapoomba kukutana nanyi
ninalo jambo au mambo muhimu kitaifa, ambayo napenda kuzungumza nanyi, na kwa kupitia
kwenu, taifa zima linapata habari. Leo
nina mambo mawili:
Wazee
Wangu;
Kwanza kabisa, nataka kurudia kuwashukuru
Watanzania wenzangu kwa moyo wenu wa upendo, mliouonyesha kwangu katika kipindi
chote cha matibabu yangu nikiwa nje na hata baada ya kurejea nchini. Kwa kweli
nina deni kubwa kwenu. Lazima nikiri kuwa, salamu zenu na taarifa kwamba
watu wamekuwa wananiombea uponyaji wa haraka na uzima zinanipa faraja kubwa na
kunitia moyo. Nadhani zimechangia sana
kuifanya afya yangu, kuendelea kuimarika kila kukicha. Bado sijawa “fit” kabisa lakini naendelea vizuri. Hali yangu ilivyo sasa sivyo
ilivyokuwa wiki iliyopita au siku niliporejea nchini.
Thursday, December 25, 2014
LOWASSA APONGEZA AMANI KISIWANI ZANZIBAR
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amewapongeza Wazanzibar na Serikali ya mseto visiwani humo kwa kudumisha amani.
Akitoa salamu zake Krismasi katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Mwanakwerekwe mjini Unguja alikokwenda kusali, Lowassa (pichani) ambaye ni Mbunge wa Monduli mkoani Arusha, alisema hali ya amani visiwani humo sasa ni shwari kabisa.
Akitoa salamu zake Krismasi katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Mwanakwerekwe mjini Unguja alikokwenda kusali, Lowassa (pichani) ambaye ni Mbunge wa Monduli mkoani Arusha, alisema hali ya amani visiwani humo sasa ni shwari kabisa.
WATOTO 53 WAONDOKA LEO KWENDA INDIA KWA MATIBABU
Watoto 53 wanaougua maradhi mbalimbali ya moyo wanaondoka nchini leo kwenda India kwa upasuaji ambapo wataagwa na Makamu wa Rais, Dk Ghalib Bilal.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mratibu wa magonjwa ya moyo katika Klabu ya Lions ya Dar es Salaam jana, Dk Rajni Kanabar (pichani), wagonjwa hao watatibiwa katika hospitali mbalimbali nchini India.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mratibu wa magonjwa ya moyo katika Klabu ya Lions ya Dar es Salaam jana, Dk Rajni Kanabar (pichani), wagonjwa hao watatibiwa katika hospitali mbalimbali nchini India.
Friday, December 5, 2014
MDAU WA BLOGU YA ZIRO99 AAMUA KUCHANA NA UKAPERA...
![]() |
Mzee Eusebio Kitosi, baba mzazi wa Elijah akitabasamu wakati wa sherehe ya Send-Off kwenye Ukumbi wa City Link, jijini Arusha Novemba 21, mwaka huu. Kulia ni mshenga, Bw David Koya. |
Subscribe to:
Posts (Atom)