Wafanyabiashara 30 wameporwa fedha taslimu na vitu vyao vya thamani vinavyokadiriwa kwa pamoja kuwa na thamani ya zaidi ya Sh milioni 20 wakati lori walilokuwa wakisafiria lilipovamiwa na majambazi.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Frednand Rwegasira alithibitisha kutokea kwa tukio hilo Julai 14 , mwaka huu, saa mbili usiku kwenye kona za Mlima Muze wilayani Sumbawawanga katika barabara ya Ntendo – Muze.
Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda huyo, wafanyabiashara hao walikuwa wakitokea mnadani kijijini Muze na walikuwa wakirejea mjini Sumbawanga wakitumia gari lenye namba za usajili T 714 BGZ lililokuwa likiendeshwa na Salum Said (36) mkazi wa eneo la Mazwi mjini hapa.
Akisimulia mkasa huo, Rwegasira alibainisha kuwa gari hilo aina ya Fuso likiwa na wafanyabiashara 30 lilipofika katika kona kali za Mlima Muze walikutana na majambazi sita wakiwa na mapanga, rungu na bunduki na kuziba barabara kwa mawe makubwa.
Baada ya kufyatua risasi hewani waliwalazimisha wafanyabiashara hao kusalimisha vitu vyao vya thamani zikiwemo simu za mkononi na fedha taslimu .
Alithibitisha kuwa hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa wala kupoteza maisha katika mkasa huo.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Frednand Rwegasira alithibitisha kutokea kwa tukio hilo Julai 14 , mwaka huu, saa mbili usiku kwenye kona za Mlima Muze wilayani Sumbawawanga katika barabara ya Ntendo – Muze.
Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda huyo, wafanyabiashara hao walikuwa wakitokea mnadani kijijini Muze na walikuwa wakirejea mjini Sumbawanga wakitumia gari lenye namba za usajili T 714 BGZ lililokuwa likiendeshwa na Salum Said (36) mkazi wa eneo la Mazwi mjini hapa.
Akisimulia mkasa huo, Rwegasira alibainisha kuwa gari hilo aina ya Fuso likiwa na wafanyabiashara 30 lilipofika katika kona kali za Mlima Muze walikutana na majambazi sita wakiwa na mapanga, rungu na bunduki na kuziba barabara kwa mawe makubwa.
Baada ya kufyatua risasi hewani waliwalazimisha wafanyabiashara hao kusalimisha vitu vyao vya thamani zikiwemo simu za mkononi na fedha taslimu .
Alithibitisha kuwa hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa wala kupoteza maisha katika mkasa huo.

No comments:
Post a Comment