Saturday, March 23, 2013

CHEKA TARATIBU...


Dereva wa bodaboda katika mbio bafuni akipiga kelele eti bafuni kuna mashetani. Wapangaji wenzake kwenye ile nyumba wakatoka kujua kulikoni, ndipo dereva huyo akaanza kuwaeleza huku akihema kwa hofu: "Jamani kila nikijimwagia maji kichwani hayafiki kwenye nywele." Badala ya kumwonea huruma, wapangaji wakaanza kucheka mpaka wanatokwa machozi. Kumbe jamaa alisahau kuvua kofia yake ya kuendeshea bodaboda! Duh...

No comments: