Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), limeondoa ombi lake la kuongeza bei ya nishati hiyo, ililowasilisha kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) Novemba mwaka jana na kufanya bei ya sasa iendelee kutumika.
Akizungumza jana, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Ewura, Titus Kaguo alisema kutokana na kuondolewa kwa ombi hilo la Tanesco, Mamlaka yake haijaidhinisha nyongeza nyingine ya bei.
Alifafanua kwamba bei zinazotumika sasa ndizo zitakazoendelea kutozwa.
“Watumiaji wa umeme wataendelea kulipa bei wanazotozwa sasa. Hakuna mabadiliko yaliyoidhinishwa,” alisema Kaguo.
Kwa mujibu wa tangazo la Ewura, kabla ya kuondoa ombi lake la dharura, Tanesco ilitaka iruhusiwe kupandisha bei ya umeme kwa wastani wa asilimia 155 kuanzia Januari mwaka jana.
Hata hivyo, kwa kuzingatia uchambuzi wake wa awali, Ewura ilitoa agizo la kuidhinisha bei ya dharura ya nishati hiyo kwa nyongeza ya asilimia 40.29 pekee.
Aidha, Mamlaka hiyo ilieleza katika tangazo hilo kuwa mtaalamu mwelekezi wa kujitegemea (AF-Mercados EMI) iliyomwajiri kutoka Hispania, alitoa mapendekezo ya bei za umeme kwa miaka mitatu.
Mtaalamu huyo alipendekeza nyongeza ya asilimia 33.8 kwa mwaka 2013, ikifuatiwa na ongezeko dogo la asilimia 0.85 kwa mwaka 2014 na asilimia 15.14 kwa mwaka 2015.
“Hata hivyo, kabla ya mchakato wa kukokotoa bei haujakamilika, Tanesco kupitia barua yake ya Januari 14, 2013, iliyopokewa na Ewura Januari 22, iliondoa maombi yake ya ongezeko la bei za umeme na kutaka za sasa ziendelee kutumika,” ilisema sehemu ya tangazo hilo.
Mwishoni mwa mwaka jana, wakati Tanesco ilipoelezea kusudio la kuongeza bei ya umeme, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alisisitiza kuwa bei hiyo haitapanda.
Katika maelezo yake, Profesa Muhongo alisema Tanesco haiwezi kupandisha bei ya umeme kwa kuwa fedha za uendeshaji wa mitambo yake, zinatolewa na Serikali.
Akizungumza jana, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Ewura, Titus Kaguo alisema kutokana na kuondolewa kwa ombi hilo la Tanesco, Mamlaka yake haijaidhinisha nyongeza nyingine ya bei.
Alifafanua kwamba bei zinazotumika sasa ndizo zitakazoendelea kutozwa.
“Watumiaji wa umeme wataendelea kulipa bei wanazotozwa sasa. Hakuna mabadiliko yaliyoidhinishwa,” alisema Kaguo.
Kwa mujibu wa tangazo la Ewura, kabla ya kuondoa ombi lake la dharura, Tanesco ilitaka iruhusiwe kupandisha bei ya umeme kwa wastani wa asilimia 155 kuanzia Januari mwaka jana.
Hata hivyo, kwa kuzingatia uchambuzi wake wa awali, Ewura ilitoa agizo la kuidhinisha bei ya dharura ya nishati hiyo kwa nyongeza ya asilimia 40.29 pekee.
Aidha, Mamlaka hiyo ilieleza katika tangazo hilo kuwa mtaalamu mwelekezi wa kujitegemea (AF-Mercados EMI) iliyomwajiri kutoka Hispania, alitoa mapendekezo ya bei za umeme kwa miaka mitatu.
Mtaalamu huyo alipendekeza nyongeza ya asilimia 33.8 kwa mwaka 2013, ikifuatiwa na ongezeko dogo la asilimia 0.85 kwa mwaka 2014 na asilimia 15.14 kwa mwaka 2015.
“Hata hivyo, kabla ya mchakato wa kukokotoa bei haujakamilika, Tanesco kupitia barua yake ya Januari 14, 2013, iliyopokewa na Ewura Januari 22, iliondoa maombi yake ya ongezeko la bei za umeme na kutaka za sasa ziendelee kutumika,” ilisema sehemu ya tangazo hilo.
Mwishoni mwa mwaka jana, wakati Tanesco ilipoelezea kusudio la kuongeza bei ya umeme, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alisisitiza kuwa bei hiyo haitapanda.
Katika maelezo yake, Profesa Muhongo alisema Tanesco haiwezi kupandisha bei ya umeme kwa kuwa fedha za uendeshaji wa mitambo yake, zinatolewa na Serikali.
No comments:
Post a Comment