![]() |
| Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira. |
Wananchi wenye hasira ambao wanadaiwa kuwa wakazi wa kijiji cha Sikaunga wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa wamevamia moja ya kambi iliyomo kwenye shamba lililonunuliwa na Nabii Josephat Mwingira wa Kanisa la Efatha Tanzania na kusababisha hasara ya zaidi ya Sh milioni 228.
Wakazi hao walifanya uharibifu mkubwa ambapo inadaiwa kuwa wameyateketeza kwa moto matrekta mawili makubwa aina ya New Holland pia nyumba kadhaa zilidaiwa kubomolewa na shehena ya mahindi kuchomwa moto wakimtaka mwekezaji huyo kuwaachia ardhi yao ambayo wanadai amewapora.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda amekiri kutokea kwa tukio hilo hivi karibuni ambapo watu 11 wanaotuhumiwa kuongoza wenzao kufanya uvamizi huo wamekamatwa na juzi walifikishwa mahakamani.
Inadaiwa kuwa, tangu Nabii Mwingira auziwe shamba hilo lililokuwa shamba la taifa la mifugo la DAFCO–Malonje lenye ukubwa ekari 10,000 na uongozi wa Halmashauri ya Manispaa miaka zaidi ya mitano iliyopita kwa bei ya Sh milioni 600 huku mwekezaji wake akituhumiwa kukiuka mkataba wa mauziano ya shamba hilo.
Hivyo, Serikali baada ya kupokea taarifa kuwa mwekezaji aliyenunua shamba hilo ameanza kulima mazao mbalimbali tofauti na mkataba wa ununuzi ambao unamtaka kufuga, iliuagiza uongozi wa mkoa wa Rukwa kuupitia upya mkataba huo ambapo tume tayari imeundwa pia imeshamaliza kazi yake.
Licha ya kukiukwa kwa mkataba huo, lakini pia watumishi wa shamba hilo wamekuwa wakituhumiwa kukamata na kutesa wananchi wanaishi pembeni mwa shamba hilo huku baadhi yao wakilalamika kukatwa masikio na wanawake kubakwa.
Kutokana na kadhia hiyo, kumeibuka uhasama baina ya watumishi wa Efatha waliomo ndani ya shamba hilo na wananchi wa vijiji jirani na shamba hilo.
Kwa mujibu wa baadhi ya wakazi kijijini humo ambao hawakuwa tayari majina yao kuandikwa gazetini wamedai kuwa wamevumilia kiasi cha kutosha, ndiyo maana wameamua kuchukua sheria mkononi, ikiwa ni jitihada za kumlazimisha mwekezaji huyo kuwaachia ardhi hiyo ambayo wanadai ni mali yao.
Akizungumzia sakata hilo la uvamizi uliofanywa katika kambi hiyo ya Sikaunga ndani ya shamba hilo Mchungaji Kiongozi Michael Meela wa Kanisa hilo la Efatha mkoani Rukwa alikiri kuwa mmiliki wa shamba hilo amepata hasara ya zaidi ya Sh milioni 228 kufuatia uharibifu huo uliofanywa na wananchi hao wenye hasira.
Akifafanua alisema kuwa uvamizi huo ulitokea mara tu baada ya Mbunge wa Jimbo la Kwela, Ignas Malocha kuhutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo na kuwahamasisha wananchi watumie nguvu ya umma kuyakomboa mashamba yao yaliyochukuliwa na mwekezaji huyo.
Hata hivyo, alikiri kuwa katika risala yao iliyoandaliwa na Mtendaji wa kijiji cha Sikaunga, R. Mkangwa kwa niaba ya Serikali ya kijiji hicho na kusomwa mbele yake pamoja kueleza changamoto kadhaa zinazowakabili, lakini pia wakazi wa kijiji hicho walitaka kujua hatima ya shamba hilo la Efatha kama watarudishiwa wao kwa sababu mwekezaji huyo amekuwa akiwatishia maisha yao.
Hata hivyo Mbunge Malocha amekanusha kuhusika na suala hilo, akisema taarifa hizo zimepikwa ili kumchafulia jina, akisisitiza hazina msingi wowote na kuongeza alikwenda hapo kufanya mikutano ya hadhara ili kuwahamasisha wananchi kujitokeza kutoa maoni ya Katiba mpya mbele ya tume ya kuratibu maoni hayo ambayo kwa sasa inafanya mikutano wilayani Sumbawanga.
Hata hivyo Kamanda Mwaruanda alipohojiwa na gazeti hili alikanusha na kueleza kuwa hakuna ushahidi wa kutosha kuwa mbunge huyo alihamasisha wakazi wa Sikaunga kutumia nguvu ya umma kuyakomboa mashamba hayo yaliyochukuliwa na mwekezaji Nabii Mwingira. Juhudi za kumpata Nabii Mwingira hazikufanikiwa.
Wakazi hao walifanya uharibifu mkubwa ambapo inadaiwa kuwa wameyateketeza kwa moto matrekta mawili makubwa aina ya New Holland pia nyumba kadhaa zilidaiwa kubomolewa na shehena ya mahindi kuchomwa moto wakimtaka mwekezaji huyo kuwaachia ardhi yao ambayo wanadai amewapora.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda amekiri kutokea kwa tukio hilo hivi karibuni ambapo watu 11 wanaotuhumiwa kuongoza wenzao kufanya uvamizi huo wamekamatwa na juzi walifikishwa mahakamani.
Inadaiwa kuwa, tangu Nabii Mwingira auziwe shamba hilo lililokuwa shamba la taifa la mifugo la DAFCO–Malonje lenye ukubwa ekari 10,000 na uongozi wa Halmashauri ya Manispaa miaka zaidi ya mitano iliyopita kwa bei ya Sh milioni 600 huku mwekezaji wake akituhumiwa kukiuka mkataba wa mauziano ya shamba hilo.
Hivyo, Serikali baada ya kupokea taarifa kuwa mwekezaji aliyenunua shamba hilo ameanza kulima mazao mbalimbali tofauti na mkataba wa ununuzi ambao unamtaka kufuga, iliuagiza uongozi wa mkoa wa Rukwa kuupitia upya mkataba huo ambapo tume tayari imeundwa pia imeshamaliza kazi yake.
Licha ya kukiukwa kwa mkataba huo, lakini pia watumishi wa shamba hilo wamekuwa wakituhumiwa kukamata na kutesa wananchi wanaishi pembeni mwa shamba hilo huku baadhi yao wakilalamika kukatwa masikio na wanawake kubakwa.
Kutokana na kadhia hiyo, kumeibuka uhasama baina ya watumishi wa Efatha waliomo ndani ya shamba hilo na wananchi wa vijiji jirani na shamba hilo.
Kwa mujibu wa baadhi ya wakazi kijijini humo ambao hawakuwa tayari majina yao kuandikwa gazetini wamedai kuwa wamevumilia kiasi cha kutosha, ndiyo maana wameamua kuchukua sheria mkononi, ikiwa ni jitihada za kumlazimisha mwekezaji huyo kuwaachia ardhi hiyo ambayo wanadai ni mali yao.
Akizungumzia sakata hilo la uvamizi uliofanywa katika kambi hiyo ya Sikaunga ndani ya shamba hilo Mchungaji Kiongozi Michael Meela wa Kanisa hilo la Efatha mkoani Rukwa alikiri kuwa mmiliki wa shamba hilo amepata hasara ya zaidi ya Sh milioni 228 kufuatia uharibifu huo uliofanywa na wananchi hao wenye hasira.
Akifafanua alisema kuwa uvamizi huo ulitokea mara tu baada ya Mbunge wa Jimbo la Kwela, Ignas Malocha kuhutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo na kuwahamasisha wananchi watumie nguvu ya umma kuyakomboa mashamba yao yaliyochukuliwa na mwekezaji huyo.
Hata hivyo, alikiri kuwa katika risala yao iliyoandaliwa na Mtendaji wa kijiji cha Sikaunga, R. Mkangwa kwa niaba ya Serikali ya kijiji hicho na kusomwa mbele yake pamoja kueleza changamoto kadhaa zinazowakabili, lakini pia wakazi wa kijiji hicho walitaka kujua hatima ya shamba hilo la Efatha kama watarudishiwa wao kwa sababu mwekezaji huyo amekuwa akiwatishia maisha yao.
Hata hivyo Mbunge Malocha amekanusha kuhusika na suala hilo, akisema taarifa hizo zimepikwa ili kumchafulia jina, akisisitiza hazina msingi wowote na kuongeza alikwenda hapo kufanya mikutano ya hadhara ili kuwahamasisha wananchi kujitokeza kutoa maoni ya Katiba mpya mbele ya tume ya kuratibu maoni hayo ambayo kwa sasa inafanya mikutano wilayani Sumbawanga.
Hata hivyo Kamanda Mwaruanda alipohojiwa na gazeti hili alikanusha na kueleza kuwa hakuna ushahidi wa kutosha kuwa mbunge huyo alihamasisha wakazi wa Sikaunga kutumia nguvu ya umma kuyakomboa mashamba hayo yaliyochukuliwa na mwekezaji Nabii Mwingira. Juhudi za kumpata Nabii Mwingira hazikufanikiwa.

No comments:
Post a Comment