CHEKA TARATIBU...

Wanandoa walibahatika kupata watoto wawili, John na Jose ambao ni watukutu ile mbaya. Kila jambo baya linalotokea mtaani basi lazima na wao wanahusika. Siku moja mama yao akasikia kuna jamaa mtaa wa jirani ni kiboko ya watoto watukutu. Akaenda kuonana naye na kukubaliana kazi ianze kesho yake. Yule jamaa akafika nyumbani pale na kukabidhiwa mtoto wa kwanza, Jose. Jamaa huyo akatumbua mimacho yake mikubwa kisha kwa sauti nzito akauliza, "Mungu yuko wapi?" Jose huku akitetemeka akabaki kimyaa. Jamaa akarudia, "Mungu yuko wapi?" Jose kimyaaa huku akichuruzika mkojo. Jamaa alipouliza mara ya tatu, Jose akatimua mbio na kujifungia chumbani kwao na kujifunika blanketi huku akitetemeka ile mbaya. Mwenzake kuona vile ikabidi aende kuuliza kulikoni? Hapo Jose huku akitetemeka akajibu, "Ndugu yangu safari hii limeibuka tatizo kubwa zaidi!" John akahoji, "Tatizo gani hilo?" Jose akajibu, "Mungu hajulikani alipo, na ninajua tu watasema ni sisi tumemficha!" Kasheshe...!"

No comments: