CCM YAPOTEZA KITI CHA UBUNGE IGUNGA...


                                     BREAKING NEWS!!!                                   
Habari zilizotufikia hivi punde, zinasema kuwa Mbunge wa Igunga kupitia CCM, Dk. Dalali Kafumu amepoteza kiti chake hicho kufuatia kushindwa katika kesi iliyofunguliwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Tabora na Mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Kashindye.
Kafumu alishinda kiti hicho katika uchaguzi mdogo kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Mbunge wa siku nyingi wa jimbo hilo, Rostam Aziz.
Mbali na Dk Kafumu, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Msimamizi wa Uchaguzi huo, Protace Magayane. Shauri hilo lilianza kusikilizwa rasmi Machi 26 na Jaji Mary Shangali.
Akizungumza kwa njia ya simu juzi, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya, Sylvester Kainda alisema Mahakama Kuu ilipanga hukumu hiyo isomwe jana lakini kwa kuwa ilikuwa Sikukuu ya Iddi, sasa inasomwa leo.
Wakili wa mlalamikaji, Profesa Abdallah Safari kwa njia ya simu yake ya mkononi alisema zaidi ya malalamiko 13 yaliwasilishwa katika Mahakama hiyo.

No comments: