Mgonjwa kazinduka baada ya kuwa amepata ajali mbaya sana. Mahojiano na daktari yaka hivi: MGONJWA: Kwanini niko hapa? DOKTA: Ulipata ajali mbaya iliyohusisha basi. MGONJWA: Enhe, ikawaje? DOKTA: Nina habari nzuri na nyingine mbaya. Ungependa kusikia ipi kwanza? MGONJWA: Nipe habari mbaya kwanza. DOKTA: Kwenye hiyo ajali miguu yako ilipondeka mno kiasi tumelazimika kuikata yote miwili. MGONJWA: Ooh inasikitisha sana. Enhe habari nzuri je? DOKTA: Kuna kijana amelazwa chumba cha pili amekupa ofa ya kukununulia kandambili! Duh...

No comments:
Post a Comment