Friday, May 31, 2013

KAKA SASA AWEKA SOKONI BARUA ALIZOTUMIWA NA RAIS BARACK OBAMA...

KUSHOTO: Moja ya barua hizo. KULIA: Malik Obama.
Mmoja wa kaka aliyechangia baba na Rais Obama sasa anauza karatasi mbili za barua alizopokea kutoka kwa ndugu yake huyo maarufu na kuziuza kwa Dola za Marekani 15,000 kila kimoja.

JICHO LA TATU...


Thursday, May 30, 2013

WATAKA FAO LA KUJITOA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII LISAIDIE WANACHAMA...

Jenister Mhagama.
Bunge limeibana Serikali likiitaka kuifanyia marekebisho sheria ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, ili pamoja na kuruhusu Fao la Kujitoa pia iruhusu mwanachama kuchukua sehemu ya mafao yake kulipia mkopo wa nyumba na sehemu nyingine kuandaa maisha yake baada ya kustaafu.

JICHO LA TATU...


MISHAHARA JUU, KUANZA KUTUMIKA RASMI JULAI...

Gaudentia Kabaka.
Hatimaye Serikali imetimiza ahadi yake ya kuongeza kima cha chini cha mishahara kama ilivyotolewa na Rais Jakaya Kikwete katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei Mosi.

Wednesday, May 29, 2013

MUHIMBILI YATANGAZA MAMIA YA NAFASI ZA MADAKTARI...

Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imetangaza mamia ya nafasi za ajira kwa idara tofauti, wakiwamo  madaktari bingwa na wauguzi wa vitengo, vikiwamo vya watoto na upasuaji wa moyo.

WATAPELIWA FEDHA, AJIRA KWA JINA LA QATAR AIRWAYS...

Moja ya ndege za Qatar Airways ikiwa safarini.
Watu kadhaa wametapeliwa na wanaojiita maofisa wa shirika la ndege la Qatar nchini, kwa kisingizio cha kuwapatia ajira ya uhudumu wa ndani ya ndege.

JICHO LA TATU...


UHAI WA MFALME ABDULLAH WA SAUDI ARABIA SASA WATEGEMEA MASHINE...

Mfalme Abdullah bin Abdulaziz al-Saud.
Mfalme wa Saudi Arabia kitabibu 'amefariki dunia' kwa takribani wiki nzima na yuko katika mashine za kumsaidia mapigo ya moyo, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchini humo.

MBUNGE ADAI MKURUGENZI MKUU WA NHC YUKO HATARINI KUUAWA...

Nehemiah Mchechu.
Baadhi ya watu wanaopinga juhudi za uongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kukabiliana na ubadhirifu, wamepanga kumwua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Nehemia Mchechu, imeelezwa.

Tuesday, May 28, 2013

MSANII MANGWAIR WA BONGOFLEVA AFARIKI DUNIA AFRIKA KUSINI...

Albert Mangwea.
Habari zilizotufikia zinasema kwamba msanii wa muziki wa kizazi kipya, Albert Mangwea 'Ngwair' amefariki dunia Afrika Kusini leo.

TRENI YA MWAKYEMBE 'YAONDOKA' NA MAISHA YA MCHUMI DAR...

Gari hilo baada ya ajali, Dar es Salaam jana.
Mchumi wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Elias Kitundu (39) amekufa papo hapo  huku mkewe Agness Msoka (37) na mtoto wao Samson Kitundu (17) wakijeruhiwa, baada ya gari lao kugonga ‘treni ya Mwakyembe’ jana alfajiri eneo la Moshi Baa  Ilala, Dar es Salaam.

MTWARA WASISITIZIWA KUWA 'WAPOLE' SUALA LA GESI ASILIA...

Moja ya mabango ya wananchi wa Mtwara wakati walipoandamana kupinga suala la gesi.
Wakazi wa Mtwara wameaswa kuzungumza lugha moja ya amani, utulivu na kujipanga vizuri ili nchi isije ikakosa fursa ya matunda yatokanayo na gesi asilia.

HUYU NDIYE KIKONGWE KABISA ANAYEISHI DUNIANI ALIYEZALIWA KARNE YA 19...

Jiroemon Kimura alipokuwa akisherehekea siku yake ya kuzaliwa hivi karibuni.
Japo bado kuna wanawake 21, lakini katika umri wa miaka 116 ni mtu wa mwisho aliye hai.

JICHO LA TATU...


BENKI NNE ZAIDI ZAJITOKEZA KUKOPESHA NYUMBA WANANCHI...

Ofisa Mtendaji Mkuu wa DCB, Edmund Mkwawa (kushoto) akisaini makubaliano na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Felix Maagi, baada ya kuingia makubaliano ya mkopo wa nyumba kwenye hafla iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Benki nne nchini zimeingia mkataba wa kukopesha nyumba zinazojengwa na kuuzwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)  hivyo kufanya idadi ya benki zinazotoa huduma hiyo kufikia 12.

MASHOGA WA KWANZA WA KIISLAMU KUFUNGA NDOA WAOMBA HIFADHI YA KISIASA...

Mashoga hao wakifungishwa ndoa kwenye ofisi ya msajili nchini Uingereza.
Wanawake wawili raia wa Pakistan wameweka historia kama Waislamu wa kwanza wa jinsia moja kufunga ndoa nchini Uingereza.

Monday, May 27, 2013

PROFESA TIBAIJUKA KWENYE KITI MOTO BUNGENI LEO...

Profesa Anne Tibaijuka.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anne Tibaijuka, leo anawasilisha hotuba yake ya bajeti kwa mwaka ujao wa fedha huku akikabiliwa na kibarua kizito cha kujibu hoja kuhusiana na migogoro ya ardhi, ubora wa majengo na masuala ya makazi. 

CHEKA TARATIBU...

Baada ya kumaliza maombi, Mchungaji akawaambia waumini wake wafumbe macho. Akainama na kuingiza mkono kwenye kapu la sadaka na kuiba pesa. Wakati akiinuka akakutana macho kwa macho na mzee mmoja aliyekuwa akiingia kanisani. Mchungaji akasema: "HERI YAKE YULE ASIYESEMA KUHUSU ALIYOYASHUHUDIA KWA MACHO YAKE…" Yule mzee akadakia: "…KWA MAANA ATAPATA MGAWO WAKE BAADA YA MISA KWISHA!" Duh...

KIKOSI MAALUMU CHAUNDWA KUPAMBANA NA WACHOCHEA VURUGU...

Advera Senso.
Polisi imetangaza kwamba imeunda kikosi maalumu kutoka Makao Makuu kwenda mikoani kushirikiana na makamanda kukamata watu wanaotuhumiwa kuchochea vurugu ikiwemo kutumia ujumbe mfupi wa simu za mkononi.

JICHO LA TATU...


MOTO WAWAKA BUNGENI MJADALA WA SERA YA TAIFA YA ELIMU...

Kikao cha Bunge kikiendelea mjini Dodoma.
Mjadala mkali umeibuka miongoni mwa wabunge wakati wa kujadili Sera ya Taifa ya Elimu na  Mafunzo iliyowasilishwa na Serikali baada ya kupinga tamko la kutaka umri wa kuanza elimu ya awali uwe miaka mitatu huku wengine wakiunga mkono.

Sunday, May 26, 2013

RAIS NKURUNZIZA WA BURUNDI AJA KUHUBIRI INJILI TANZANIA...

Rais Pierre Nkurunziza.
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza, anatarajiwa kuja nchini Agosti, kuhubiri Injili katika mkutano mkubwa wa Injili unaoandaliwa na Baraza la Makanisa ya Kipentekoste nchini (PCT), imefahamika.

HILI NDILO BAO LA ARJEN ROBBEN LILILOIPA BAYERN MUNICH UBINGWA WA ULAYA 2013...

  
Mabingwa wa soka nchini Ujerumani, Bayern Munich usiku wa kuamkia leo imetawazwa kuwa mabingwa wapya wa Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuwachapa Borussia Dortmund mabao 2-1 katika mechi ya fainali iliyowakutanisha miamba hao wawili wa Ujerumani kwenye Uwanja wa Wembley, nchini Uingereza. Hiyo ilikuwa fainali ya pili kwa Bayern Munich katika kipindi cha miaka mitatu, ambapo ilishuhudia mchezaji mwenye kasi ya ajabu Arjen Robben akiwapa raha mashabiki wake hao kwa kufunga bao la ushindi dakika ya 90 ya mchezo, baada ya kuwasononesha katika fainali zilizopita dhidi ya Chelsea. Katika fainali zilizopita, Robben alikosa penalti ambayo ilikuja kuigharibu timu hiyo kwa kukosa ubingwa.

NDEGE YENYE ABIRIA 297 YASINDIKIZWA NA NDEGE ZA KIVITA BAADA YA TISHIO LA UGAIDI...

Ndege hiyo ya Shirika la Pakistan International Airlines baada ya kutua salama.
Ndege za kivita za RAF zilipigania na kuingilia ndege iliyokuwa ikiwasili kutoka Pakistan juzi huku kukiwa na hofu za uwezekano wa kutekwa ndege hiyo.

CHEKA TARATIBU...

Ili kumdhibiti mkewe, jamaa mmoja akabuni mtindo ambao aliamini kwamba ni dawa tosha. Kila siku anapokuwa kazini mida ya mchana lazima apige simu, na mambo yakawa hivi.

WATANO WAFA AJALI YA BASI LA SUPER CHAMPION...

Kamanda David Misime.
Watu watano wamekufa papo hapo na wengine sita wamejeruhiwa, watatu wakiwa katika hali mbaya baada ya basi la Super Champion kugongwa na lori la mafuta eneo la Silwa, barabara ya Dodoma-Morogoro, mkoani Dodoma jana.

JICHO LA TATU...


BUNGE LAUNDA KAMATI KUCHUNGUZA YA MTWARA...

Spika Anne Makinda.
Spika Anne Makinda ameunda Kamati Maalumu ya Bunge kwenda kuzungumza na wananchi wa Mtwara kuhusu sakata la ujengwaji wa bomba la gesi asilia kutoka mkoani humo hadi Dar es Salaam.

UMOJA WA AFRIKA SASA WATANGAZA KUMTAMBUA RASMI MWALIMU NYERERE...

Hayati Mwalimu Nyerere.
Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, ni miongoni mwa Watanzania watatu wanaotarajiwa kutambuliwa na kuenziwa na Umoja wa Afrika (AU) rasmi kama Mwafrika Mashuhuri wa Kimajumui.

Saturday, May 25, 2013

MTOTO ALIYEZALIWA JELA AREJEA NA KUMTOA MAMA YAKE GEREZANI...

Kanhaiya Kumari (kushoto) akiwa na mama yake, Vijaya mara baada ya kuachiwa huyu.
Mtoto mdogo wa kiume wa mwanamke ambaye amedhoofika kwenye jela kwa takribani miaka 20 nchini India kwa upungufu wa Pauni za Uingereza 119 katika pesa za dhamana hatimaye amehakikisha kuachiliwa huru kwa mama yake.

MAHAKAMA YAMWACHIA HURU MTOTO RAMA 'MLA VICHWA'...

Ramadhani Suleiman 'Rama mla kichwa' (kulia) na mama yake mzazi, Khadija (katikati) walipofikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza.
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imemuachiwa huru Ramadhani Suleiman (Rama mla kichwa) aliyekuwa anakabiliwa na kesi ya mauaji, baada ya kubaini hana akili timamu.

JAJI ASHITAKIWA KWA KUIBA VIDHIBITI VYA DAWA ZA KULEVYA...

Paul Pozonsky.
Jaji mmoja ameshitakiwa kwa kuiba dawa za kulevya aina ya cocaine za ushahidi katika kesi alizoziendesha nchini Marekani.

HALI SHWARI MTWARA, WALIOKAMATWA SASA WAFIKIA 121...

Polisi wakidhibiti hali ya usalama Mtwara.
Mji wa Mtwara ambao kwa siku mbili kuanzia Jumatano wiki hii uligubikwa na vurugu kubwa kiasi cha kuibua hofu ya usalama wa wakazi wake, imerejea katika hali ya kawaida, ingawa shughuli za kiuchumi zimeonekana kuendelea kusimama.

JICHO LA TATU...


BRITISH AIRWAYS YATUA KWA DHARURA BAADA YA KULIPUKA INJINI ANGANI...

KUSHOTO: Moshi ukifuka kwenye moja ya injini za ndege hiyo angani. KULIA: Mafundi wakiichunguza injini hiyo mara baada ya kutua Uwanja wa Heathrow.
Abiria mmoja ameelezea jinsi 'moto mkubwa' ulivyokuwa ukionekana kutoka ndani ya ndege ya British Airways kabla kwa namna ya ajabu kulazimisha kutua kwa dharura kwenye Uwanja wa Heathrow jana.

SARAFU MOJA AFRIKA MASHARIKI KATIKA HATUA ZA MWISHO...

Samuel Sitta.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta,  amewasilisha hotuba ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka ujao wa fedha huku akieleza mikakati iliyowekwa katika uanzishwaji wa Umoja wa Fedha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaozifanya nchi wanachama kutumia  sarafu moja.

Friday, May 24, 2013

SHEHA AJERUHIWA BAADA YA KUMWAGIWA TINDIKALI ZANZIBAR...

Sheha Mohammed Omar Said `Kidevu’.
Matukio ya kujichukulia sheria mkononi yameendelea kujitokeza hapa, na juzi jioni Sheha wa Shehia (Kata) ya Tomondo Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja Mohammed Omar Said `Kidevu’ alivamiwa na watu wasiojulikana na kisha kummwagia tindikali ambayo imemjeruhi vibaya sehemu ya kifua na jicho la kulia.

WATU 91 WATIWA MBARONI KWA VURUGU ZA GESI MTWARA...

Wananchi wakiandamana muda mfupi kabla ya kuzuka vurugu hizo mkoani Mtwara.
Serikali imelaani vikali vurugu zilizotokea Mtwara juzi na imeapa kuwasaka waasisi wa vurugu hizo ndani na nje ya Mtwara na ndani na nje ya nchi ili waliohusika kupanga, kushawishi, kuandaa na kutekeleza vurugu hizo wafikishwe kwenye mkono wa sheria.

ACHOMA MOTO ZAHANATI KWA WIVU WA KIMAPENZI...

Kamanda Faustine Shilogile.
Sehemu ya jengo la Zahanati ya Digarama katika Wilaya ya Mvomero, imechomwa moto na mtu anayedaiwa kufanya hivyo kutokana na wivu wa mapenzi.

JICHO LA TATU...


Thursday, May 23, 2013

MWANASHERIA WA KIKE ALIYESHITAKIWA KWA KUFANYA UKAHABA NAYE AWASHITAKI WENZAKE...

Reema Bajaj.
Mwanasheria mmoja wa Illinois ambaye alipatikana na hatia ya kufanya ngono na mwanaume mmoja kwa malipo ya Dola za Marekani 100 anamshitaki aliyekuwa wakili wake wa utetezi na mawakili wengine wawili kwa madai ya kusambaza picha zake za utupu.

POLISI WALIOBAMBIKIA KESI YA FUVU LA MTU WAFUKUZWA KAZI...

Kamanda Faustine Shilogile.
Askari Polisi watatu  kati yao wawili wenye cheo cha Sajini na mwingine Koplo wa  Jeshi la Polisi mkoani Morogoro, wamefukuzwa kazi baada ya kufikishwa  mahakama ya Kijeshi wakituhumiwa kushirikiana na raia kumbambikia mfanyabiashara fuvu la kichwa cha binadamu.

MSICHANA ALIYEBAKWA NA WANAUME 20 SASA NI MJAMZITO WA MIEZI SABA...

Msichana huyo akiwa mbele ya nyumba inayodaiwa ilitumika kufanyia unyama huo.
Msichana mmoja wa Texas ambaye alikuwa na miaka 11 tu wakati alipobakwa na wanaume 20 kwa kipindi cha zaidi ya miezi mitatu mwaka 2010 amebainisha kwamba sasa ni mjamzito wa miezi saba akiwa na umri wa miaka 14.

VURUGU ZA MTWARA ZASITISHA BAJETI YA NISHATI NA MADINI DODOMA,,,

Polisi wakijipanga kudhibiti vurugu hizo Mtwara mapema jana.
Rais  Jakaya Kiwete amesema serikali itawakamata wanasiasa wanaochochea vurugu mkoani Mtwara kwa kisingizio cha kuzuia gesi isitoke mkoani humo.

MTANGAZAJI ANYONYA MAZIWA YA MAMA MMOJA 'LIVE' KWENYE TELEVISHENI...

Mtangazaji huyo akinyonya maziwa ya mama.
Mtangazaji wa Televisheni ya Uholanzi amewaacha midomo wazi watazamaji baada ya kunywa maziwa moja kwa moja kutoka kwenye matiti ya mam mmoja wakati wa kipindi chake cha wakati wa kipekee Jumamosi usiku.

UJENZI WA BOMBA LA GESI MTWARA-DAR ES SALAAM KUENDELEA...

Profesa Sospeter Muhongo.
Serikali imewasilisha bungeni hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka ujao wa fedha, huku ikisisitiza kuwa azma ya kujenga bomba la kusafirisha gesi ya asili kutoka Mtwara kuelekea Dar es Salaam  iko pale pale.

JICHO LA TATU...


BIBI HARUSI MTARAJIWA AFURUMUSHWA NA MBWA...

Bibi Harusi huyo akitokomea huku mbwa naye akimfuata kwa kasi.
Video ya mwanamke asiye na bahati aliyevalia gauni jeupe la harusi akiwa anafukuzwa na kushambuliwa na mbwa mchangamfu imetumwa kwenye mtandao.

Wednesday, May 22, 2013

MKENYA ALIYECHINJA WATU 400 KWA PANGA APEWA HIFADHI UINGEREZA...

John Thuo.
Muuaji ambaye aliua karibu watu 400 nchini mwake amepatiwa hifadhi ya kisiasa nchini Uingereza.