Tuesday, April 30, 2013

HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII MWAKA 2013/2014...


HOTUBA YA WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII
MHESHIMIWA BALOZI KHAMIS SUEDI KAGASHEKI (MB),
AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA
MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/2014

Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki akiwasilisha bungeni jana.
UTANGULIZI

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba kutokana na Taarifa  ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira iliyowasilishwa leo ndani ya Bunge lako Tukufu na Mwenyekiti wake Mhe. James Daudi Lembeli (Mb.), Bunge lako Tukufu sasa lipokee na kujadili Makadirio na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii na Taasisi zake kwa mwaka 2013/14.

Mheshimiwa Spika, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuendelea kuniwezesha kuiongoza Wizara hii yenye dhamana ya kusimamia Rasilimali za Maliasili na Malikale na kuendeleza Utalii. Nitajitahidi kwa kadri ya uwezo wangu, nikishirikiana na viongozi wenzangu ndani ya Wizara na wadau wote wa sekta hii kuhakikisha kuwa ulinzi na matumizi endelevu ya rasilimali hizo ni kwa manufaa ya Watanzania na dunia nzima. 

Mheshimiwa Spika, napenda kuishukuru kwa dhati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira kwa kuchambua na kujadili Taarifa ya Utekelezaji kwa mwaka 2012/13 na Mpango wa Bajeti wa Wizara yangu kwa mwaka 2013/14. Nalihakikishia Bunge lako Tukufu kuwa ushauri wa Kamati umezingatiwa.

Mheshimiwa Spika, napenda kuungana na wenzangu kutoa pole kwako Mheshimiwa Spika na kwa waheshimiwa Wabunge kutokana na kuondokewa na aliyekuwa mbunge mwenzetu Mhe. Salim Hemed Khamis Mbunge wa Chambani - CUF. Vilevile, natoa pole kwa familia za marehemu na watanzania wote kwa ujumla kutokana na majanga mbalimbali yaliyotokea nchini. Namwomba Mwenyezi Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema peponi. 

Mheshimiwa Spika, Hotuba yangu imegawanyika katika sehemu kuu tano. Sehemu ya kwanza ni Utangulizi; Sehemu ya pili inazungumzia Utekelezaji wa Mpango wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2010 - 2015; Sehemu ya tatu ni Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango kazi wa mwaka 2012/2013 ambao umezingatia utekelezaji wa  ahadi pamoja na maelekezo yaliyotolewa Bungeni na maagizo mbalimbali ya Viongozi Wakuu wa Serikali. Sehemu hii inazungumzia pia changamoto ambazo Wizara ilikabiliana nazo katika utekelezaji. Sehemu ya nne ni Mpango wa Utekelezaji na Malengo ya Wizara kwa mwaka 2013/2014, na sehemu ya tano ni  hitimisho ambapo bajeti inayoombwa kwa ajili ya utekelezaji wa mpango wa mwaka 2013/2014 inawasilishwa.

MASTAA JANA NA LEO...

Msanii wa Marekani, Ludacris alivyokuwa utotoni (kushoto) na muonekano wake wa sasa (kulia). Hakika siku hazigandi!

KESI YA ALIYEGONGA NA KUUA TRAFIKI MSAFARA WA RAIS YAAHIRISHWA...

KUSHOTO: Wasamaria wakifunika mwili wa trafiki huyo eneo la tukio. KULIA: Mtuhumiwa Jackson Simbo.
Kesi inayomkabili dereva, Jackson Simbo anayetuhumiwa kumgonga na kumuua askari wa Usalama Barabarani, imeahirishwa tena mpaka Juni 3, mwaka huu, kutokana na Wakili anayeendesha kesi hiyo kuumwa.

MZAHA WA LEO...

******************************
Ukiona kwenye familia yenu unakazaniwa sana kusoma ujue kwenye urithi haumo!
******************************
 

AFARIKI WAKATI AKITAKA KUWEKA REKODI YA DUNIA YA GUINNESS...

Roy akijaribu kujinasua kwa mikono baada ya kuwa amenasa nywele zake.
Mchezaji michezo ya hatari amefariki dunia katika harakati zake za kuweka rekodi ya dunia wakati akijaribu kuvuka juu ya mto mmoja kwa kutumia waya mwembamba ulioungwa katika nywele zake.

BABU WA KIKOMBE CHA LOLIONDO AIBUKIA NMB MOBILE...

Ofisa wa NMB tawi la Loliondo, Lembris Lesion, akimwelekeza juzi Mchungaji mstaafu Ambilikile Mwasapile jinsi ya kujiunga na NMB Mobile ili ‘kujisevia’ huduma zitolewazo kwa wateja wa NMB waliojisajili kwa kutumia NMB Mobile. (Picha kwa hisani ya NMB).

UDINI WAVURUGA MCHAKATO WA KATIBA MPYA...

Jaji Joseph Warioba.
Udini na siasa za uanaharakati vinaonekana kuanza kutafuna na kuathiri utamaduni wa Watanzania na mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya.

JICHO LA TATU...


BAJETI WIZARA YA MAJI YAPIGWA JEKI SHILINGI BILIONI 185...

Waziri wa Fedha, William Mgimwa.
Baada ya wabunge kugomea bajeti ya Wizara ya Maji kutokana na ufinyu wake, Serikali imekubali kuiongeza Sh bilioni 184.5.

GODBLESS LEMA ASHITAKIWA KWA UCHOCHEZI...

Godbless Lema.
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini hapa, akituhumiwa kuchochea kutenda kosa na kusababisha uvunjifu wa amani.

TANESCO YAELEMEWA NA MZIGO WA KAZI...

Makao Makuu ya Tanesco yaliyoko Ubungo, Dar es Salaam.
Shirika la Umeme (Tanesco) limetajwa kuzidiwa na mzigo wa kazi, kutokana na kuzalisha, kusambaza umeme na kukusanya mapato peke yake.

OMBI LA KUSIKILIZWA UPYA KESI YA JERRY MURO LATUPWA...

Jerry Muro.
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali ombi la kusikilizwa upya kwa kesi ya kuomba na kupokea rushwa ya Sh milioni 10, iliyokuwa inamkabili aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji (TBC), Jerry Muro na wenzake.

SPIKA MAKINDA AKANUSHA KUPOKEA RIPOTI YA JAIRO...

Spika Anne Makinda.
Spika wa Bunge, Anne Makinda, amekanusha ofisi yake kupokea rasmi ripoti ya kuchunguza tuhuma zinazomkabili  aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini David Jairo, na kuiacha iozee mikononi mwake.

KESI YA IDDI SIMBA HASARA YA BILIONI 2.3 ZA UDA KUENDELEA LEO...

Iddi Simba.
Kesi ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kulisababishia Shirika la Usafirishaji Dar es Salaam (UDA), hasara ya Sh bilioni 2.3 inayomkabili Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika hilo, Iddi Simba kuendelea kusikilizwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Monday, April 29, 2013

UAMUZI WA HOJA KESI YA MTANGAZAJI JERRY MURO KUTOLEWA LEO...

Jerry Muro.
Uamuzi wa hoja katika kesi ya kutaka kuomba na kupokea rushwa, iliyokuwa inamkabili aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji (TBC), Jerry Murro, unatolewa leo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

BINTI WA KAHABA ASHINDA FIDIA SHILINGI MILIONI 52 KWA MATESO YA UTOTONI...

KUSHOTO: Collette alivyo sasa. KULIA: Akiwa amebebwa na mama yake wakati akiwa na umri wa miaka mitatu.
Binti wa kahaba ameshinda fidia ya malipo ya Pauni za Uingereza 20,000 baada ya kushitaki ustawi wa jamii kwa kushindwa kumpeleka kwenye matunzo ya kudumu wakati alipokuwa mdogo ili kumnusuru kutoka kwa mama yake mwenye maneno makali.

MADAKTARI WALIOFUTIWA USAJILI WAANZA KUJITETEA...

Madaktari wakiwa katika moja ya mikutano yao wakati wa mgomo wao.
Madaktari 20 walioshiriki mgomo mwaka jana na kufutiwa usajili, kutokana na agizo la Baraza la Madaktari Tanganyika, wameanza kujitetea, lakini kupitia Chama cha Madaktari nchini (MAT).

JICHO LA TATU...


BABA AHOFIA MAISHA YA BINTI YAKE WA MIAKA MITANO ALIYEBAKWA...

Shambulio hilo limeibua hasira ya waandamanaji kote mjini Delhi.
Baba mzazi wa binti mwenye miaka mitano muathirika wa ubakaji amezungumzia hofu yake kwamba shambulio hilo la kikatili litamwacha binti huyo kutengwa na jamii kwa maisha yake yote yaliyobaki.

BAJETI KIPORO WIZARA YA MAJI YATINGA TENA BUNGENI LEO...

Kikao cha Bunge mjini Dodoma.
Mkutano wa 11 unaendeleo leo mjini Dodoma, ambapo Bajeti ya Wizara ya Maji iliyokwama kupitishwa baada ya wabunge kuigomea, inatarajiwa kuwasilishwa, ikiwa na  maboresho, hususani eneo la nyongeza ya fedha katika miradi ya maji.

MZAHA WA LEO...

******************************
Mbwa pia ana kichaa, lakini 
hawezi kuokota makopo dampo!
******************************

ASKARI MWANAUME ABAKWA NA WANAWAKE WANNE BAADA YA KUTEKWA...

Askari mmoja mwanaume anadaiwa kutekwa kisha kudhalilishwa kijinsia na wanawake wanne kwa karibu wiki moja kabla ya kupigwa mawe na kutupwa katikati ya milima.

WABUNGE SASA KUAMUA WATAKAOPATA MIKOPO ELIMU YA JUU...

Cosmas Mwaisobwa.
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza kuanza kupokea maombi ya mikopo mipya, huku ikiwaachia wabunge kuamua idadi ya wanufaika.

Sunday, April 28, 2013

MZAHA WA LEO...

************************************
Hata uwe na fujo kiasi gani, huwezi kugombea foleni kupima virusi ya ukimwi!
************************************

'MUUAJI' AUAWA KWA KUPIGWA MAWE MAKABURINI MBEYA...

Eneo la makaburi mkoani Mbeya.
Katika hali isiyo ya kawaida, mkazi wa Kitongoji cha Maweni, Kijiji cha Mkwajuni wilayani Chunya, Flavin Mwamosi Mwachuki (70) amepigwa hadi kufa na hatimaye kuzikwa kaburi moja na mtu anayedaiwa kumuua kishirikina.

CHEKA TARATIBU...

Mjukuu kamnong'oneza babu yake: "Naomba Shilingi 500!" Kwakuwa babu hakuwa na kitu akavunga kwa kusema: "Ninong'oneze sikio la huku, hilo bovu!" Mjukuu akamnong'oneza sikio jingine: "Naomba Shilingi 5,000!" Babu akahamaki: "Ohoo! Huku ndio sisikii kabisaaa. Bora kule ulikoomba Shilingi 500 nadhani ntasikia!" Kasheshe...

CHADEMA KUMBURUZA KORTINI RC ARUSHA KUHUSU SAKATA LA LEMA...

Magesa Mulongo.
Siku mmoja baada ya polisi mkoani kumkamata Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), sasa chama chake kinahaha kumnasua mbunge huyo  kwa kumgeuzia kibao Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo wakidai watamfungulia kesi mahakamani.

JICHO LA TATU...


MWANAMKE AREJESHEWA POCHI YAKE ILIYOIBWA ZAIDI YA MIAKA 20 ILIYOPITA...

Jeri Cox Chastain akikagua baadhi ya vitu vilivyokuwamo ndani ya pochi hiyo.
Vitu visivyouzika ambavyo mwanamke mmoja alipoteza kwa zaidi ya kipindi cha miaka 20 hatimaye vimerejeshwa kwake.

MKE WA RAIS KIKWETE ASOMESHA 'YATIMA FEKI'...

Mama Salma Kikwete.
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete amefichua kuwa, amewahi kupelekewa yatima `feki’ katika shule anayoisimamia ya Wama Nakayama iliyopo Rufiji mkoani Pwani, ambayo ni maalumu kwa watoto yatima na waliotoka katika mazingira magumu.

Saturday, April 27, 2013

MWANAUME ATIMULIWA KWENYE TAMASHA SABABU NI MZURI MNO...

   
Intaneti imejawa na tetesi kwamba huyu ni mwanaume ambaye ametimuliwa nchini Saudi Arabia kwa kuwa ni anavutia mno.

JICHO LA TATU...


MZAHA WA LEO...

***********************************
Mwanamke anayejua kwa uhakika alipo mumewe kila saa ni mjane, wengine wanadanganywa tu!
***********************************

UTAFITI WABAINI BANGI INAFAA KUONDOA KABISA MAUMIVU MWILINI...

Mmea wa bangi ukiwa shambani.
Bangi ikiwa katika hali ya vidonge inaweza kufanya kazi vizuri kabisa kuondoa maumivu kuliko ikiwa katika hali ya moshi na kuwa na madhara kidogo mno, wamesema wataalamu.

CHEKA TARATIBU...

Padri katika kanisa moja alitangaza kila muumini atoe sadaka kulingana na uzuri wa mke au mume wake. Wengi wakahamasika na kutoa hadi Shilingi 100,000. Lakini mwishoni kabisa mwa zoezi hilo, muumini mmoja akatoa Shilingi 500! Padri akamwita na kumuuliza: "Ina maana mkeo sio mzuri?" Jamaa akajibu: "Ukimuona naamini utanirudishia chenji!" Balaa...

AZUNGUKA MIGAHAWA 6,300 YA KICHINA, BADO HAWEZI KUTUMIA FIMBO ZA KULIA CHAKULA...

Mpenzi wa chakula cha Kichina amekula kwenye migahawa 6,300 tofauti na kusafiri kote Marekani akitimiza tamaa yake ya mapishi ya pande za Asia.

Friday, April 26, 2013

AKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUMNAJISI KUKU JIKE MUSOMA...

Kijana aliyejulikana kwa jina la Yusuph Bakari (28), Mkazi wa Kigera Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara, anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kunajisi kuku jike.

JICHO LA TATU...


MAGUFULI ASAINI MKATABA KUNUNUA KIVUKO BAGAMOYO-DAR ES SALAAM...

Dk John Magufuli.
Waziri wa Ujenzi, John Magufuli amesaini mkataba wa ununuzi wa kivuko chenye thamani ya Sh bilioni 7.9 chenye uwezo wa kubeba abiria 300 na mwendo wa kilometa 40 kwa saa kitakachokuwa kikifanya safari kati ya Bagamoyo na katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

WABUNGE WAUNGANA KUKATAA BAJETI WIZARA YA MAJI...

Wabunge katika kikao mjini Dodoma.
Bajeti ya Wizara ya Maji ya mwaka wa fedha 2013/14, iliyokuwa ipitishwe na Bunge jana, imekwama na kuahirishwa hadi Jumatatu.

CHEKA TARATIBU...

Wachungaji watatu walikutana wasimuliane matatizo yao ili waweze kuombeana. Wa kwanza akasema: "Jamani mimi tatizo langu ni wizi. Yaani kila nikimaliza ibada lazima nidokoe sadaka." Wa Pili akasema: "Tatizo langu mimi ni uzinzi. Yani kila nikiona msichana lazima nimtongoze." Wa tatu akaanza kulia. Wenzake wakamuuliza kulikoni naye akawajibu: "Jamani mimi tatizo langu umbea, yani siwezi kabisa kutunza siri. Na haya yote lazima nikamweleze Askofu!" Kasheshe...

BABA MTAKATIFU APONGEZA MUUNGANO TANGANYIKA NA ZANZIBAR...

Papa Francis I.
Viongozi wa mataifa mbalimbali akiwamo Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis, wametuma salamu za pongezi kwa Rais Jakaya Kikwete kwa niaba ya Watanzania, kwa kuadhimisha miaka 49 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. 

Thursday, April 25, 2013

MFUKO WA PENSHENI PSPF WACHUNGULIA KABURI...

Mkurugenzi Mkuu, Adam Mayingu.
Baada ya kukanusha kwa matangazo katika vyombo vya habari kuhusu hali mbaya ya Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), Mkurugenzi wake, Adam Mayingu, sasa amekiri kuwa na hali mbaya.

ASILIMIA 7 YA WATU WAZIMA TANZANIA WANA KISUKARI...

Asilimia saba ya watu wazima nchini wanaumwa kisukari huku theluthi moja kati yao, haina uelewa juu ya ugonjwa huo, jambo linalosababisha wafike hospitalini katika hali mbaya.

JICHO LA TATU...


MACHINGA WANAOINGIZA 40,000/- KWA SIKU SASA KUTOZWA KODI...

Baadhi ya wamachinga wakiwa kazini katika moja ya maeneo ya jiji la Dar es Salaam.
Serikali imeanza kuimarisha ukusanyaji mapato yake, kwa kutoza kodi pia wafanyabiashara wadogo wanaotembeza bidhaa zao kwa wateja barabarani,  maarufu kama Wamachinga.

NYUMBA ZA VIONGOZI WA CCM ZATEKETEZWA MOTO...

Mbunge wa Liwale, Faith Mitambo.
Nyumba zaidi ya saba za kuishi na nane za maduka pamoja na mifugo; vyote vikimilikiwa na viongozi wa CCM, akiwamo mbunge na madiwani wilayani Liwale, vimeteketezwa kwa moto na kuharibiwa na wahalifu.

Wednesday, April 24, 2013

MADAKTARI WALIOGOMA WAFUTIWA USAJILI WAO...

Baadhi ya madaktari na wauguzi wakati wa mgomo.
Madaktari 20 waliokuwa katika mafunzo kwa vitendo ambao walishiriki mgomo mwaka jana, wamefutiwa usajili kutokana na agizo la Baraza la Madaktari Tanganyika.

NAIBU SPIKA ATETEA MAWAZIRI KUHUSU UTORO BUNGENI...

Job Ndugai.
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, amesema mawaziri wanapokosekana ndani ya Bunge, haimaanishi hawako Dodoma, ila hawaonekani kwa kuwa kila mmoja anajitahidi kuweka mambo yake sawa katika mkutano huo wa Bajeti.

JICHO LA TATU...


UADILIFU WA KIFEDHA SERIKALINI WAIMARIKA...

Janeth Mbene.
Naibu Waziri wa Fedha, Janeth Mbene, amesema   uadilifu na uaminifu katika usimamizi wa fedha kwenye wizara na idara, umekuwa mkubwa kwa sasa na hiyo imesaidia mapato kuongezeka.

Tuesday, April 23, 2013

GODBLESS LEMA AIBWAGA TENA CCM MAHAKAMANI...

Godbless Lema.
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, kwa mara nyingine amewabwaga mahakamani wanachama wa CCM, waliokata rufaa katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2010, yaliyompa mbunge huyo wa Chadema ushindi.

BEI YA CHAKULA SASA KUPUNGUA, KAMPUNI 300 ZAJITOKEZA KUWEKEZA...

Vyakula mbalimbali katika meza sokoni.
Tatizo la ongezeko la gharama za maisha, linalotokana na ongezeko la bei ya chakula nchini, linatarajiwa kupungua baada ya kampuni takribani 300 za uwekezaji wa ndani na nje, kuonesha nia ya kuwekeza katika uzalishaji wa chakula nchini.

JALADA LA WILFRED RWAKATARE KUPELEKWA KWA DPP...

Wilfred Rwakatare.
Upelelezi  wa kesi inayomkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Rwakatare na Ludovick Joseph, umekamilika na jalada lake litapelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kwa hatua zaidi.

Monday, April 22, 2013

HII NDIO SIRI YA USHINDI YANGA, WACHEZAJI WAAHIDIWA MILIONI 100 WAKITWAA UBINGWA, ...

Kikosi cha timu ya soka ya Yanga kilichowasambaratisha maafande wa JKT Ruvu jana.
Timu ya Soka ya Yanga, jana imeiangushia kipigo cha mabao 3-0 JKT Ruvu na sasa kuhitaji pointi moja tu kuweza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.