Bei za mazao katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuu za Pasaka katika soko la Kariakoo
zimeongezeka kutokana na imani iliyojengeka kwa wafanya biashara kuwa uwezo wa
manunuzi unakuwa juu.
Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, jijini Dar es
Salaam, Florens Seiya alisema jana katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya
habari.
Seiya alisema kila inapofikia kipindi cha sikukuu kubwa za
kidini, imekuwepo desturi kwa wafanyabiashara nchini kupandisha bei za vitu sio
kwenye bidhaa tu hata nguo ama usafiri.
Alitaja bidhaa zinazopanda bei katika kipindi hiki kuwa ni
nyanya maji, vitunguu maji, pilipili hoho, vitunguu swaumu, tangawizi, karoti,
njegere, matunda mbalimbali na mchele. Alisema wastani wa ongezeko za bei hizo
ni Sh 5,000 hadi 100,000 kutokana na aina ya
mazao.
Alitolea mfano nyanya kwa kawaida hivi sasa boksi ni Sh 35,000
lakini kipindi hiki imekuwa Sh 40,000. Mchele gunia ni Sh 150,000 kipindi cha
sikukuu ni Sh 200,000. Tangawizi awali gunia liliuzwa Sh 200,000 hivi sasa ni
Sh 300,000.
No comments:
Post a Comment