MAMA ALIPA MADENI KWA KUUZA BIKIRA YA BINTI YAKE DOLA 500 TU...

KUSHOTO: Mama huyo, Rotana akionesh picha aliyopiga na binti yake huyo. KULIA: Dara Keo.
Raia wa Cambodia, Dara Keo wakati akiwa na miaka 12 mama yake mzazi, Rotana aliuza bikira ya mtoto wake huyo kwa tajiri ili apate pesa kulipa deni la kamari la marehemu mumewe.

Keo ambaye sasa ana miaka 17 ametoa siri hiyo sasa ambapo mama yake naye anafafanua "wanaonidai walikuwa wakinitishia maisha na kunifanyia vurugu na mimi sikuwa na uwezo wa kulipa".
Rotana mwenye miaka 62 kwa sasa anasema wakati huo alikuwa akipata dola moja ya Kimarekani kwa siku (Sh 1,600) na kubainisha "uoga, wasiwasi kuhusu madeni viliniumiza na mwishowe nilikata tamaa".
Kwa mujibu wa utamaduni wa dini ya Tao ya nchini humo, kufanya mapenzi na msichana bikira kunaongeza muda wa kuishi.
Awali Keo alipelekwa kwa daktari kuhakikisha kama kweli ana bikira ili kuondoa wasiwasi kwa mwanaume angenunua bikira yake kutokana na kwamba madalali wa bikira wamekuwa matapeli na kuwaweka bikira za bandia wasichana ili wapate fedha nyingi.
"Baada ya kupata uhakika wa kuwa na bikira nilipopelekwa kwa mwanaume aliyenunua bikira yangu na nilikaa huko kwa wiki nzima ambapo alikuwa akinibaka bila kutumia kondomu,"anasimulia Keo.
Mwanaume aliyenunua bikira ya Keo alikuwa mwanasiasa maarufu. Hata hivyo Keo na mama yake wamekataa kumtaja jina.
Keo anasema "aliniweka kwenye hoteli kwa wiki moja na kila siku alikuwa akija mara mbili hadi mara tatu na kunibaka, alikuwa akitumia nguvu na niliumia sana".
Baada ya wiki moja Keo aliachwa na michubuko na kulia sana na hakuweza kutembea na alipatwa na maumivu makali pindi alipokwenda haja ndogo kwa wiki mbili.
Keo ni miongoni mwa wasichana wadogo wengi ambao bikira zao zinauzwa nchini Cambodia kwa wanasiasa na polisi ambao ndiyo wateja wakubwa.
Familia zinazouza bikira hizo za watoto wao hupata dola za kimarekani 1,500 (Sh milioni 2.4) ambayo ni sawa na mshahara wa mkuu wa familia kwa miaka minne.
Kwa upande wa Rotana kutokana na kukabiliwa na madeni mengi na kutishiwa maisha aliuza bikira ya Keo kwa dola za kimarekani 500 tu(Sh 800,000).
Vannith Uy (41) anayefanya kazi kwa miaka mingi kama mpishi kwenye baa ijulikanayo Beer Garden ambapo wasichana huonesha sehemu ya maungo yao kuwavutia wanaume wanaotafuta wasichana bikira waweze kulala nao, anasema yeye mwenyewe aliuza bikira ya mtoto wake, Chamnan Sok wakati mwanawe huyo akiwa na miaka 18.
Anasema ameshashuhudia zaidi ya wasichana 50 wakifanya kazi kwenye baa hiyo waliouza bikira zao.
Licha ya Keo 'kuuzwa' na mama yake anasema alihuzunika kilichomkuta mama yake na kutishiwa maisha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha kulinda Haki za Watoto cha Cambodia, Nget Thy anasema watoto wa nchini humo wapo kwa ajili ya kuwafaidisha wazazi wao na si vinginevyo na hata haki za watoto hazitambuliki.

No comments: