Serikali
imefunguliwa kesi 1,179 na wananchi , mashirika na taasisi mbalimbali,
Bunge lilielezwa.
Kesi hizo ni
kati ya kesi 1,192 zilizofunguliwa mahakamani kuanzia mwaka 2010 hadi 2014.
Kati ya kesi hiyo Serikali imefungua jumla ya kesi 13 kama mshitaki.
Naibu Waziri wa
Sheria na Katiba Ummy Mwalimu aliliambia Bunge kuwa katika kipindi cha 2010
hadi 2014 jumla ya kesi zilizosikilizwa na kumalizika mahakamani ni 591.
Alisema kati ya
kesi hizo zilizosikilizwa, Serikali imeshinda kesi 511 na imeshindwa kesi 80.
Kesi ambazo bado zinaendelea kusikilizwa mahakamani ni 601.
Ummy alikuwa
akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Amina Abdulla Amour (Cuf) ambaye
alitaka kufahamu katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ni kesi ngapi za
kushitaki na ngapi za kushtakiwa kwa Serikali zimefunguliwa.
Mbunge huyo pia
alitaka kufahamu ni kesi ngapi Serikali imeshinda na zile ambazo imeshindwa.
Katika swali lake la nyongeza mbunge huyo alihoji kwa nini Serikali imeshtakiwa
mara nyingi na wananchi wake.
Katika majibu
yake ya nyongeza, Naibu Waziri alisema suala la wananchi kuishitaki Serikali ni
suala la kikatiba na Serikali haina mamlaka ya kuzuia mtu asiishitaki
mahakamani.
Alisema
inachofanya Serikali kwa sasa ni kuwaelimisha watendaji wake waamue na kutenda
mambo kwa kufuata sheria za nchi; kwani kesi nyingi dhidi ya Serikali kushitakiwa zinatokana na
watendaji kufanya maamuzi bila kufuata sheria.
Aliongeza kuwa
licha ya hatua hiyo, Serikali pia iko kwenye juhudi kuhakikisha inaimarisha
vitengo vya sheria katika taasisi, wakala na idara zake ili waweze kuwaelimisha
watendaji kuhusu masuala ya kisheria.
Pia
Mwalimu alisema Serikali inajitahidi kuwaelimisha wananchi wajue mipaka yao na
wajibu wao kwa Serikali ili kuepusha mivutano baina ya taasisi za serikali na
wananchi.
No comments:
Post a Comment