Hukumu
ya kesi ya kuomba na kupokea rushwa inayomkabili Mbunge wa Bahi (CCM), Omary
Badwel inatarajia kutolewa Aprili 29,
mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Hakimu
Mkazi, Hellen Riwa anatarajia kutoa hukumu hiyo baada ya Mahakama kusikiliza na
kupitia ushahidi pamoja na vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo na pande
zote mbili katika kesi hiyo.
Badwel
anadaiwa kati ya Mei 30 na Juni 2 mwaka 2012, katika maeneo tofauti Dar es
Salaam, alishawishi apewe rushwa ya Sh milioni nane kutoka kwa aliyekuwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Sipora Liana.
Inadaiwa
Badwel aliomba rushwa hiyo ili awashawishi wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu
za Serikali za Mitaa (LAAC), kupitisha hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya
Mkuranga mkoani Pwani.
Aidha anadaiwa Juni 2, 2012 katika Hoteli ya
Peacock, iliyopo Ilala, alipokea rushwa ya Sh milioni moja kutoka kwa Sipora.
Katika
utetezi wake, alidai hajawahi kuomba wala kupokea rushwa kutoka kwa Sipora na
kuiomba Mahakama itende haki kwa kuwa tuhuma dhidi yake, zilikuwa ni njama za
kumchafua.
Alidai
Sipora katika ushahidi wake mahakamani, alikiri kuwa “sijawahi kumuomba
rushwa pia kamati ninayodaiwa kutaka kuishawishi ina wajumbe 15 nisingeweza
kuwashawishi kwa kuwa sina mamlaka hayo”.
No comments:
Post a Comment