MKUU WA JESHI LA POLISI WA ZAMANI APATA PHD


Aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP mstaafu Said Mwema, amepewa Shahada ya Uzamivu (PHD) ya heshima iliyotolewa na Chuo Kikuu cha Omega Global cha Afrika ya Kusini.

Mwema amepewa heshima hiyo, baada ya chuo hicho kutambua juhudi ya kazi nzuri na uadilifu aliouonesha katika kipindi chake cha utumishi kwa Taifa.
Akizungumza katika dhifa hiyo Dar es Salaam jana, Jaji Mkuu wa Tanzania, Othuman Chande, aliyehudhuria alisema kiongozi bora ni yule anayekubalika kwa wenzake pamoja na jamii inayomzunguka.
“Kiongozi mzuri ni yule anayekubalika na wenzake pamoja na jamii yote inayomzunguka. Leo hii tupo hapa kwa sababu ya kazi nzuri aliyoifanya  IGP mstaafu Said Mwema, kazi yake nzuri Mungu ameiona, sisi tumeiona na hata wenzetu wa chuo hiki cha Omega pia wameiona na kutambua,” alisema.
Alisema uadilifu wa Mwema umewezesha Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wananchi, kupunguza vitendo vya kihalifu kwa kiasi kikubwa. 
Mwakilishi wa Chuo Kikuu cha Omega Global University, Professa Vusumuzi Sibiya, alisema huu ni wakati wa kutambua kazi nzuri ya kiongozi sio kusubiri hadi akifa.
“Tunatambua kazi yake ya uadilifu na jinsi alivyolitumikia si tuTaifa lenu bali hata sisi kwetu Afrika ya Kusini tunajivunia kazi yake maana taifa letu tunaiona Tanzania kama mzazi,” alisema Sibiya.

No comments: