BREAKING NEWS!!! ABIRIA WOTE WAHOFIWA KUFA AJALI YA BASI LA MAJINJA MAFINGA


Habari zilizotufikia zinasema kwamba watu wapatao zaidi ya 60 wanahofiwa kufariki dunia baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori katika eneo la Changarawe, Mafinga, wilayani Mufindi mkoani Iringa muda mfupi uliopita.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari, basi hilo mali ya kampuni ya Majinja lililokuwa likitokea mkoani Mbeya lilibamizwa na lori lililokuwa likitokea Dar es Salaam na katika harakati za dereva wa lori hilo kukwepa shimo barabarani, ndipo trela lake lilipoligonga basi hilo na kisha kupinduka na kulifunika kabisa.
Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kwamba kwa zaidi ya saa nzima hakuna sauti yoyote ya abiria iliyoweza kusikika na hivyo kuzua hofu kwamba huenda abiria wote wamepoteza maisha.
Wakati zoezi ya kuinua trela hilo zikiendelea, baadhi ya miili imeharibika vibaya huku baadhi yao ikiwa imepasuka vichwa kiasi kutisha kutazama.
Hadi chanzo chetu kinaondoka eneo la tukio, juhudi za kuondoa trela hilo zilikuwa zikiendelea kujaribu kunusuru endapo kuna majeruhi wowote ndani ya basi hilo.
Trafiki aliyekuwepo eneo la tukio ambaye hakutaka kutaja jina lake, alisema matumaini ya kukuta abiria walio hai ni madogo mno hasa kwa kuzingatia jinsi basi hilo lilivyopondeka vibaya sana.
Taarifa zaidi endelea kuperuzi ziro99blog.

No comments: