BAAMEDI 700 WATUNUKIWA VYETI VYA KIMATAIFA

Kampuni ya bia ya Serengeti imewatunuku vyeti wahudumu wa baa 700, walioshiriki mafunzo ya kimataifa ya Diageo Master Academy (MBA), yaliyoandaliwa kwa ajili ya kuwapa wahudumu hao ujuzi wa kufanya kazi kwa weledi.

Akitunuku vyeti hivyo kwa wahitimu hao jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Masoko wa Vinywaji Vikali, Stanley Samtu,  alisema mafunzo hayo yatawawezesha wahitimu hao kushiriki shindano la kitaifa na la kimataifa la Diaego Master Bar Academy.
“Tumewatunuku vyeti vya kimataifa vya MBA wahudumu wa baa kutoka mikoa kumi nchini baada ya kuhitimu mafunzo ya mwezi mmoja,” alisema.
Alisema mafunzo hayo yamewapatia ujuzi wa kuhudumia wateja, kuchanganya bia, kujua wajibu wao na aina ya vinywaji vikiwemo vya Barleys, Gordons, Grants,  John Walker, Guiness, Smirnoff na jamii zote za bia za Serengeti.
Alisema mafunzo hayo ya kimataifa kwa Afrika,  yalianza kutolewa  Februari 7, mwaka huu na kukamilika Machi 7 na  yaliyolewa na wakufunzi  kutoka Afrika Kusini.
“Mafunzo hayo yalifanyika katika mikoa  ya Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Morogoro na Mbeya,” alisema.
Kuanzia sasa wahitimu wote wameandikishwa katika shindano la kimataifa la Diageo Master Bar Academy na watahitajika kujibu maswali kwa njia ya simu ya mkononi.
Alisema shindano la kuwapata washindi  kumi wa juu (top ten),  litafanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa Aprili 2015  na kila mmoja atapatiwa zawadi ya dola 1,000 (Sh milioni 1.7) za Marekani.
Alifafanua kuwa mshindi wa jumla, atapata tiketi ya kushiriki shindano la kimataifa la ‘Diageo World Class’ litakalofanyika mwaka huu Johannesburg, Afrika Kusini.

No comments: